HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

SUMU YA PENZI SEHEMU YA THEMANINI NA NANE(88)

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


“unataka kufanya nini mke wangu.. hapana tafadhali usifanye hivyo..” alianza kulia mume wangu akitamani kuja kunitoa, lakini Yule kaka alikuwa makini kushikilia bastola yake akimuoneshea mume wangu akAtulia kimya kama ananyolewa.
“Yule mchumba wa jamaa alionekana kulia na kutotaka hata kuangalia nilichokua nikikifanya.
“Basi nikaanza kumchezea aliposimama vizuri nikamuinamia na kuushukilia msumeno wake kwa nyuma na kuuchomeka ili aanze kuranda mbao.
“Sikujali nikamtazama mume wangu akionekana kuumia kiasi cha mwisho, nikawa najiuliza kama yeye alichepuka na kunisaliti mimi, sasa nini kilichomuuma?
Potelea mbali acha nimuadhibu akasimulie kwa mama yake, shangazi yake, hadi kwa babu yake. Lakini kwa muda huo nilitaka kumuonesha kuwa hata mimi siyo mjinga, naweza pia kufanya anachokifanya.
Basi Yule kaka alipomaliza kukojoa, nikajichomoa na kupandisha chupi yangu. Kisha nikabeba vyangu na kuaga.

UKITAKA KUSOMA STORY YA LEO AU ZILIZOPITA ZILIZOKAMILIKA NITAFUTE WHATSAPP KWA NAMBA HII 0713363965 NA KAMA HUNA WHATSAPP PIGA SIMU UPEWE MAELEKEZO YA   KUTUMIWA

MWISHO

SUMU YA PENZI SEHEMU YA THEMANINI NA SABA (87)

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Kiukweli, nilikuwa nimestaajabu mno, na sasa ndiyo nikagundua kwanini nilikuwa na wasiwasi na mume wa Gululi kurudiana na Gululi harakaharaka vile. 
Ilivyoonesha kuwa alitaka kuwachanganya Gululi na kile kibinti cha chuo, sasa amefumaniwa. Na kwa kuwa nilikuwa mbali sikuweza kwenda cha zaidi nilimshauri tu Gululi cha kufanya.
“Gululi huyo mwanaume amekuelekeza kuwa amemfumania mumeo gesti gani?” nilihoji.
“ndiyo ni palepale kazini kwa mume wangu..” alisema Gululi.
“Gululi naomba ujikaze uende, ukajionee isije kuwa anataka kukufitinisha..” nilisema Gululi akaitikia kuwa anaenda muda huohuo. Akakata simu.
Muda wote nikawa nampigia hakuwa akipokea, nikazidi kuwa na wasiwasi. Baadaye usiku akanipigia simu mwenyewe sasa akionekana amepoa mno kuliko mwanzoni.
“Gululi nini kinachoendelea.!” Nilihoji.
“Mary nimefanya kitu ambacho, sitakijutia maisha yangu yote, najua umefanya kila uwezalo kunisaidia, lakini mwisho wa siku uvumilivu umenishinda nimeamua kutokuwa mjinga tena kwenye mapenzi,” alisema Gululi.
“Gululi niambie umefanya nini?”
Basi akanisimulia mambo ambayo nilipoyasikia tu hata mimi mwenyewe nikabaki mdomo 



UKITAKA KUSOMA STORY YA LEO AU ZILIZOPITA ZILIZOKAMILIKA NITAFUTE WHATSAPP KWA NAMBA HII 0713363965 NA KAMA HUNA WHATSAPP PIGA SIMU UPEWE MAELEKEZO YA   KUTUMIWA

ITAENDELEA ALHAMISI 

VALENTINES'S DAY: ASILI NA HISTORIA YAKE HADI KUSISIMUA ULIMWENGU

Siku ya wapendanao au Valentine's day ina historia ndefu sana. 
Asili ya siku ya wapendanao "Valentine's Day" ni St Valentine, mhubiri wa kikristo aliyekuwa akiishi karibu na mji wa Roma katika karne ya tatu wakati wa utawala wa Claudis II.

Claudis alitaka awe na jeshi kubwa akategemea vijana wangejitolea na kujiunga na jeshi lake. Lakini vijana wengi hawakupenda vita kwakuwa hawakutaka kuziacha familia zao na watoto wao.

