HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

Gwajima awajibu waliomtabiria kifo

Mchungaji wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amesema hatakufa hadi pale atakapotimiza lile lililomleta duniani.
Ameyasema hayo leo wakati wa ibada ya Jumapili kanisani kwake ikiwa ni siku chache baada ya mhubiri mmoja wa kimataifa kutabiri kuwa Gwajima atakufa ifikapo 2018.
“Mungu ndiye anajua siku saa na dakika ya kufa kwangu si mwanadamu,” amesema Gwajima

Askofu Gwajima akemea wanaoizungumzia nchi vibaya

Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amewaonya baadhi ya watu wanaoiongelea vibaya nchi akiwataka waache mara moja kwa kuwa wanachochea uvunjifu wa amani.
Askofu Gwajima amesema kinachotakiwa watu waizungumzie nchi vizuri kwa kuwa amani itakuwepo na uchumi wa nchi utaendelea kukua.
"Namkemea yule mtu ambaye anaiongelea vibaya nchi yetu huwezi ukawa unatoa kinywa kinachoashiria uvunjifu wa amani,"
"Huwezi kila siku unalaani kwa kuiongelea vibaya nchi yetu lazima nikemee ili nchi yetu iweze kuendelea kuwa na amani,"amesema Gwajima katika mahibiri kanisani kwake leo.

Maalim Seif akutana na Gwajima


Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad ameutua mgogoro wa chama che kwa Askofu Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima huku kiongozi huyo wa kidini akitangaza kuwa atamlipua Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba Jumapili ijayo.

Akizungumza Dar es Salaam jana wakati alipomtembelea Askofu Gwajima, Maalim Seif alibainisha kwamba amemweleza kiongozi huyo mambo mbalimbali ikiwemo suala la mgogoro ndani ya CUF, aliodai umesababishwa na Lipumba.

Alisema kuwa ameamua kwenda kwa Askofu Gwajima kumweleza hayo kwa sababu ni rafiki yake na hawajaonana siku nyingi lakini pia kiongozi huyo alikuwa haelewi mgogoro wa CUF umesababishwa na nani.

"Nimemweleza Askofu Gwajima mambo mengi hususani mgogoro wa CUF hivyo ataamua mwenyewe nini afanye kutokana na niliyomweleza,"alisema.

Aliongeza kuwa mbali na kwenda kwa Gwajima  pia ameshazungumza na viongozi wengine wa dini husuani ya Kiislamu.

Kwa upande wake, Askofu Gwajima alisema kuwa ameshafahamu chanzo cha mgogoro huo kwa kuwa Maalim ni rafiki yake wa siku nyingi lakini Lipumba hana urafiki naye.



"Mimi huyu ni rafiki yangu kwa hiyo nilitaka kujua Professa Lipumba anafanya nini kuvuruga CUF, hivyo nilitaka kujua Lipumba amepatwa na nini mpaka amevuruga chama chako na kiukweli mimi nilikuwa siufahamu vizuri huu mgogoro ila saizi Seif ameniambia kwa hiyo na mimi nataka nitafakari alichoniambia rafiki yangu ni ‘digest’ baada ya hapo nitajua nafanya nini” alisema Gwajima

Alipoulizwa kama watu watarajie chochote kutokea kuhusu CUF, Maalim Seif na Lipumba kwenye ibada Jumapili ijayo, Gwajima alijibu: “Kumbe mnajua, subirini Jumapili ifike nitamlipua na tutajua amekula maharage ya wapi.”

Askofu Gwajima amwomba Spika kuahirisha Bunge kwa ajili ya msiba

Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephath Gwajima amemtaka Spika wa Bunge kuahirisha kikao cha Bunge siku ya kuaga miili ya watoto waliofariki kwa ajali jana.
Amesema kama Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta aliamuru viongozi kusimama kuwakumbuka watoto hao itakuwa ajabu kwa Bunge kuendelea na vikao vya Bunge.
Amesema Spika akiahirisha Bunge kwa siku moja itatoa nafasi kwa wabunge hao kwenda Arusha ili kuomboleza pamoja.

