HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

SERIKALI KUWALIPA WALIMU MADENI YAO BAADA YAKUJIRIDHISHA NI HALALI

 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akijibu maswali ya wabunge katika kikao cha kumi cha Mkutano wa saba wa Bunge la 11 leo Mjini Dodoma Aprili 20, 2017. 

Serikali imesema itaendelea kulipa madeni ya walimu kadri inavyoyapokea na kujiridhisha kwamba madeni hayo ni halali.
Waziri mkuu Mhe.Khasim Majaliwa amesema hayo bungeni mkoani Dodoma wakati akijibu maswali ya papo  kwa hapo.

Amesema Serikali imeandaa utaratibu mzuri wa kulipa madeni hayo kila yanapohakikiwa na kuwataka walimu kuendelea kufanya kazi zao kwa
bidii.

Awali mbunge wa Kilolo Mhe.Venance Mwamoto alimuuliza Waziri mkuu sababu za baadhi ya madeni ya walimu  kulipwa  kwa kusuasua na Serikali na mengine kutokulipwa.

Serikali yatoa ajira kwa walimu 3,081

Serikali imesema jumla ya walimu 3,081 wakiwemo walimu 7 wa shule ya Sekondari Omumwani Kagera, wameajiriwa, hivyo bado kuna nafasi ya walimu 1.048 kati ya nafasi 4,129 za walimu wa Sayansi na Hisabati zilizotolewa kibali cha ajira.

Taarifa hiyo imetolewa leo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) George Simbachawene alipokuwa  akizungumza na Waandishi  Habari,ofsini kwake ambapo amewataka walimu wote walioajiriwa wanatakiwa kuripoti katika vituo vyao vya kazi kuanzia tarehe 18 hadi 25 mwezi huu.

Amesema walimu walioajiriwa  wamepangwa moja kwa moja na TAMISEMI katika halmashauri zote nchini ambazo zina upugufu wa walimu wa Sayansi na Hisabati.

Simbachawene amesema kati ya walimu hao walioajairiwa walimu 1,537 ni wa Shahada  na walimu 1,544 ni wa Stashahada.

“Sehemu kubwa ya walimu wa Shahada wamepangwa  kwenye shule za kidato cha tano na sita na wachache kwenye shule za kidato cha kwanza hadi cha nne’’ alisema.

Simbachawene amekiri  kuwa kuna upungufu wa walimu 26,026 wa masomo Sayansi na Hisabati katika shule mbalimbali za sekondari nchini.

“Moja ya changamoto kubwa ambazo zinaikabili sekta ndogo ya elimu ya sekondari ni upungufu wa walimu wa Sayansi na Hisabati upungufu uliopo  katika shule 3,602 ni 26,026 sawa na asilimia 60.14 ya walimu 43,248 wanaohitajika” amesema Simbachawene

Amesema walimu wanaohitajika kwa masomo hayo ni walimu 43,248 lakini waliopo kwa sasa ni 17,252 pekee.

Amesema kwa sasa serikali ina shule za sekondari 3,602 na kati ya hizo shule 333 ni za kidato cha tano na sita huku zingine 54 za kidato cha tano zimeanzishwa .

Aidha amesema shule hizo za sekondari kwa upande wa masomo ya Sanaa ina ziada ya walimu 7,463 ambapo waliopo ni walimu 63,240 na wanaohitajika ni walimu 55,777.

“Kutokana na ziada hiyo ya walimu wa Sanaa serikali imeanza kuchukua hatua yawahamisha walimu hao katika shule za msingi ili kuziba upungufu wa walimu katika shule hizo’’ alisema.

WAKUU WA SHULE NA WAKURUGENZI DAR WATAKIWA KUTOA SABABU ZA SHULE ZAO KUFELI

Kufuatia Dar es Salaam kufanya vibaya katika mtihani wa kidato cha nne kwa mwaka 2016 kwa kuingiza shule 6 kati ya kumi zilizofanya vibaya, ofisi ya Elimu Mkoa imewaagiza wakuu wa shule na wakurugenzi kutoa taarifa za kina juu ya sababu zilizopelekea kufanya vibaya.

