HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

WAZIRI WA KILIMO ATEMBELEA SKIMU YA UMWAGILIAJI YA USENSE KATAVI













Mhe. Hussein Bashe (Mb), Waziri wa Kilimo ameendelea na ziara yake ya kikazi na kukagua mradi wa ukarabati wa skimu ya umwagiliaji ya Usense, mkoani Katavi tarehe 20 Julai 2024 na kuongea na wanakijiji wanufaika wa mradi huo.

Mradi wa Usense upo katika eneo la ukubwa wa hekta 106 ambapo Waziri Bashe amewaambia wanakijiji malengo ya Serikali ni kuboresha na kuongeza huduma mbalimbali kwa ustawi wa jamii zao.

Amewaeleza malengo hayo ni kuanza ujenzi wa awamu mbili wa kuvuta mkondo wa maji kupitia ujenzi wa mfereji wa maji; na baadae bwawa la maji ili kurahisisha shughuli za umwagiliaji wa kilimo.

Katika kufanikisha awamu hizo mbili, Waziri Bashe amemwelekeza Bw. Raymond Mndolwa, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC) kutengeneza daraja la kivuko ambalo litawezesha wakulima kuwa na umbali wa kilomita 1.8 kufanya shughuli za kilimo cha umwagiliaji badala ya kutembea umbali wa kilomita 7 ambazo wamekuwa wakitembea hadi sasa.

Waziri Bashe ameomba wanakijiji hao wasiuze ardhi ili miradi hiyo iwe na manufaa makubwa kwa familia zao na vizazi vijavyo. Aidha, Waziri Bashe anaendelea na ziara yake mkoani Kigoma tarehe 21 Julai 2024 ambapo atakagua mradi wa umwagiliaji wa Lueche mkoani humo.

MISS UBUNGO MWAKA 2014 DIANA KATO ASHIRIKI SIKU YA MAZINGIRA KWA KUFANYA USAFI HOSPITALI YA AMANA

Aliyekuwa Miss Ubungo 2014/16,  Diana Joachim Kato akipanda mti katika  Hospitali ya Rufaa ya Amana wakati wa  maadimisho ya siku ya Mazingira Duniani
Diwani wa Kata ya Ilala, Saady Khimji  akipanda mti katika  Hospitali ya Rufaa ya Amana wakati wa  maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani
Baadhi ya vijana wakifanya usafi wamazingira yanayoizunguka Hospitali ya Rufaa ya Amana wakati wa  maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani
Diwani wa Kata ya Ilala, Saady Khimji(wa pili kushoto) na Aliyekuwa Miss Ubungo 2014/16,  Diana Joachim Kato(kushoto) wakiwa kwenye picha ya pamoja walipofika katika Hospitali ya Rufaa ya Amana  kwa ajili ya kupanda miti pamoja na kufanya usafi wa mazingira yanaoizunguka hospitaii hiyo leo.

Na Ripota Wetu, Globu ya jamii
ALIYEKUWA Miss Ubungo jijini Dar es Salaam mwaka 2014-2016 Diana Joachim Kato ameshiriki kuadhimisha wiki ya mazingira kwa kufanya usafi katika Hospitali ya Rufaa ya Amana jijini.

Miss huyo ambaye ana mradi wake wa maji safi na salama amefanya usafi huo kwa kushirikiana na Diwani wa Kata ya Ilala jijini Saady Khimji.Hivyo ameamua kushiriki siku ya mazingira duniani kwa kuamua kuitumia siku ya leo kufanya usafi hospitalini hapo ikiwa pamoja na kupanda miti.

Akizungumza baada ya kufanya usafi huo Diana Kato amesema ameamua kushiriki siku ya mazingira duniani kwa kufanya usafi katika hospitali hiyo pamoja na kupanda miti huku akiweke akitoa mwito kwa Watanzania kuendelea kutunza mazingira.