Gwajima afutiwa mashtaka ya kutoa lugha chafu

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeifuta kesi ya kutoa lugha chafu inayomkabili Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Josephat Gwajima.
Hakimu Mfawidhi, Cyprian Mkeha aliifuta kesi hiyo leo chini ya kifungu cha 225 cha sheria ya Mwenendo wa Makosa ya jinai (CPA).
Kesi hiyo imefutwa baada ya Wakili wa Serikali, Joseph Maugo kueleza kuwa hawakuwa na shaidi na kuomba wapewe ahirisho.
Katika uendeshwaji wa kesi hiyo upande wa mashtaka uliita ushahidi mmoja kwa miezi 14.
Katika kesi hii, Gwajima anadaiwa kuwa kati ya Machi 16 na 25,2015 Tanganyika Packers Kawe alitumia lugha chafu na kumdhihaki Muhadhama wa Kanisa Katoliki Askofu Kardinal Polcarp Pengo.

VIDEO: GWAJIMA AWASILI CLOUDS NA KUWAPA POLE

Askofu wa kanisa la Ufufuo na uzima Joseph Gwajima amezungumza na waandishi wa habari wa Clouds Media Group na kusema kilichomfanya afike katika ofisi hizo ni kutoa pole kwa kuwa yeye ni sehemu ya sababu za uvamizi huo.
“Isingekuwa busara watu wavamiwe na mimi ni mhusika mkuu halafu nisije kutoa pole,” alisema
Hatua ya Gwajima imekuja baada ya tukio la kituo hicho kuvamiwa na mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda akiwa na polisi wenye silaha.
Gwajima amewasilia saa 4:00 asubuhi akiwa na msafara wa magari zaidi ya manne na walinzi wake takribani 30 na alipofika alipokelewa na Mkurugenzi wa vipindi na Uzalishaji Ruge Mutahaba na kufanya mazungumzo na waandishi wa habari na baadaye na uongozi wa kituo hicho.
Amewataka Clouds kuendelea na kazi zao za kawaida na kutaka suala hilo lisichukuliwe kisiasa huku akikisitiza kuwa Mkuu wa mkoa alikosea.

Gwajima amshambulia tena Makonda

Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima ametaja makosa ya kisheria yaliyomfanya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kukimbilia Afrika Kusini.
Akizungumza leo kanisani kwake, Ubungo, jijini hapa, Gwajima alidai kosa la kwanza la Makonda ni kughushi cheti ambacho kinaonyesha yeye ni Paul Makonda wakati akifahamu kuwa yeye ni Daudi Bashite.
“Kosa hilo kwa mujibu wa Gwajima ni kifungo cha miaka saba.Kosa jingine ni kula kiapo cha ukuu wa wilaya na ukuu wa mkoa akisema yeye ni Makonda wakati akijua yeye ni Bashite,” alisema
Gwajima alisema kosa la hilo la kula kiapo na cheti feki ni kifungo cha miaka mitatu.
Kosa jingine alisema ni kupokea mshahara na posho kwa jina la Makonda wakati akifahamu si yeye na kuongeza kuwa kosa hilo likithibitika atatakiwa kurudisha mishahara na posho zote alizochukua.

POLISI WATINGA NYUMBANI KWA GWAJIMA, AGOMA KUFUNGUA MLANGO

Jeshi  la Polisi kwa mara nyingine jana lilizingira nyumba ya Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, kwa kile lilichodai kuwa lilifika kufanya uangalizi.

Taarifa ambazo zimethibitishwa na Askofu Gwajima mwenyewe, zinaeleza kuwa polisi walifika nyumbani kwake wakiwa katika gari lao.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, polisi hao walipojaribu kutaka kuingia nyumbani kwa askofu huyo, walizuiwa mlangoni kwa sababu hawakuwa na kibali chochote wala maelezo yanayojitosheleza ya kutaka kukutana na kiongozi huyo wa kiroho.