Akiongea na TBC, kaimu Afisa elimu mkoa, Janeth Nsunza, alisema bado wanaendelea na kikao kujadili tathmini ya matokeo hayo na wamesema watatoa taarifa kamili watakapomaliza majadiliano.
Alisema, “Kati ya shule 10 ambazo hazikufanya vizuri shule hizo ni Kitonga, Nyeburu, Mbopo, Mbondole, Somangila day na Kidete kufuatia shule hizo sita kutofanya vizuri mkoa wa Dar es Salaam, mkoa umepokea taarifa hizo kwa masikitiko makubwa kwani imekuwa ni kinyume cha matarajio yetu na serikali yetu kwa ujumla.”
“Kwakuwa matokeo yametanganzwA, hatua za kufahamu nini hali hiyo imejitokeza zimechukuliwa mara baada ya matokeo hayo kutangazwa ambapo wahusika wanaendelea kutoa maelezo yao, licha kwa kuwepo kwa viashiria katika mtihani wa Mock na wakurugenzi waliwaelekeza wakuu wa shule hizo kuondoa hali hizo mapema,” aliongeza Nsunza.

SERIKALI YAMWAGA AJIRA ZA WALIMU WA SAYANSI NA HISABATI

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.



MWALIMU AFARIKI KATIKA MKUTANO WA CHAMA CHAO CHA CWT JIJINI DAR ES SALAAM

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


 Mwalimu Tuhobwike Mwinuka Mwakatumbula enzi za uhai wake.
 Jeneza lenye mwili wa mwalimu Tuhobwike Mwinuka Mwakatumbula likiwa ndani ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Wazo Hili Dar es Salaam leo asubuhi wakati wa ibada ya kuuaga mwili huo.
Binamu wa marehemu, Nobert Nselu (kulia) akimsaidia rafiki wa karibu wa marehemu mama Malugu wakati mwili wa marehemu ukiwasili nyumbani kwake.
 Rafiki wa marehemu mama Malugu (katikati) akisaidiwa.
 Waombolezaji wakiwa msibani nyumbani kwa marehemu 
Wazo Hill.

 Ni huzuni kubwa 
 Wakina mama wakiwa na maua wakati wakisubiri mwili wa marehemu kuingizwa ndani.
 Geneza lenye mwili wa marehemu likiingizwa nyumbani kwake. 
 Mtoto mkubwa wa marehemu Nico Mwakatumbula (katikati), akisaidiwa baada ya kutoa heshima za mwisho kwa mama yake.
 Waombolezaji wakiingiza jeneza lenye mwili wa marehemu katika Kanisa la KKKT Usharika wa Wazo Hill.
 Mwili ukiwa kanisani.
 Mume wa marehemu akiwa na watoto wake. Kutoka kulia ni Gloria, Kelvin na Nico.
 Wanafamilia wakiwa katika ibada hiyo ya kumuaga mpendwa wao.
 Waumini wa kanisa hilo wakiwa kwenye ibada hiyo.N a Dotto Mwaibale

MWALIMU Tuhobwike Mwinuka Mwakatumbula wa Shule ya Msingi Kumbukumbu katika Manispaa ya Kinondoni amefariki dunia wakati akiwa katika mkutano wa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) na viongozi wa Idara ya Elimu wa manispaa hiyo.

Kifo cha mwalimu huyo kimetokea Desemba 1, 2016 Siku ya Ijumaa majira ya jioni wakati viongozi hao walipokuwa wakimalizia ziara yao ya kutembelea shule mbalimbali katika manispaa hiyo.

Akizungumza na Jambo Leo mume wa marehemu Samuel Mwakatumbula alisema mke wake hakuwa na tatitizo lolote la kiafya na siku ya tukio hilo aliamka salama na kumuaga kuwa anawahi kwenye mkutano huo.

"Siku chache kabla ya kifo chake mke wangu aliniambia alikuwa hajisikii vizuri kwani alikuwa na uchovu wa kawaida" alisema Mwakatumbula.