"Nimeona ni vema leo nikawa katika hospitali ya Rufaa ya Amana kwa ajili ya kufanya usafiti na baada ya hapo nikashiriki kupanda miti .Hii yote ni katika kuadhimisha siku ya mazingira duniani .Kubwa zaidi nitoe rai kwa Watanzania tuwe sehemu ya kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuhakikisha tunatunza mazingira yetu ili nayo yatutunze

Taasisi ya Mo Dewji yatoa msaada kwa watoto wenye saratani

Taasisi ya Mo Dewji imetoa msaada kwa watoto wanaopatiwa matibabu ya magonjwa ya saratani katika kituo cha Tumaini la Maisha katika hospitali ya Taifa Muhimbili, Jijini Dar es Salaam.

Msaada ambao umetolewa ni unga wa ngano, khanga na sabuni za kuogea, kufua na kunawia mikono.

Akikabidhi msaada huo, Kaimu Meneja Miradi wa Taasisi ya Mo Dewji, Belinda Paul alisema taasisi yao itaendelea kuwa na utaratibu wa kutoa msaada katika kituo hicho ili kuwafariji watoto ambao wanapatiwa matibabu.

Alisema hiyo sehemu ya kwanza kutoa msaada kwani wamekuwa na utaratibu wa kusaidia jamii kutokana na uhitaji uliopo hivyo kwa kufanya hivyo wanaamini watakuwa wamegusa maisha ya Watanzania wengi.

Aidha, Paul amewataka watu wengine wenye uwezo kuweka utaratibu wa kusaidia watu wengine wenye uhitaji kama watoto waliopo katika kituo cha Tumaini la Maisha.

Kaimu Meneja Miradi wa Taasisi ya Mo Dewji, Belinda Paul akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watoto ambao wanapatiwa matibabu katika kituo cha Tumaini la Maisha.

Kaimu Meneja Miradi wa Taasisi ya Mo Dewji, Belinda Paul akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wasimamizi wa kituo cha Tumaini la Maisha wakati walipokuwa wakikabidhi msaada katika kituo hicho.

Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (USDM) ambao wanalipiwa gharama za masomo na Taasisi ya Mo Dewji wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watoto wanaopatiwa matibabu katika kituo cha Tumaini la Maisha.

WANAFUNZI LUGALO WALIA NA MIUNDOMBINU KWA WALEMAVU


Na Mwandishi Wetu, IRINGA
WAHITIMU wa kidato cha sita wa Sekondari ya Lugalo mkoani hapa wameiomba Serikali kuisadia kuboresha miundombinu kwa ajili ya wanafunzi walemavu.
Katika Risala yao kwa mgeni Rasmi wamesema pamoja na mafanikio mengi waliyoyapata kupitia shule hiyo bado wanakabiliwa na changamoto kubwa ya kukosekana kwa uzio, mfumo mbovu wa maji taka kukosekana kwa karatasi maalum za walemavu wasioona pamoja na kutokuwa na miundombinu rafiki kuwezesha kuwa salama katika mazingira ya shule kwa wanafunzi wenye uhitaji maalum pamoja na uhaba wa waalimu wa Sayansi.
Akijibu Risala ya wanafunzi hao, Mwenyekiti wa Umoja wa Wanafunzi waliosoma shuleni hapo, Nayman Chavalla, kupitia kampuni inayoitwa Lugalo Associate Company Limited wameanza kukarabati nyumba ya Mkuu wa shule pamoja na ya Makamu wa shule na kuahidi kuwa umoja huo utaendelea kusaidia shule hiyo endapo matokeo ya taaluma yataboreshwa.
Chavalla ameongeza kuwa Umoja huo unayo nia ya dhati katika kusaidia kutatua changamoto za elimu shuleni hapo na kuwataka walimu kufuta daraja sifuri na daraja la nne katika matokeo ya kitaifa ili kuleta motisha kwa wadau wanaochangia maendeleo ya shule.
Pia amesema pamoja na kuwa Serikali inahamasisha Elimu Bure lakini bado jukumu la kujibidiisha katika masomo na kuinua viwango vya ufaulu ni la Mwanafunzi na waalimu wenyewe katika kukuza taaluma yenye viwango.
Mmoja wa wahitimu mwenye ulemavu wa macho, Elizabeth Mwaisoba mwenye umri wa miaka 18 amesema kuna haja kwa Serikali kuendelea kusaidia wazazi wenye watoto wenye uhitaji maalum katika kupata elimu kwani inahitaji kipato kikubwa katika kuwahudia wanafunzi wenye uhitaji wa ziada na kuiomba Wizara husika kutillia mkazo suala la komputa zenye sauti ili nao waweze kwenda sambamba na teknolojia ya sasa.
Felista Mkesela, mwenye ualbino, amesema ipo haja ya waalimu kuona umuhimu wa kuweka vifaa vya kukuza maandishi ya ubaoni na kuongeza muda wa ziada kwa wanafunzi walio na ulemavu wawapo darasani, kwani kuwapa muda sawa na wanafunzi wa kawaida kunaathiri kufanya vizuri katika masomo yao.
Mkuu wa Shule hiyo,  Benjamin Kabungo, amesema kwa sasa shule hiyo ina wanafunzi 63 wenye ulemavu wakiwemo wasioona, albino, wenye uoni hafifu, na walemavu wa viungo na kwamba walimu 4 wa Elimu Dumishi, awali Shule hiyo ambayo ilianzishwa mwaka 1945 na kujulikana kama The H.H Aga Khani, pia imeanzisha ufugaji wa viumbe wakiwemo panya weupe kwa ajili ya kufanya utafiti wa Kisayansi.