Askofu Gwajima  jana alikiri polisi hao kumfuata nyumbani kwake na hivyo kulazimika kumtafuta wakili wake mara moja.

“Ni kweli walikuja wakiwa na gari la polisi, lakini walipofika nami nilimpigia mwanasheria wangu ambaye aliniambia tuwaulize wametumwa na nani na kama wana ‘search warrant’ (kibali cha kufanya upekuzi) au ‘arrest warrant’ (kibali cha kukamata),” alisema.

Askofu Gwajima alisema walipowauliza, walimtaja Afande Kingai kama ndiye mtu aliyewatuma, lakini hawakuwa na kibali chochote.

Kwa mujibu wa Askofu Gwajima, mwanasheria wake alifanya mawasiliano ya simu na Afande Kingai ambaye amepewa jukumu la kuwafuatilia wale wote waliotuhumiwa katika sakata la dawa za kulevya na kumuuliza sababu za kumfuata nyumbani.

“Afande Kingai amemweleza mwanasheria wangu kuwa walikuwa wamekuja kwa ajili ya ‘observation’ (uangalizi) tu, kwa hiyo mwanasheria wangu akasema kama ni ‘observation’ tu tusiwaruhusu kuingia ndani kwa sababu sheria ya hivyo hakuna, na sisi tumewazuia hawakuingia ndani,” alisema Askofu Gwajima.

Alipoulizwa kama kufuatwa kwake sasa na polisi kuna uhusiano wowote na kauli alizozitoa kanisani kwake hivi karibuni kuhusu elimu ya Paul Makonda ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Askofu Gwajima alisema huenda ikawa hivyo, lakini akasisitiza kuwa hana uhakika kwa sababu hajazungumza na askari waliomfuata.

Na alipoulizwa kama anadhani ujio huo pia unatokana na andiko ambalo linasambaa kwenye mitandao ya kijamii ambalo linasema Jumapili ijayo mwalimu aliyemfundisha mtu mmoja anayetajwa kwa jina la Bashite atakuwapo kanisani kutoa ushuhuda, Askofu Gwajima alikana akisema andiko hilo si lake.

Pamoja na hayo, Askofu Gwajima alikwenda mbali na kuhoji: “Hata kama ni kweli, sasa unaogopa mwalimu kuja… kanisani kwangu wapo watu wengi waliosoma naye Bashite kuanzia shule ya msingi na Sekondari ya Pamba… vyeti kama huna huna tu.”

Alipoulizwa haoni kauli yake kwamba Rais Magufuli ni tofauti kabisa na Makonda ilikuwa na nia ya kuwatenganisha viongozi hao, Askofu Gwajima alisema aliyemtaja kwa kumshambulia ni Makonda na si Rais.

“Aliyenitaja kwa kunishambulia katika sakata la dawa za kulevya ni Makonda na si Rais, mimi nimemuongelea Makonda, mimi ni mtumishi wa Mungu siwezi kuongozwa kwa ‘speculation’, si unajua hata Yesu alisema kama wewe huna dhambi basi uwe wa kwanza kushika jiwe,” alisema Askofu Gwajima.

Alipoelezwa kuwa katika mahubiri yake ni kama anaonekana kumshtaki Makonda, askofu huyo alisema: “Nilisema nitamshtaki kwa mahakama iliyo juu yake na nilisema Makonda aombe radhi, angekuwa mstaarabu baada ya sakata lile yeye mwenyewe angenipigia simu na kuniambia Gwajima nilikengeuka, lakini hajafanya hivyo.”
 
Pamoja na hayo, Askofu Gwajima alisema kwa aliyoyafanya Makonda tayari amekwishamsamehe na ndiyo maana hajampeleka mahakamani.