Mwakatumbula alisema alipigiwa siku na kuambiwa kuwa mke wake alianguka ghafla wakati mkutano ukiendelea na kupoteza fahamu ambapo alikimbizwa Hospitali ya Mount Mkombozi iliyopo maeneo ya Morocco ambapo waliambiwa tayari alikuwa amefariki.

Mwili wa marehemu ulisafirishwa jana kwenda Kiwira wilayani Rungwe mkoani Mbeya kwa maziko yatakayofanyika leo marehemu ameacha mume na watoto watatu, Nico, Kelvin na Gloria.

WALIMU WATATU WATIWA MBARONI KWA KUWAZUIA WANAFUNZI KUFANYA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


POLISI mkoani Dodoma inawashikilia walimu watatu wa shule za sekondari kwa tuhuma ya kuwazuia wanafunzi wa kidato cha nne, kufanya Mtihani wa Taifa.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa alisema kwamba walimu hao wa shule za sekondari za Zoissa na Mnyakongo wilayani Kongwa, walikamatwa Novemba Mosi mwaka huu.

Kamanda Mambosasa alisema kwamba, wakati wa mtihani wa somo la Kiingereza, walimu hao walimzuia mwanafunzi Amina Said wa shule ya sekondari Zoissa kwa madai ya kuwa ni mjamzito na kumpeleka kituo cha afya, kupimwa muda wa mtihani, lakini majibu yalionesha hakuwa na ujauzito.

Aidha, mwanafunzi Bahati Ntigonza wa shule ya sekondari Mnyakongo, alizuiliwa kuingia katika chumba cha mtihani kwa kuwa hakuvaa sare ya viatu, hivyo alirudishwa nyumbani kuvaa viatu huku wenzake wakiendelea na mtihani.

Kamanda Mambosasa aliwataja watuhumiwa waliokamatwa kuwa ni Lukonge Mwezo ambaye ni Mkuu wa Shule ya Sekondari Mnyakongo, Omari Athumani Mkuu wa Shule ya Sekondari Zoissa na Daud Suleimani John aliyekuwa mwalimu wa zamu katika shule ya sekondari Mnyakongo.

SARE ZA CCM ZAMSHUSHA CHEO MWALIMU MKUU

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Kasamwa ya mkoani Geita, Dennis Otieno anadaiwa kushushwa cheo kutokana na kuzuia wanafunzi kuvaa sare za CCM kwenye mahafali ya kidato cha nne.

Pia, taarifa hizo zinasema mkuu huyo wa shule alipinga kitendo cha baadhi ya walimu kuchangisha fedha wazazi wa watoto ambao ni wanachama wa Klabu ya Magufuli ili kufanya sherehe hilo kutokana na agizo la Rais la kufuta michango yote mashuleni.

Otieno, ambaye alikataa kuzungumzia suala hilo, anadaiwa kushushwa cheo kutokana na shinikizo la makada wa chama hicho tawala, hasa mwenyekiti wa CCM mkoani Geita, Joseph Kasheku, maarufu kwa jina la Msukuma, ambaye amethibitisha kushushwa cheo kwa mtumishi huyo wa umma.

Kwa mujibu wa taarifa hizo zilizosambazwa kwenye mitandao ya kijamii zinasema Otieno aligombana na mwalimu

CHANZO: MWANANCHI

MWALIMU ASHINDA KESI YA KUMTUKANA MWANAFUNZI WA KIDATO CHA 6 HUKO IRINGA

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Mahakama ya Mwanzo Iringa  Mjini imemuachia huru mwalimu wa Shule ya Sekondari ya Kiwele baada ya kukosa ushahidi wa kumtia hatiani katika kesi ya  kumtukana mwanafunzi.

Mwalimu huyo, Elizabeth Maliga (32) ameshtakiwa kwa madai ya kumtukana mwanafunzi huyo wa kidato cha sita, Rehema Mwakatobe na mama yake.

Amedaiwa kufanya kosa hilo wakati akimsainia Rehema barua ya kumuita mama yake kwenda shuleni hapo kusikiliza kosa la kuchelewa shuleni.

