HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

Wanafunzi 2,348 washinda rufaa za mikopo ya elimu ya juu

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetuma vyuoni majina ya wanafunzi 2,348 walioshinda rufaa zao na inaendelea kukamilisha malipo ya mikopo yao.
Hatua hiyo ya bodi ya mikopo imekuja baada ya wanafunzi hao kushinda katika rufaa zao za mikopo ya elimu ya juu walizokata tangu Novemba Mosi mwaka jana na kuhitimishwa Januari 31, mwaka huu.
Taarifa ya bodi hiyo iliyotolewa leo (Jumatano) imewaarifu waombaji na umma kwa ujumla kuwa zoezi hilo limefungwa rasmi hadi hapo litakapotangazwa tena katika mwaka ujao wa masomo.

Tucta yawakingia kifua wadaiwa HESLB

Rais wa Tucta, Tumaini Nyamhokwa

Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta) limetoa siku 14 kwa Serikali kuwarejeshea wafanyakazi fedha za mikopo ya elimu ya juu wanazokatwa kimakosa vinginevyo watafanya uamuzi mgumu
Akizungumza leo (Jumanne) Rais wa Tucta, Tumaini Nyamhokwa amesema wafanyakazi hao waliingia mkataba na Bodi ya Mikopo ya wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) ya kukatwa asilimia nane.
Amesema baada ya sheria mpya iliyopitishwa Agosti 2016 imebadilisha na sasa wanakatwa asilimia 15 bila kujali walikopa lini mikopo hiyo.

MAJINA YA WANAFUNZI WALIOPATA MKOPO BAADA YA KUKATA RUFAA BODI YA MIKOPO 2016/2017

Bodi ya Mikopo imetangaza majina ya wanafunzi waliofanikiwa kupata mkopo baada ya kukata rufaa.


BODI YA MIKOPO YAONGEZA KIWANGO CHA MAKATO KWENYE MISHAHARA YA WATUMISHI

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.





WATANZANIA WANAOSOMA NCHINI CHINA WATOSWA NA BODI YA MIKOPO

Watanzania waliopata ufadhili wa kusoma nchini China, hawatapata mikopo baada ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) kuwaondoa kwenye orodha ya wanufaika. 

Taarifa iliyotolewa na HESLB, ikijibu Ubalozi wa Tanzania nchini China, kuhusu madai ya kuchelewa kwa fedha za mikopo kwa wanafunzi wanaosoma nchini humo imeeleza kuwa hatua hiyo inatokana na maelekezo ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwamba wanafunzi wote wanaopata ufadhili kutoka nchi rafiki watajitegemea ikiwamo gharama za tiketi za ndege.

Barua hiyo ya Desemba 20, 2016 iliyomnukuu Mkurugenzi Mtendaji wa bodi hiyo, Abdul Razaq Badru inaeleza kuwa mwaka huu wanafunzi hao hawatanufaika na mikopo kama ilivyokuwa ikitolewa miaka ya nyuma.

Jana, akizungumza na waandishi wa habari, Badru aliitambua barua hiyo huku akisita kutolea ufafanuzi wake kwa madai ilikuwa ni majibu kwa wanafunzi hao wa China.

Hata hivyo, alisema endapo kutakuwa na madai kutoka kwa wanafunzi hao watalazimika kutolea ufafanuzi.

Akizungumzia suala hilo Naibu Waziri Elimu, Stella Manyanya alisema ni hekima zaidi kuangalia au kusaidia wanafunzi wa ndani wasiokuwa nacho kuliko wanaopata ufadhili wa nje ya nchi.

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WADANGANYIFU FOMU ZA MIKOPO YA ELIMU YA JUU

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Naibu katibu mkuu wizara ya elimu sayansi na teknolojia, Profesa Simon Msanjila, amesema serikali imebaini kuwa idadi kubwa ya wanafunzi walioomba mikopo kupitia bodi ya mikopo ya elimu ya juu nchini, wameandika na kujaza taarifa za udanganyifu katika fomu zao za maombi.