GWAJIMA, AZZAN WARIPOTI POLISI KITUO CHA KATI JIJINI DAR

Aliyekuwa mbunge wa Kinondoni, Idd Azzan ameripoti polisi leo asubuhi baada ya kuambiwa afanye hivyo.
Akiwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam, Azzan amesema baada ya kuripoti kama alivyotakiwa ameruhusiwa na kuelezwa kuwa aende katika kituo hicho baadaye.
Azzan amesema tangu watu waanze kumzungumzia kuhusiana na dawa za kulevya ni muda mrefu na hivyo amezungukwa na maadui wengi.
"Mimi tangu nianze kuzungumzwa sijaanza leo, wanasikiliza kwenye mitandao ya kijamii, hawajui mimi nina maadui wangapi ambao wananizunguka. Utakuta mtu tu ananitaja kwa chuki zake," amesema Azzan.
Amesema polisi walienda nyumbani kwake kupekuwa na hawakupata kitu chochote. “Nasubiri hiyo baadaye wataniambia kitu gani”
Wakati huo huo, Mchungaji Josephat Gwajima aliyedai angekwenda kuwaona wenzake waliosalia polisi, naye pia ameripoti polisi saa 10.46 asubuhi
Msaidizi wa askofu huyo amesema Gwajima ametakiwa kuripoti tena mchana huu.

VIDEO: ASKOFU GWAJIMA AFUNGUKA MAMO MAZITO LEO JUMAPILI BAADA YA KUTOKA POLISI


Baada ya jana Feb. 11 Askofu Josephat Gwajima wa kanisa la Ufufuo na Uzima kuachiwa na Polisi baada ya mahojiano yaliyodumu toka Alhamisi kituo cha Polisi kati Dar es salaam kufuatia sakata la dawa za kulevya, leo February 12 2017 akiwa kwenye Ibada kanisani kwake amesimulia.


"Nilienda moja kwa moja kwa Kamanda Sirro, nikamkuta na Manji, wakasema wewe na Manji tunakwenda kuwapima kwa mkemia mkuu wa Serikali, wale watu waliokuwa wanapima walikuwa wanapima kwa uwazi kabisa, wakapima vitu vyote majibu hamna chochote.

“Waliposema twende tukapime nilikua tayari, na mimi nilisema ndani yangu hata ukiona Pombe andika umeona dawa za kulevya, nikasema mimi sina tatizo twendeni nyumbani kwangu na mkikuta hata sigara andikeni ni dawa za kulevya, wakasachi na hawakukuta kitu”

==>Msikilize hapo chini akiongea

BREAKING NEWS: ASKOFU GWAJIMA AACHIWA JIONI HII

Baada ya kukaa polisi siku mbili akihojiwa na jeshi la polisi kutokana  listi ya watu wanaotuhumiwa na dawa za kulevya aliyoitaja Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda kwenye awamu ya pili ambayo ilijumuisha majina ya watu 65 akiwemo Askofu Gwajima.

Kutoka Kituo cha Polisi Kati Dar es salaam jioni hii, Askofu huyo wa kanisa la Ufufuo na Uzima Josephat Gwajima akiwa anatoka kwenye kituo hicho cha Polisi alikokua ameshikiliwa toka Alhamisi kufuatia kutajwa kwenye orodha ya Mkuu wa Mkoa Dar es salaam Paul Makonda.