Claudis akafikiria akaona hawa vijana kuwakomesha waingie jeshini ni kupiga marufuku watu kuoana.Kuanzia hapo akapiga marufuku watu kuoana akitegemea vijana hawatajali sasa kujiunga na jeshi kwasababu ya familia zao.

Askofu Valentine naye kwa siri akawa anawafungisha ndoa vijana hao kwa siri. Claudius aliposikia habari hizo aliamuru Valentine akamatwe na akahukumiwa adhabu ya kifo cha kunyongwa.

Wakati akiwa jela akisubiri siku yake ya kunyongwa Valentine alikuwa akitembelewa na vijana waliokuwa wakimpelekea maua kuonyesha wako pamoja nae.

Mmoja wa vijana waliokuwa wakienda kumtembelea ni mtoto wa mkuu wa gereza ambaye aliruhusiwa kuingia mpaka kwenye selo la Valentine "kupiga naye stori".

Inasemekana kwamba Valentine aliangukia katika mapenzi na binti huyo wa mkuu wa gereza wakati anasubiria kunyongwa.

Inasemekana kwamba muda mchache kabla hajanyongwa Valentine aliomba kalamu na karatasi na kuandika meseji yake ya kuaga akiweka sahihi "From Your Valentine" ( kutoka kwa Valentine wako )

Valentine akanyongwa tarehe 14 februari mwaka 269 AD. Baada ya kunyongwa kwa Valentine, vijana wa Roma walianza kumuiga Valentine na kuwaandikia na kuwatumia wanawake waliowapenda salamu za mapenzi.

Tangia siku hiyo tarehe hiyo ikaanza kuhusishwa urafiki, upendo na mahaba duniani huku ikihusishwa zaidi na mambo ya mapenzi.

Siku hiyo imezidi kuwa maarufu kila miaka inavyoenda huku huku makampuni yakiigeuza siku hiyo kuwa ya biashara zaidi kwa kufanya kila kitu maalumu kwa siku ya wapendanao kionekane kuwa inabidi kiwe chekundu kuanzia kadi za salamu, maua, mpaka nguo wavaazo wapendanao inabidi ziwe nyekundu.

Kuna watu wengi pia ambao hawasherehekei siku hii kwa kuhoji umuhimu wa kuonyesha kumjali umpendaye katika siku moja tu ya mwaka badala ya siku zote 365.

SUMU YA PENZI SEHEMU YA THEMANINI NA SITA(86)

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Basi ikawa kama vile Gululi amenitia moyo, japo kuwa mbinu zangu sio za kihivyo lakini zilikuwa zikienda vizuri. Siku hiyo nikamwambia juu avae kitop chini akavaa khanga, ikabidi nimfunge mimi mwenyewe maana yeye alikuwa akizoea kujifunga tumboni kama mtu mzima, wakati wasichana wakisasa wote wanafunga mlegezo. 
Tukaenda na vikapu vyetu kununua mahitaji ya kupika mchana kwa makusudi japokuwa nilijua hatuwezi kukutana na mumewe Gululi lakini nilitaka mtaa mzima ukimuona Gululi ukampe taarifa mumewe kuwa mkewe kawa mcharo.
Basi taratibu tukatembea na kununua vyetu, tukawa tunarudi, kama kawaida vijiwe vya madereva bajaji  wakawa wanazidi kumsumbua Gululi, wengine wakimsifia tu hadharani kuwa amependeza, wengine ni wanawake wa hapo mtaani wakimtazama kwa husuda, tena nikamtaka tujipitishe kwenye vijiwe vya marafiki wa mumewe ili mradi tu maneno yakamfikie mlengwa.