Hukumu hiyo imetolewa wakati Taifa likiwa kwenye mjadala mkubwa baada ya picha za video zilizosambaa mitandaoni kuonyesha kundi la walimu wa Shule ya Sekondari ya Kutwa ya Mbeya likimshambulia mwanafunzi Sestian Chikungu.

Tayari Serikali imeshatangaza kuwafukuza chuo walimu hao na Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi kwa ajili ya kuchukua hatua zaidi.

Akisoma hukumu ya kesi hiyo iliyochukua takriban dakika 45, Hakimu wa Mahakama hiyo,  Abdallah Kutvai alisema upande wa mashtaka umeshindwa kuishawishi mahakama kumtia hatiani mshtakiwa huyo.

“Jukumu la kuthibitisha kosa ni la upande wa mashtaka. Hiyo ni kwa mujibu wa kifungu cha tano cha Sheria ya Ushahidi ya Mahakama ya Mwanzo iliyofanyiwa marejeo mwaka 2002.

“Mashahidi wa upande wa mashtaka wametofuatiana tarehe za kutendwa kosa hilo. Shahidi namba moja ambaye ni mlalamikaji anasema kosa limetendeka Septemba 13, mwaka huu kwenye kikao cha kujadili mwenendo wa utekelezaji wa adhabu zilizotolewa na walimu kwa wanafunzi shuleni hapo,”alisema Hakimu Kutvai.

Amefafanua kuwa shahidi namba mbili alishindwa kubainisha siku ya tukio na kutaja tarehe tatu tofauti, ambazo ni Septemba 13, 14 na 15, siku ambayo mwanafunzi huyo alipewa barua ya kurudishwa nyumbani kwao Dar es Salaam kumfuata mzazi.

NECTA kuanza kukagua wenye Vyeti FEKI Kuanzia Kesho kwa Watumishi Wote

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Hatua ya Baraza la Mitihani nchini (Necta) kutoa ratiba ya kufanya uhakiki wa vyeti vya kidato cha nne, sita na ualimu kwa watumishi wote wa umma sasa ni wazi imezidi kupandisha joto kwa vigogo na watumishi mbalimbali ambao hawana sifa za kielimu kushika nafasi walizo nazo.

Katika taarifa yake ya sasa Baraza la Mitihani nchini, limetangaza kuwafuata katika maeneo yao ya kazi watumishi wote walioko katika mamlaka za mikoa, halmashauri na manispaa kwa ajili ya kufanya uhakiki wa vyeti vyao hivyo vya kitaaluma.

Kwa mujibu wa barua iliyosainiwa na  Edga Kasuga kwa niaba ya Katibu Mtendaji wa Baraza hilo kwenda kwa Makatibu tawala wa Mikoa, uhakiki utafanyika katika ofisi za Makatibu Tawala wa mikoa kuanzia Oktoba 10 hadi 14 mwaka huu, ingawa ratiba nyingine ya uhakiki imeonyesha zoezi hilo litafikia tamati Novemba 7 mwaka huu.

“Ili kufanikisha zoezi hilo Baraza limetaka kupata orodha (nakala- laini ya soft copy) ya watumishi wote wa umma waliopo katika Mkoa, Halmashauri na Manispaa.

“Nakala za vyeti vya kidato cha nne, cha sita na ualimu vya watumishi wote walioandikishwa na chumba cha kufanyia uhakiki,” inaeleza taarifa hiyo ya Baraza la Mitihani.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Baraza la Mitihani, uhakiki huo utafanywa katika makundi matano katika mikoa tofauti tofauti.

Oktoba 10, mwaka huu kundi la kwanza litafanya uhakiki katika Mkoa wa Mtwara, kundi la pili Singida, kundi la tatu Rukwa, kundi la nne Katavi na kundi la tano litakuwa Geita.

Oktoba 17 mwaka huu, kundi la kwanza litakuwa Lindi, la pili Manyara la tatu Songwe, la nne Kigoma na la tano litakuwa Mwanza.

Oktoba 24 mwaka huu, kundi la kwanza litakuwa Morogoro, la pili Arusha, la tatu Mbeya, la nne Tabora na la tano Mara.