Baadhi ya Waumini wa Kanisa lake walikua nje ya kituo hicho cha Polisi jioni hii na walisikika wakizungumza maneno mbalimbali ya kushukuru kama vile “Asante Yesu”

GWAJIMA NA YUSUF MANJI WAKESHA NA POLISI DAR

Ni kama shughuli zilisimama kwa saa kadhaa katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini Dar es Salaam wakati watu wawili maarufu nchini, Askofu Josephat Gwajima na mfanyabiashara Yusuf Manji waliporipoti kituoni hapo wakitaka wahojiwe.
Wawili hao, pamoja na wengine 63 walitakiwa waripoti kituoni hapo leo kwa ajili ya kuhojiwa kuhusu biashara ya dawa za kulevya, utumiaji au kama wana taarifa zinazoweza kusaidia Jeshi la Polisi kukomesha biashara hiyo haramu.
Wito huo ulitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ambaye juzi aliita waandishi ofisini kwake na kutaja orodha ya watu 65, wakiwemo wanasiasa, wafanyabiashara na viongozi wa dini.
Lakini, Manji, ambaye ni mwenyekiti wa moja ya klabu kubwa nchini ya Yanga, na Askofu Gwajima, anayeongoza kanisa la Ufufuo na Uzima, walienda kituoni hapo jana na walisikindikizwa na mashabiki na waumini wao.
Manji, ambaye ni Mwenyekiti wa Kampuni ya Quality Group, alifika kituoni hapo saa 4:54 asubuhi akiwa wa kwanza na alifika akiwa ndani ya gari aina ya Range Rover ya rangi nyeusi, akifuatana na watu wawili alioingia nao kituoni.
Dakika chache baada ya kuingia, Manji alitoka ndani na akawa anazungumza na watu waliovalia sare na wengine kiraia na baada ya muda aliingia tena ndani ya kituo.
Ilipotimu saa 6:10 mchana, Manji alitoka na kuonekana anaondoka, lakini alipofika getini askari walimfuata na wakarudi naye ndani.
“Mzuie, mzuie, mzuie,” alisikika mmoja wa polisi akisema wakati Manji akionekana kuondoka. Mfanyabiashara huyo alitii amri na kurudi kituoni.
Wakati Manji akiwa ndani ya kituo hicho, saa 7:33 mchana Askofu Gwajima aliwasili akiambatana na watu wapatao 10 walioonekana kuwa ni viongozi wa kanisa hilo na wote wakaingia kituoni.
Wakati viongozi hao wakiwa ndani, saa 8:00 mchana waumini takribani 20 walionekana kuwa ni wa kanisa la Ufufuko na Uzima walifika wakiwa wamevalia suti nyeusi. Waumini hao wa kike na kiume walikusanyika nje ya kituo hicho na kujipanga mstari nje ya geti la kuingilia kituoni, lakini askari waliwazuia na kuwataka kukaa mbali na eneo hilo ili wasubiri hatma ya askofu wao.
Taarifa kutoka ndani ya kituo hicho zilisema kuwa watuhumiwa hao hawakutoa maelezo yoyote kwa sababu Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Siro alikuwa kwenye kikao ofisini kwa Makonda.
Eneo hilo pia lilifurika mashabiki kadhaa wa klabu ya Yanga waliokuwa wakifuatilia hatma ya Manji.
Baada ya ukimya uliotawala eneo hilo huku waandishi wa habari wakifuatilia matukio hayo kwa mbali kutoka nje, Manji na Gwajima walionekana wakitoka kituoni saa 10:27 jioni na wote kupanda gari dogo jeupe aina ya Toyota Land Cruiser na kuondoka.
Baada ya kurejea, Kamanda Siro aliwaambia waandishi wa habari kuwa hangeweza kuzungumzia suala hilo jana.