UKITAKA KUSOMA STORY YA LEO AU ZILIZOPITA ZILIZOKAMILIKA NITAFUTE WHATSAPP KWA NAMBA HII 0713363965 NA KAMA HUNA WHATSAPP PIGA SIMU UPEWE MAELEKEZO YA   KUTUMIWA

ITAENDELEA JUMATANO

SUMU YA PENZI SEHEMU YA THEMANINI NA TANO (85)

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


“hii baa ina matatizo gani? Tumekuja hapa dakika nzima hakuna wahudumu wala nini au tuondoke!” nilimfokea huyo mwanaume bila kujali mguu wa Gululi aliyekuwa akinigonga kwa chini.
“hapana dada msiondoke popote niombe radhi,” alisema na kuita mhudumu mmoja kwa amri. Akaanza kuwakoromea wale wahudumu e na kuwataka watusikilize haraka sana.
Basi mhudumu mmoja akaja na alipochukua oda na kuondoka, nikamuuliza sasa vizuri Gululi.
“ndiyo huyu!”
“ndiyo yeye.”
“anafanya nini mbona amekuja kibosibosi?”
“mh nilisikiaga ni meneja wa baa, inawezekana!” Alisema Gululi.
“sikia nimeona anavyokutolea macho, sasa hiyo ni hatua nzuri lakini usije ukajilegeza kwa chochote.. la sivyo atakutumia na kukuacha tena..” nilimuonya Gululi tena nikimtaka hata asimuangalie.
Nilipochunguza vizuri nikagundua  kumbe ile baa ina upande wa lodge hapohapo. 
Tena nikamuangalia mume wa Gululi nikagundua ni wakujakuja  yaani alionekana amechelewa kujanjaruka kwa hiyo hakuwa na tatizo la kurudishwa kwenye mstari.
Yaani anaweza kuwa amechepuka na kumuacha mkewe kwa ajili tu ya fasheni au kufuata mkumbo wa marafiki, wanaume kama hao wapo, unakuta kisa marafiki zake wana wasichana wa aina fulani na yeye unakuta anamdharau mkewe au mpenzi wake wa muda mrefu ili kuwa na msichana wa aina hiyo ili mradi tu apate sifa kwa hao marafiki zake.


UKITAKA KUSOMA STORY YA LEO AU ZILIZOPITA ZILIZOKAMILIKA NITAFUTE WHATSAPP KWA NAMBA HII 0713363965 NA KAMA HUNA WHATSAPP PIGA SIMU UPEWE MAELEKEZO YA   KUTUMIWA

ITAENDELEA JUMANNE

SUMU YA PENZI SEHEMU YA THEMANINI NA NNE (84)

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Basi nilirudi nyumbani na mambo mengine yakaendelea vizuri, tena mume wangu ndiye akanikumbusha kuhusu mafunzo yangu ya kungwi akaniulizia naendeleaje.
Mh kiukweli nilikuwa hadi nimesahau kama nilikuwa na mazoezi ya kukaza misuli ya kipapatio. Nikakumbuka sasa nikaona ngoja humohumo nimchomekee kuhusu kuniruhusu kuwa naenda kwa kungwi kuanzia kesho. Akaniruhusu bila hiyana. 
Basi nilichofanya kwanza ni kuingia chumbani na kuanza kutafuta vinguo vyangu vyote vikali vya zamani, nikavijaza kwenye kibegi full. mapema kesho yake nikachomoka hadi kwa akina Gululi.
Tena alionekana ana hamu kweli ya kujua nilikuwa na mipango gani ya kumrudisha mumewe, tena Bibi Gululi naye hakuwa mbali alikuwa akinyapianyapia ili kuona ninafanyajefanyaje, ukweli ni kwamba hata sikuwa na mpango wowote wa maana.
Kabla ya kufungua begi nikaanza kumuuliza Gululi; maswali yangu mawili  matatu.
“hivi, Gululi huyo msichana anayetembea na mumeo yupojeyupoje! Usidanganye kuwa tu mkweli!”niliuliza.
“ni kisichana cheupe hivi, kinavaavaa uchiuchi, kina mashauziii!” alianza kuelezea.
“najua unaongea kwa kukisimanga, lakini kwa maneno yako inaonekana kwanza ni kizuri, kinajua kuvaa na kina swaga,” nilimchana ukweli Gululi.
“kwa hiyo unanisimanga?” alipaniki Gululi.