WAKAZI WA ARUSHA KAMA UNA KIPAJI HII INAKUHUSU


HERI YA KUMBUKUMBU YA KUZALIWA BLOGGER CATHBERT KAJUNA

Leo Aprili 10 ni siku ya kuzaliwa kwa Journalist/Photojournalist na Blogger Cathbert Angelo Kajuna mmiliki wa Kajunason Blog (www.kajunason.com) na Mwandishi/Mpigapicha wa MMG.

"Napenda kuchukua fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuweza kunifikisha siku ya leo ya kuzaliwa kwangu, hakika yeye ni mwema maana amenivusha katika milima na mabonde na amekuwa akinifanyia mambo makubwa katika maisha yangu.

Pili nipende kutoa shukrani kwa familia yangu, ndugu jamaa na marafiki wote ambao mmekuwa bega kwa bega pale ambapo nimekuwa nikikwama mmekuwa mkinishika mkono na kunivusha hakika sina cha kuwalipa bali mwenyezi Mungu awaongezee busara, upendo na amani.

Tatu, kabisa nipende kutoa shukrani za pekee kwa Mke wangu, Mama yangu Mzazi, baadhi ya ndugu na marafiki ambao bila wao labda nisigekuwa hapa leo, nianze na Familia ya Kajuna Jr (Kennedy), Familia ya Michuzi Media Group ikiongozwa na Ankali Michuzi, Michuzi Jr na Othman hakika najivunia ukarimu na upendo wetu kwangu najivunia kuwa mmoja ya mwanafamilia, Familia ya Jackson Mmbando, rafiki zangu Seki David, Edwin David, Portnes, Mwesiga Kyaruzi, Shebby Mpondela, Franklin Alexander, Ally Jamal, Imani Ntila, James Jonathan na Dr. Heri Tungaraza. Wengine ni Raymond Maganga, Myoma Kapya - Chilala, Mike Mukunza, Muhidin Sufian, Bakari Kimwanga, John Bukuku, Abraham Mossi, Sylvia Mwehozi, Leah Mushi, Mary Masinda, Tiba  Josephat Lukaza, Ruben (Baba Countinho) na wale wote ambao nimekuwa nikishirikiana nao kwa namna moja au nyingine katika kusaka ugali wetu wa kila siku.