Gwajima amvaa Makonda
Awali, Gwajima alizungumza na waumini wa kanisa lake na kumuomba Rais John Magufuli ambadilishe kazi Makonda, akimsifu kuwa ni mchapakazi, lakini hawezi kazi ya utawala kutokana na ama kutokomaa au kutokuwa na uzoefu.
Akijibu maswali ya waandishi wa habari baada ya kuongea na waumini, Askofu Gwajima alisema kitendo cha Makonda kumtaja hadharani akihusishwa na dawa za kulevya kinaonyesha ana nia ovu na kanisa hilo.
“Sisemi Magufuli amfukuze kazi, hapana, Makonda ni jasiri na mchapakazi, lakini kazi ya utawala, kuongoza watu imemshinda atamharibia Rais,” alisema.
“Usalama wa Taifa watakuwa wanafahamu kama Askofu Gwajima anahusika au hahusiki kwa namna moja ama nyingine na dawa za kulevya. Kitendo cha Makonda kunitaja kupitia vyombo vya habari kinaonyesha ana chuki na mimi na hajui masuala ya utawala.
“Hivi hafahamu kwamba nina waumini zaidi ya 70,000, nina makanisa 400 na maaskofu 25. Ameshindwa vipi kuchunguza na kuniita hadi atangaze kwenye vyombo vya habari?”
Alisema sababu nyingine ya kutaka Rais Magufuli ambadilishe kazi ni kutokana na viongozi wa Serikali hivi sasa kufanya kazi kwa hofu.
“Mawaziri, wakuu wa mikoa wanaogopa wanaposikia sauti ya Makonda, wanadhani kila anachofanya ametumwa na Rais Magufuli. Si kweli anawatisha tu huyo,” alisema.
“Magufuli amekuwa akimpongeza Makonda kwa kazi nzuri anazozifanya, lakini si kila anachofanya anatumwa na Rais.”
Aliwataka viongozi wengine kutokuwa na hofu na Makonda kwa kuwa anachokifanya ni kuwatisha wenzake kwa kutumia jina la Rais.
“Nimekuwa nikijiuliza sifahamu chochote kuhusu dawa za kulevya, huyu Makonda ananipakazia hivi ili kumfurahisha nani?” alihoji.

Wivu na chuki binafsi
Askofu Gwajima alisema hivi karibuni walikuwa kwenye mechi ya soka kati ya viongozi wa dini na wa serikali ambayo yeye na Makonda walicheza timu moja.
“Kwa kuwa nilichelewa, niliamua kutumia helikopta hadi uwanjani lakini wakati tukicheza mpira, Makonda alikuwa ananiangalia kwa jicho la chuki mpaka nikawa nashangaa. Sasa leo nimeamini kijana mwenzangu ana chuki binafsi,” alisema.
Alisema Makonda anatakiwa kufahamu kwamba si kila anayefanikiwa kiuchumi anakuwa anajihusisha na dawa za kulevya.
Askofu Gwajima alisema ana shahada ya uzamivu ya filosofia (PhD) na hulipwa dola 1,000 za Kimarekani (sawa na zaidi ya Sh2.2 milioni) kwa saa anapofanya uhadhiri vyuoni.
“Nimetoka Japan ambako nilikaa miezi mitatu, unadhani nitachuma kiasi gani?” alihoji.
“Sasa kijana mwenzangu Makonda asiwe na chuki binafsi, bali angeniuliza unapataje fedha, lakini si kuvunja heshima yangu niliyoijenga siku nyingi.”
Alisema hajawahi kunywa pombe, kuvuta sigara na wala hajui dawa za kulevya zikoje.

Makonda kanisani
Gwajima alisema Makonda akiwa na spika wa zamani wa Bunge, Marehemu Samuel Sitta waliwahi kufika kanisani kwake kuombewa.
“Nilimkaribisha Makonda madhabahuni na akazungumza na waumini akisema ni heshima kubwa kupata nafasi ile na tulisali pamoja. Je, kipindi kile hakuhofia kuwa nahusika na dawa za kulevya?” alihoji.
Nisirudishwe kwa Lowassa
Alipoulizwa kama patashika anazopata zinatokana na kuwa karibu na aliyekuwa mgombea wa Chadema, Edward Lowassa, mchungaji huyo alisema anashangaa kuona anarudishwa kwa mtu aliyeona anafaa kuwa Rais.
“Wakati wa uchaguzi kila mtu aliona mtu aliyefaa kuwa Rais na mimi niliona Lowassa ndiye aliyekuwa anafaa kuwa Rais,” alisema Gwajima.
“Lakini bahati nzuri Lowassa hakuchaguliwa na badala yake amechaguliwa Magufuli ambaye anafanya kazi ambayo ingeweza kufanywa na wapinzani. Kwa hiyo namuunga mkono. Nashangaa kwamba mimi namuunga mkono, lakini wanazidi kunirudisha kwa yule.
“Mimi si mnafiki. Wakati Rais Jakaya Kikwete akiwa madarakani niliikosoa sana Serikali yake, lakini nashukuru sasa Magufuli anafanya kazi zilizotarajiwa na Watanzania wengi, ndiyo maana mara nyingi nampongeza.”