Oktoba 31 mwaka huu, kundi la kwanza litakuwa Pwani, la pili Kilimanjaro, tatu Ruvuma, la nne Shinyanga na la tano Simiyu.

Novemba 7 mwaka huu, kundi la kwanza litakuwa Dar es Salaam, la pili Tanga, la tatu Njombe, la nne Dodoma na la tano Iringa.
==


WATOTO 22, MWALIMU WA MADRASA MBARONI KWA KUTUMIA MILIPUKO

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


POLISI Mkoa wa Pwani inawashikilia watoto 22 wa madrasa iitwayo Arahma iliyopo Kata ya Nianjema Tarafa ya Mwambao wilayani Bagamoyo kwa tuhuma za kujifunza namna ya kutumia milipuko.
Mbali ya kuwashikilia watoto hao, waliokamatwa walipokuwa wakijaribu kukimbia, kati yao 16 ni wa kike na sita wa kiume kwa ajili ya uchunguzi zaidi wa tukio hilo, pia inamshikilia mwalimu wao, Ashura Said (47) mkazi wa Kimarang'ombe Kata ya Nianjema kwa kwa tuhuma za kuendesha mafunzo ya kigaidi kwa watoto.
Kwa mujibu wa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Bonaventura Mushongi, Ashura Said mbaye ni mwalimu wa madrasa iitwayo Arahma, na alikamatwa wakati wa msako wakushitukiza uliofanywa na makachero wa jeshi hilo.
Mushongi amesema mtuhumiwa alikamatwa Oktoba Mosi saa tisa alasiri kutokana na taarifa zilizokuwa zimetolewa na raia wema juu ya mwenendo wa mwalimu huyo wa madrasa .
Alisema baada ya kumfanyia upekuzi, walikuta bomu moja la moshi lenye namba G2020c.SS-STCS katika makazi yake.
“Katika uchunguzi wa awali tumeweza kubaini kuwa makazi hayo yanamilikiwa na Taasisi ya Kiislamu iitwayo AKHA LAAGUL ISLAM iliyosajiliwa kwa lengo la utoaji huduma kwa watoto yatima kwa watoto kutoka maeneo mbalimbali kama vile Dar es Salaam, Handeni Tanga, Mlandizi na Bagamoyo kwa Mkoa wa Pwani, lakini badala yake wamekuwa wakitumika kwa mafunzo yasiyofaa kwa watoto wa kituo hicho,” alisema Kamanda Mushongi.
Katika tukio lingine, watu wasiofahamika wamevamia Ofisi ya Serikali ya Kijiji cha Kimanzichana Kusini na kumuua mtu mmoja na kumjeruhi mwingine kwa risasi.
Kamanda Mushongi alisema tukio hilo ni la juzi saa 11 alfajiri katika Kitongoji cha Ukwama Kata ya Kimanzichana Tarafa ya Mkamba Wilaya ya Mkuranga, wakati aliyeuawa akiwa anajaza fomu za mkopo wa Benki ya Akiba Commercial Bank (ACB) ni Bakar Said (45) mkazi wa Kimazinchana Kusini.
“Watu wawili walivamia ghafla wakiwa na silaha mbili na kuanza kuwafyatulia risasi ambazo zilimpiga Bakari na kutoweka kusikojulikana wakitumia pikipiki,” alisema Mushongi.
Alisema mtu huyo aliuawa kwa kupigwa risasi kifuani upande wa kulia na kutokea chini ya bega la kushoto mgongoni. Mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mkuranga na utakabidhiwa kwa ndugu zake mara baada ya uchunguzi kukamilika.
Aidha, katika tukio hilo, Omary Ally (55) ambaye ni Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Kimanzichana Kusini, alijeruhiwa kwa kupigwa risasi kwenye mkono wa kushoto na amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mkuranga kwa matibabu.
“Katika eneo la tukio kumekutwa maganda mawili ya risasi yanayotumika kwenye silaha ya SAR/SMG na tunapenda kuwahakikishia wananchi wote usalama wao na kwamba tutahakikisha tunapambana kwa nguvu zetu zote na wale wote wenye nia ya kuwatia hofu wananchi hawataweza kufanikiwa katika mipango yao waliodhamiria," alisema.