Mwisho, Shukrani za pekee ziwaendee wanachana wote Tanzania Bloggers Network (TBN) popote mlipo nawaomba tuendelee kushirikiana kwa pamoja, Umoja ni Nguvu.
Ni mimi Cathbert A. Kajuna.
10.04.2018


UBALOZI WA KUWAIT NA TAASISI YA DORIS MOLLEL WATOA MSAADA WA VIFAA TIBA KWA WATOTO NJITI, HOSPITALI YA BENJAMINI MKAPA, DODOMA

Balozi wa Kuwait nchini Tanzania, Jaseem Al Najem (kushoto) akimkabidhi Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Benjamini Mkapa, Dkt. Alphonce Chandika, sehemu ya vifaa tiba kwa ajili ya Watoto Njiti, vilivyotolewa na Ubalozi wa Kuwait kwa kushirikiana na Taasisi ya Doris Mollel, katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika mwishoni mwa wiki, mjini Dodoma. Wengine pichani ni Muanzilishi wa Taasisi ya Doris Mollel na Balozi wa Watoto Njiti nchini, Doris Mollel (wa pili kushoto), Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa Hospitali hiyo, Neema Tawale (wa pili kulia) pamoja na Kaimu Mkuu wa Huduma za Uuguzi, Salome Kasanga.

The Ambassador of Kuwait in Tanzania His Excellency Hon. Jaseem Al Najem (L) Handing Over Equipments to support Premature babies at Benjamin Mkapa Hospital to the Executive Director of the Hospital, Dr. Alphonce Chandika, A support from the Embassy of Kuwait in Collaboration with Doris Mollel Foundation end of this week in Dodoma. second from left is Ms. Doris Mollel Founder of Doris Mollel Foundation and Ambassador to Preterm babies in Tanzania , Neema Tawale(second from right) together with Acting Director of Nursing at Benjamin Mkapa Hospital Sr Salome Kasanga.
 Muanzilishi wa Taasisi ya Doris Mollel na Balozi wa Watoto Njiti nchini, Doris Mollel akieleza jambo kwa waandishi wa habari juu ya vifaa hivyo vilivyogharimu dola za Marekani elfu ishirini (20,000 USD) huku Balozi wa Kuwait nchini Tanzania, Jaseem Al Najem (kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Benjamini Mkapa, Dkt. Alphonce Chandika (kulia) wakimsikiliza, katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika mwishoni mwa wiki, mjini Dodoma.
Balozi wa Kuwait nchini Tanzania, Jaseem Al Najem,  Muanzilishi wa Taasisi ya Doris Mollel na Balozi wa Watoto Njiti nchini, Doris Mollel, Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Benjamini Mkapa, Dkt. Alphonce Chandika wakimsikiliza Kaimu Mkurugenzi Huduma za Upasuaji wa Hospitali ya Benjamini Mkapa, Dkt. Januarius Hingi wakati akitoa maelezo ya namna vifaa hivyo vitakavyosaidia wakina mama wanaojifungua watoto wanaozaliwa kawaida na wale wanaozaliwa kabla ya wakati. 
Sehemu ya vifaa hivyo.

Cancer Case in Tanzania: Room for Development

  Today Tanzania is facing a cancer crisis with as many as 35,000 new cases expected to be diagnosed a year. 
  In spite of the emergence of cancer as a serious national problem, there are only two cancer hospitals in the country. 
  The largest cancer disease hospital is the Ocean Road Cancer Institute (ORCI), located in Dar-es-salam. The Institute handles nearly 3,000 new cancer patients and up to 10,000 follow-up cases annually. Up to 20% of ORCI's patients are children, who are usually treated with both chemotherapy and radiotherapy. The ORCI is equipped with diagnostic imaging services and cancer screening. 
  However, regular screening and early diagnosis is not a common event in Tanzania. Only a small number of patients from all over the country can afford to travel to Dar-es-salaam for cancer check-up. 