KESI YA GWAJIMA KUSIKILIZWA TENA SEPTEMBA

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


 Askofu Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Tanzania, Josephat Gwajima, akitoka katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam jana, kusikiliza kesi inayomkabili ya kutoa lugha ya matusi na kukutwa na silaha. (Na Mpiga Picha Wetu).

Na MwandishiWetu

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, imeahirisha kesi ya kutoa lugha ya matusi  na kukutwa na silaha zinazomkabili Askofu Mkuu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima Tanzania, Josephat Gwajima, kutokana na hakimu anayesikiliza shauri hilo kutokuwapo.

Kesi hiyo iliahirishwa leo na Hakimu Mkazi Magreth Bankika, ambaye alisema kesi hiyo itaendelea kusikilizwa Septemba 2, mwaka huu.

Askofu Gwjima alikuwapo mahakamani wakati kesi hiyo ikiahirishwa, ikiwa ni mara yake ya kwanza tangu iliporipotiwa kuwa ni mgonjwa.

Askofu Gwajima alifika mahakamani hapo saa 2:00 asubuhi akiongozana na walinzi pamoja na wafuasi wake.

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Shadrack Kimaro, aliieleza mahakama kuwa shauri hilo limetajwa kwa ajili ya kusikilizwa na shahidi mmoja alikuwapo, lakini wamepata taarifa kuwa hakimu anayesikiliza shauri hilo hayupo, hivyo kuiomba mahakama kupangiwa tarehe nyingine.

Hakimu Bankika aliahirisha kesi hiyo hadi Septemba 2, mwaka huu itakapoendelea kusikilizwa.

Katika kesi hiyo ambayo Askofu Gwajima anatetewa na Wakili Peter Kibatala, anadaiwa kati ya Machi 16 na 25, mwaka huu katika viwanja vya Tanganyika Packers, vilivyopo Kawe, jijini Dar es Salaam, alitoa lugha ya matusi dhidi ya Askofu wa Kanisa Katoliki, Mwadhama Policarp Kardinali Pengo, jambo ambalo lingeweza kusababisha uvunjifu wa amani.

Hivi karibuni Askofu Gwajima akiwa nje ya nchi, Jeshi la Polisi lilitangaza kumsaka kwa ajili ya kumhoji kutokana na mahubiri aliyoyatoa Juni 11, mwaka huu kanisani kwake Ubungo.

Katika mahubiri hayo yaliyosambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii, askofu huyo alisikikika akiukosoa utendaji kazi wa Rais mstaafu Jakaya Kikwete na kumtaka Rais John Magufuli kumchukulia hatua kutokana na mabaya aliyoyafanya katika utawala wake.

Alipojea nchini alikamatwa na polisi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam na kuhojiwa kwa saa kadhaa na kuachiwa.

ASKOFU GWAJIMA AMJIBU KATIBU MKUU WA ZAMANI WA CCM, YUSUF MAKAMBA ALIYEMUITA MUONGO

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.

Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima amemjibu katibu mkuu wa zamani wa CCM, Yusuf Makamba aliyemtuhumu kuwa ni mwongo akisema leseni yake ni ya kuendesha magari makubwa na siyo vibajaji na maguta. 

