HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

WANAWAKE WASHIKA NAFASI MBALIMBALI ZA UONGOZI MASOKONI JIJINI DAR ES SALAAM

 Mwenyekiti wa Soko la Gezaulole lililopo Kiwalani Bomu bomu, Muhidin Waziri 'Ndolanga' akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kuhusu changamoto iliyokuwepo katika soko hilo juu ya vitendo vya ukatili wa kijinsia ambavyo hivi sasa vimedhibitiwa baada ya kupata mafunzo kutoka Shirika la Equality for Growth (EfG). Kulia ni Mwezeshaji wa Kisheria wa soko hilo.
 Mwezeshaji wa Kisheria katika soko hilo, Amina Mussa 
akizungumza na wanahabari.
 Mfanyabiashara katika soko hilo, Zena Mohamed akielezea wanawake kupiga hatua ya maendeleo baada ya kupata mafunzo hayo yaliyotolewa na EfG.
 Wanawake wakipata mahitaji mbalimbali katika soko hilo.
 Mteja akinunua bamia.
 Mfanyabiashara, Mzee Mohamed Bawe akisubiri wateja.
 Mfanyabiashara Mwantum Mohamed akizungumza na waandishi (hawapo pichani ), kuhusu kupungua kwa vitendo vya ukatili katika soko hilo la Gezaulole.
 Mfanyabiashara wa kisamvu katika soko hilo, Asna Andrew (katikati), akitwanga kisamvu tayari kwa kukiuza. Alisema ushirikiano baina ya wafanyabiashara na viongozi umeleta tija ya kukabiliana na vitendo vya ukatili wa kijinsia.
 Mfanyabiashara wa Soko la Tabata Muslim, Sauda Kalengela akizungumza kupungua kwa ukatili wa kijinsia.
 Muuza samaki wa kukaanga katika Soko la Tabata Muslim, Anthony Venance akionesha miundombinu mibovu katika soko hilo. Katika masoko kukikosekana miundombinu mizuri wakati Manispaa zinazosimamia masoko hayo zikitoza ushuru bila kukarabati miundombinu hiyo pia ni ukatili wa kijinsia kwa wanatumiaji wa  masoko hayo.
 Mwezeshaji wa kisheria katika soko la Tabata Muslim, Aisha Juma akizungumzia ukatili wa kijinsia aliofanyiwa mwanaume mmoja katika maeneo ya Tabata ya kuporwa vyombo vyake na mke wake.
Mwezeshaji wa kisheria katika soko la Tabata Muslim, Irene Daniel akizungumzia wanawake katika soko hilo kujitambua na kushika nafasi mbalimbali za uongozi baada ya kuwezeshwa na EfG.


Na Dotto Mwaibale

WANAWAKE Wafanyabiashara katika masoko jijini Dar es Salaam hasa yale yaliyowezeshwa mafunzo na Shirika la Equality for Growth (EfG) wamejitambua na kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika maeneo yao ya biashara.

Hayo yamebainishwa na Mwezeshaji wa Kisheria katika Soko la Tabata Muslim, Irene Daniel wakati akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana kuhusu faida waliyoipata baada ya kupata mafunzo ya kupinga ukatili wa kijinsia katika masoko kupitia Shirika la Equality for Growth (EfG)

"Kwa kweli wanawake hivi sasa tupo imara, tunajitambua na tunauthubutu baada ya kupata dozi kutoka EfG kwani hapo awali tulikuwa waoga na hatukuzijua haki zetu ndio maana tulikuwa nyuma kimaendeleo" alisema Daniel.

Alisema baada ya kupata mafunzo hayo na kuwezeshwa kuzijua sheria na mambo yaliyokuwa yakimdhalilisha mwanamke hali imekuwa shwari katika masoko kwani hivi sasa wanafanya biashara zao katika mazingira salama.

Alisema kutokana na hali hiyo wanawake wameweza kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi na kuwa wajumbe katika kamati za masoko jambo ambalo ni la kujivunia.

"Tuna kila sababu ya kulishukuru shirika hilo kwani sasa tumeweza kufungua akaunti zaidi ya moja baadhi yetu wamefanikiwa kununua hata magari na tunaendelea na biashara zetu bila ya kuwepo vitendo vya udhalilishaji kama ilivyokuwa siku za nyuma" aliongeza Daniel.

Mfanyabiashara mwingine katika soko hilo ambaye pia ni Mwezeshaji wa Kisheria Aisha Juma alisema mafunzo hayo waliyopata ya uwezeshaji wa kisheria yamesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza kama sio kumaliza kabisa vitendo vya ukatili wa kijinsia masokoni na hata majumbani.

Alisema elimu hiyo waliyoipata kupitia EfG imesaidia sana kuweka mambo sawa na ushirikiano baina yao katika masoko kwani leo hii hakuna mtu wa kumnyanyasa mwenzake kutokana na jinsia yake na anayebainika amekuwa akichukuliwa hatua.