The United Republic of Tanzania National Health Policy advocates the right for cancer patients to be treated free of charge. Prior to diagnosis, patients are required to cover for themselves the expenses related to screening of cancer and any other necessary medications which are not covered by the government.
  In general, this challenging situation with cancer patients can be alleviated by opening of new screening centers and nuclear medicine facilities which are indispensable for cancer diagnostics and treatment.  

  With advanced nuclear technologies, Tanzanian doctors will be able to deliver more precise diagnosis, treatment and be able to evaluate treatment given to cancer patients. Specialists at ORCI are now able to employ more innovative 3D scanning of tumors, that detects the abnormal cells at early stages with more accuracy than the scanners of previous generation.  
  Once the tumor is identified, medical specialists are able to use modern technology such as contouring computer software to define and separate the healthy tissue from affected one in order to apply radiation and medical isotopes in a more accurate way to minimize exposure to healthy tissues and organs. .

  Tanzanian government is exerting considerable efforts to tackle health issues with new strategies and programs at all levels, starting from preparation of specialists capable to deliver professional service. Compared to other East African countries, Tanzania is the only country with the highest number of nuclear medicine specialists even though their number is still very low.
  Nuclear medicine specialty involves the use of facilities such as PET/CT (Positron Emission Tomography/Computer Tomography) and currently PET/MRI(Positron Emission Tomography/Magnetic Resonance Imaging), Hybrid SPECT/CT (Single Photon  Emission Computed Tomography),Thyroid Uptake System and so on.

  PET/CT, PET/MRI and SPECT/CT require radiopharmaceuticals and radioisotopes in diagnosis of patient’s disease or in evaluation of treatment given to cancer patients.
  Commonly used radiopharmaceuticals in nuclear medicine department include flourine-18 flouorodeoxyglucose (18F-FDG), Technetium-99m (99mTC), Molybdenium-99, Iodine-123 and Iodine-131 (123I and 131I), Thalium-201 (201TI) and so on.
  Development of nuclear medicine can be boosted by creating of nuclear research center, equipped with nuclear research reactor. 

  For instance, production of medical isotopes to treat cancer and other diseases could not be possible without research reactors development. The case of South Africa shows that research reactors have potential to adjust nuclear technologies for social development. Thus, South Africa's SAFARI-1 research reactor is among the leading producers of medical isotopes in Africa. It is also one of the four largest producers of key isotope Molybdenum-99 which is used in over 70% of nuclear medicine procedures globally. 

  As one of the nuclear medicine specialist in the country, i urge the government to consider setting up a nuclear medicine center which will greatly improve the quality of services provided in the health sector. The center will serve all individuals regardless whether they are suffering from cancer or not. The applications of  nuclear medicine department includes diagnosis of benign and malignant tumor in the body, detection of cancer metastases, evaluation of  bone trauma and  cancer metastases, evaluation of kidney, heart, lung, brain, thyroid diseases and so on. I am aware that the government intends to set-up a nuclear medicine department at Benjamin Mkapa Hospital, Dodoma, Tanzania, since i was actively involved in its planning.

  As the current phase government focuses on industrialization drive, this is an opportunity for her to invest heavily in nuclear medicine department and research centers so as to attract patients from other countries, earning country the much needed foreign currency. The government will save a lot of money which otherwise would have been used to send patients abroad due to lack of nuclear medicine facilities in the country. 

  Other area where the country will also save money is by production of its own radio pharmaceuticals and radioisotopes locally instead of importing them from other countries. Exporting of radio pharmaceuticals and radioisotopes to our neighboring countries will also earn our country foreign currency. The countries with nuclear medicine and research centers in Africa include Egypt and South Africa. This will make Tanzania the leading hub of nuclear medicine technology and researches in the entire east African region. God bless Africa, God bless Tanzania.

  The author is a nuclear medicine physician and lecturer at The University of Dodoma, currently undertaking PhD studies at Tongji Medical College of Huazhong University of Science and Technology, P.R. China.

Dr.Khamis H.Bakari,