MKUU WA SHULE YA SEKONDARI YA MBEYA DAY ASIMAMISHWA KAZI BAADA YA TUKIO LA KUPIGWA MWANAFUNZI SHULENI HAPO

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.




UPDATES:WAZIRI NDALICHAKO AWATIMUA CHUO WALIMU WA MAFUNZO WALIOMPIGA MWANAFUNZI SHULE YA KUTWA MBEYA

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Hatimaye Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Ndalichako amewafukuza chuo walimu waliohusika na kumpiga mwanafunzi wa kidato cha tatu wa shule ya kutwa Mbeya.

Mpaka sasa Mkuu wa Shule na baadhi ya walimu wamefikishwa katika kituo cha polisi kwa mahojiano kuhusiana na tukio hilo.

Chanzo: TBC, habari za mikoani

WAZIRI MWIGULU NCHEMBA ALIAGIZA JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA KUWAKAMATA WALIMU WOTE WALIOMUADHIBU MWANAFUNZI KIKATILI

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba ameagiza Jeshi la Polisi mkoani Mbeya kuwakamata walimu walioonekana kwenye video wakimwadhibu mwanafunzi vibaya. Tukio hilo lilitokea 28. September.

Mnamo Tarehe 28.9.2016, mwanafunzi aitwaye Sebastian Chinguku wa form 3A mbeya day sec school aishie Uyole alipigwa na walimu watatu, Mwl Frank Msigwa, John Deo UDSM na Sanke Gwamaka wa Nyerere Memorial, wote wakiwa mafunzo. 

Mwl Frank alitoa assignment ya Kingereza na baadhi ya wanafunzi hawakufanya akiwepo Sebastian , darasani mwl alimpiga kofi kijana na kijana akahoji kwanini anampiga wakashikana koo, ndipo walimu wakamchukua na kumpeleka staff room na kuanza kumpiga .

Tangu tar 29. September mwanafunzi hakuonekana shuleni. Na mwl E.H wa Iringa University ndio aliyekuwa akisema mwacheni mtamuumiza  na ndiye  aliyechukua video.

Hao walimu wote hawapo wameondoka kwenda kwenye vyuo vyao. POLISI wanaendelea kuwahoji uongozi wa Mbeya Day Sec School na Mwanafunzi aliyeumizwa ikiwepo kumpeleka hospitali.

Nimeelekeza vyombo vya dola Dar wawatafute chuoni kwao hao walimu kuhusiana na shambulio hilo kwa mwanafunzi huyo.
 Tazama hapa video ya walimu wakimpiga mwanafunzi hapa chini

MWALIMU AHUKUMIWA MIAKA MITATU JELA KWA KUOMBA RUSHWA YA SH. 130,000

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Mahakama  ya Hakimu Mkazi ya Bukombe mkoani Geita imemhukumu Mwalimu wa Shule ya Msingi Umoja, Daniel Nyingati kwenda jela miaka mitatu au kulipa faini ya Sh milioni 1.6 baada ya kupatikana na makosa ya  kuomba na kupokea rushwa.

Hukumu hiyo ilitolewa juzi na Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Bukombe, Gabriel Kurwijila.

Alisema  mshitakiwa Nyingati amekutwa  na hatia ya kuomba  rushwa ya  Sh 130,000 kutoka kwa Marco Elias  aweze kumdahili mtoto wake aliyekuwa amehitimu  masomo ya shule ya msingi kinyume na sheria.
Hakimu Kurwijila alisema   ushahidi ulitolewa mahakamani pande zote mbele ya  waendesha mashitaka kutoka  Taasisi ya Kuzuia na Kudhibiti Rushwa Tanzania (Takukuru), Kelvin Murusuri na  Husna Kiboko umejitosheleza na kumtia hatiani mwalimu Nyingati.

Alisema mahakama inamhukumu mwalimu Nyingati kwenda jela miaka mitatu au kulipa faini ya Sh milioni 1.6 kwa kuwa alitenda kosa la kuomba na kupokea rushwa.