Akihubiri katika kanisa lake jana, Gwajima bila kutaja jina la Makamba, alisema: “Siwezi kushughulika na vigari vidogovidogo nyie mnanifahamu, mimi nina leseni ya kuendesha semi trailer …nadhani mmenielewa,” alisema huku waumini wake wakimshangilia. 

Juzi, Makamba aliwaeleza wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalumu wa CCM kuwa Askofu Gwajima ni kiongozi wa dini lakini ni muongo na kuwa uongo wake unawaudhi hata waumini wake ambao ni wanachama wa chama hicho. 

Alisema Gwajima amekuwa akisema uongo kuwa Rais mstaafu, Jakaya Kikwete hataki kuachia madaraka ya uenyekiti wa chama hicho, kitu ambacho Rais huyo mstaafu alikanusha akisema ni yeye alikwenda kumshawishi Dk John Magufuli kuchukua nafasi hiyo kabla ya muda wa uliopangwa kikatiba. 

Katika mahubiri hayo, Gwajima pia alisema mafunzo aliyoyapata tangu akiwa mdogo ni kuogopa kugombana na watu wa aina tatu, walevi, wazee na wagonjwa. 

“Baba yangu alinifundisha nisigombane na walevi, wazee na wagonjwa kwani ukimpiga kidogo mtu wa aina hiyo anaweza kufa,” alisema Gwajima. 

“Hata nyie waumini wangu nawaomba msigombane na watu wa aina hiyo kwani mnaweza kupata matatizo,” alisema. 

Kiongozi huyo aliongoza mamia ya waumini wake kumuombea Rais Magufuli kwa kushinda uenyekiti wa CCM akisema kofia hizo mbili zimempa meno ya kung’ata na zitamwongezea kasi ya kutatua matatizo ya wanyonge nchini.

Rais Magufuli juzi alichaguliwa kuwa Mwenyekiti wa CCM baada ya kupata kura zote 2,398 alizopigiwa na wajumbe wa mkutano huo. 

Kutokana na ushindi huo, Gwajima alisema Magufuli amepewa meno ya `kung’ata’ kila upande tofauti na alipokuwa na kofia moja ya urais. 

Alisema kwa muda mfupi aliokaa madarakani, elimu ya msingi na sekondari zimeanza kutolewa bure kitendo ambacho maskini na wanyonge wa nchi hii wameanza kuuona mwanga. 

Alisema ataendelea kumwombea Magufuli kwa sababu kazi anazozifanya zinawanufaisha wanyonge na maskini ambao kwa muda mrefu walipuuzwa katika nchi yao.

“Kuchaguliwa kwake kuwa mwenyekiti ni zawadi kwetu Watanzania, tuendelee kumwombea kila siku ili aendelee kufanya kazi yake kwa ufanisi zaidi,” alisema. 

Alisema nafasi hiyo mpya itamwezesha kupambana na rushwa tatizo ambalo ameonyesha kuwa `atalivalia njuga’ hata ndani ya chama hicho. 

Mbali na Rais Magufuli, Gwajima aliwaombea pia Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, mawaziri na Spika wa Bunge kwamba Mungu awalinde ili wamsaidie Rais kutekeleza majukumu yake. 

Kwa mwezi mzima, Askofu Gwajima amekuwa akitafutwa na Polisi baada ya kusambaa kwa sauti inayosikika kama yake ikitaka Rais mstaafu Kikwete afikishwe mahakamani kwa makosa yote yaliyofanyika katika utawala wake. 

Katika mkanda huo, sauti hiyo inadai baadhi ya viongozi wa CCM wametuma watu mikoani kupiga kampeni ya kutaka Magufuli asipewe uenyekiti ambao umekuwa ukishikiliwa na Kikwete. 

Baada ya sauti hiyo, Gwajima aliondoka nchini kwenda Japan lakini Polisi waliendelea kumsaka hadi Julai 12 walipomkamata katika Uwanja wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA), aliporejea. Alihojiwa na kuachiwa siku hiyohiyo.