UKITAKA KUSOMA STORY YA LEO AU ZILIZOPITA ZILIZOKAMILIKA NITAFUTE WHATSAPP KWA NAMBA HII 0713363965 NA KAMA HUNA WHATSAPP PIGA SIMU UPEWE MAELEKEZO YA   KUTUMIWA

ITAENDELEA JUMATATU 

SUMU YA PENZI SEHEMU YA THEMANINI NA TATU (83)

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Huwezi amini sasa nyumba ilitulia, ikabidi ratiba yetu ya sherehe ya utambulisho ihuishwe kama kawaida, tukawa tunasubiriwa sisi tu tupone kwanza vile vijeraha vyetu ili tusije tukachekesha kwenye harusi.
Basi wiki moja kila kitu kilikuwa tayari, huwezi amini kile kijeraha pembeni ya jicho hakikuniharibu hata kidogo, sanasana kikaniongezea urembo wangu na hata Mr X wangu naye alikuwa hivyohivyo.
“baba we are ready! (tupo tayari),” nilimwambia baba nikiashiria kwamba hata kesho au kesho kutwa tufanye sherehe yetu ya utambulisho maana niliisubiria kwa hamu sana. “hivi nyinyi hayo makovu mliambiazana muumie pamoja au?” aliuliza baba kiutani na kucheka.
Haikupita siku nyingi sana, ndugu marafiki, watu wa karibu wote walitaarifiwa na sherehe ya utambulisho tulipanga ifanyike Mlimani City, na mimi nikahakikisha nawatumia kadi ya Mwaliko Kungwi wangu Bibi Gululi na mwanaye Gululi, pia nikawatumia kadi rafiki zangu Getrude na Catherine.
Hayawihayawi sasa yamekuwa; siku ikafikia, ndugu zangu kibao kutoka mikoani na hapa mjini wakajaa na kujazana, na wengine hata ambao sikuwa nikiwafahamu, wengi wakawa wanakuja na kunipongeza kwa kuolewa na mtu wa mamtoni.

UKITAKA KUSOMA STORY YA LEO AU ZILIZOPITA ZILIZOKAMILIKA NITAFUTE WHATSAPP KWA NAMBA HII 0713363965 NA KAMA HUNA WHATSAPP PIGA SIMU UPEWE MAELEKEZO YA   KUTUMIWA

ITAENDELEA JUMAPILI

SUMU YA PENZI SEHEMU YA THEMANINI NA MBILI (82)

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Nilikuja kushtukia nipo hospitali na nilishonwa nyuzi tano. Daktari aliniambia nilikuwa na bahati jeraha lilikuwa juu ya jicho na laiti kama Hadija angenilenga jichoni basi ningekuwa chongo.
Mh! japo nilikuwa kiburi kwenye suala la kumuomba Mungu, aisee siku hiyo nilijikuta nikimshukuru Mungu mno maana Hadija alionekana wazi kabisa kukusudia kuharibu uso wangu. Nadhani alifahamu fika kuwa pengine sura yangu ikiwa na hitilafu ndiyo mapenzi ya mume wangu yatapungua.
Nikakumbuka habari ambazo mara kwa mara huwa nazisikia kuwa mwanamke kachanwa usoni na viwembe au kamwagiwa maji ya moto; yote hayo yanatokana na kuwa wanaringia uzuri wao kwenye mapenzi, kwa hiyo wengine wanadhani hiyo ndiyo dawa ya kuwakomesha.
Na ni kweli kabisa, sasa fikiria kama mpenzi wako anakupenda kwa jinsi ulivyo na sura ya kuvutia, siku ukiungua, au umekuwa chongo kama nilivyonusurika mimi, unafikiri kutakuwa na mapenzi tena hapo!
Kuna mchekeshaji mmoja maarufu wa Uingereza karne ya 20, alikuwa akiitwa Charlie Chaplin huyu jamaa alishawahi kuandika kuwa ‘Your Naked Body Should Belong to someone who is in love with your Naked Soul.” Akiwa na maana; “utupu wa mwili wako apewe mtu ambaye ana mapenzi ya dhati na utupu wa roho yako.”


UKITAKA KUSOMA STORY YA LEO AU ZILIZOPITA ZILIZOKAMILIKA NITAFUTE WHATSAPP KWA NAMBA HII 0713363965 NA KAMA HUNA WHATSAPP PIGA SIMU UPEWE MAELEKEZO YA   KUTUMIWA

ITAENDELEA JUMAMOSI