Profesa Msanjila ameyasema hayo alipokuwa mgeni rasmi katika mahafali ya nne ya chuo kikuu cha Sayansi na teknolojia mkoani Mbeya (MUST), ambapo wanafunzi zaidi ya 800 walihitimu kozi mbalimbali ikiwemo usanifu wa majengo na uhandisi. Alisema serikali imeanza uhakiki wa kupitia fomu zote zilizowasilishwa katika bodi hiyo na kueleza kuwa atakayebainika kujaza nafasi zisizokuwa sahihi lazima afikishwe katika vyombo vya sheria.
“Siku hizi kuna changamoto kwamba kila mwanafunzi akipata udahili ni definition kwamba ametoka familia maskini sasa sijui kama hilo ni kweli. Lakini tuelewe kwamba kuna vigezo ambavyo vimewekwa na ambavyo tunapima ni nani apate mikopo hiyo na vigezo vimewekwa na serikali. Changamoto nyingine ni kwamba waombaji wengine sio wote baadhi wanatoa taarifa zisizo sahihi wanawasilisha document za kuombea mikopo na kufoji na vinginevyo,” alisema Msanjila.
“Serikali imeanza kufanya uhakiki wa fomu zote zilizotumika kwenye maombi na wale watakaogundulika kutumia taarifa za uongo sheria itachukua mkondo wake,” aliongeza.

BODI YA MIKOPO(HESLB) YATANGAZA MAJINA YA WADAIWA SUGU KUANZIA MWAKA 1994 HADI 2014, YATAZAME HAPA

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inatangaza orodha ya majina ya Wadaiwa Sugu ambao wamehitimu katika Vyuo mbalimbali vya Elimu ya Juu kuanzia mwaka wa masomo 1994/1995. 

Wasugu hao wanapewa siku 30 kulipa madeni yao ndani ya muda huo kabla hatua za kisheria hazijachukuliwa na wahusika kulazimika kulipia gharama za kuwasaka na kuendesha kesi.

Kwa mawasiliano zaidi piga 0763 459 165 au 0767 513 208 au tembelea ofisi zetu za Makao Makuu, Dar es salaam au ofisi zetu za kanda zilizopo Dodoma, Zanzibar, Mwanza na Arusha.

Kuona orodha hiyo bofya viunganishi vifuatavyo:










WADAIWA SUGU BODI YA MIKOPO WAPEWA SIKU 30

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa bodi hiyo Abdul-Razaq Badru amesema kuwa hadi sasa kuna jumla ya wadaiwa sugu 142,470 wenye mikopo ya shilingi 239,353,750,170.27 iliyokwishaiva hawajajitokeza wala kuanza kulipa mikopo yao.

Akitolea ufafanuzi wa maana ya neo "Wadaiwa Sugu", Badru amesema kuwa ni wanufaika waliokopeshwa, muda wa matarajio ukapita bila kuwasilisha taarifa zao na kulipa madeni ya mikopo waliyokopeshwa tangu mwaka wa masomo 1994/1995.

Kuhusu hatua zinazochukuliwa na bodi hiyo, Badru amesema mbali na kutoa siku 30, bodi hiyo inakamilisha taratibu za kuwafikisha mahakamani kwa kuvunja sheria ya bodi ya mikopo kifungu cha 19A(1).

Hatua nyingine ni pamoja na kuyawasilisha majina hayo katika taasisi za mikopo, kuwasiliana na wadhamini wao pamoja na kuyatangaza hadharani majina ya wadaiwa sugu wote ili waajiri, wadhamini na wadau wengine wayajue na kutoa taarifa katika bodi hiyo.

Kuhusu takwimu za mikopo iliyotolewa, amesema tangu 1994/95 hadi 2015/16 jumla ya shilingi 2,595,932,575.56 zimekopeshwa kwa jumla ya wanufaika 379,179.

Amesema kati ya mikopo yote iliyokopeshwa, mikopo iliyoiva ni shilingi 1,425,708,285,046.48 kwa wanufaika 238,430 ambao tayari wamemaliza kipindi chao cha matazamio.

Badru amesema kuwa jumla ya wanufaika wa mikopo 93,500 wamebainika na kupelekewa ankara za madeni yao, ambapo kati yao wanufaika 81,055 wanaendelea kulipa.