Akitolea mfano alisema ukatili wa kijinsia hafanyiwi mwanamke peke yake kwani yeye ameweza kusimamia moja ya kesi ya ukatili wa kijinsia aliofanyiwa mwanaume mmoja maeneo ya Tabata baada ya kuporwa vitu vyake vya ndani na mke wake ambaye alisaidiana na mama yake licha ya vitu hivyo kununua mwanaume huyo. 

Mfanyabiashara katika Soko la Gezaulole lililopo Kiwalani Bomubomu, Mwantum Mohamed alisema wanawake katika soko hilo wana nguvu ya pamoja jambo lililosaidia kuondoa kabisa vitendo vya ukatili wa kijinsia,

Mwenyekiti wa Soko hilo, Muhidin Waziri 'Ndolanga' alisema faini ya sh.10,000 anayotozwa mtu atakayebainika kutoa lugha ya matusi au kumdhalilisha mtu yeyote kwenye soko hilo imesaidia kuwatsha watu wenye nia ya kutenda kosa hivyo kulifanya soko hilo kuwa eneo salama la kutafuta riziki na si matusi.

Shirika hilo liliendesha mafunzo na kufanya kampeni ya kupinga ukatili wa kijinsia katika masoko ya Ferry, Temeke Sterio, Tabata Muslim, Gezaulole, Kisutu na  Ilala Mchikichini yote yakiwa jijini Dar es Salaam ambapo kampeni hiyo pia inafanyika katika Mikoa ya Mwanza na Tanga.

MAONYESHO YA KIMATAIFA YA TASWE YAANZA KWA KISHINDO UKUMBI WA CARDINAL RUGAMBWA OYSTERBAY - DAR

Maonyesho ya Kimataifa ya Ushirika wa akinamama wajasiliamali wa Tanzania (TASWE) yameanza kwa kishindo leo katika ukumbi wa Cardinal Rugambwa Oysterbay. Akizungumza kwa juu ya maonyesho hayo, mwenyekiti na mwanzilishi wa Taswe Saccos, Bi Anna Matinde alisema "Maonyesho haya yamekuwa na hamasa kubwa wafanyabiashara na bidhaa kutoka Comorro, Afrika Mashariki na mikoa mbalimbali nchi zinapatikana hapa kwa wingi na kwa bei nafuu. "Tunawakaribisha wote mje mkutane na wafanyabiashara hawa pamoja na wadau wetu na kujionea bidhaa mbalimbali. Maonyesho yanaaza saa 2 asubuhi mpaka saa 2 usiku", . Aliongeza Anna Matinde.
Mfanyabiashara kutoka Comorro, Siti Marahaba akiuza baadhi ya bidhaa zake katika maonyesho ya kimataifa ya Taswe
 Bi Sarah Abiudi akionyesha bidhaa za kiafrika zinazopatika katika maonyesho ya Taswe.
 Bi. Arafa Awadhi Mfanyabiasha mwanachama wa Taswe (kulia) akitoa maelezo juu ya bidhaa zake na mmoja ya mteja aliyetembelea maonyesho hayo
 Wafanyabiashara kutoka zanzibar wakionyesha bidhaa mbalimbali za kiasili zinazopatikana katika maonyesho ya kimataifa ya TASWE
 Mjasiliamali kutoka Nairobi Kenya, Bi Jesca Alphonce akionyesha namna ya ktumia moja kati ya bidhaa za urembo kwa wateja waliojitokeza kwenye maonyesho hayo
 Mfanyabiasha na mwanachama wa Taswe bi. Elizabeth akionyesha bidhaaa kwa wateja waliotembelea maonyesho
 Maonyesho haya ya akina mama wanachama wa Taswe yanaendelea ukumbi wa Cardinal Rugambwa Oysterbay ambapo yalifunguliwa jana Machi 25, 2017 na kilele chake kitakuwa 31.03.2017.

Joint UN Women and UNESCO Message for International Women's Day - 08 March 2017

Joint Message from UN Women Representative, Maria Karadenizli and UNESCO Head of Office and Representative for the United Republic of Tanzania, Ms Zulmira Rodrigues on International Women’s Day -Everybody has a stake in promoting equality between men and women, at all levels of society 
“The story of women's struggle for equality belongs to no single feminist nor to any one organization but to the collective efforts of all who care about human rights.” These words by activist Gloria Steinem testify to the universal nature of the fight for women’s rights and once a year, on 8 March, we restate our commitment to gender equality as a force driving dignity for all.
 Inequality between men and women penalizes societies at all levels of development. The violence, injustice and stereotypes suffered by too many women in their personal or professional lives undermine society as a whole, and deprive of it considerable potential for creativity, strength and confidence in the future. 
As the United Nations has adopted the ambitious 2030 Agenda for Sustainable Development, the full empowerment of girls and women is one of humanity’s most powerful levers for development. Rural women are directly responsible for the production of half the world’s food – and it is primarily women who manage and gather natural resources. Ninety per cent of rapes in the world take place precisely when women are on their way to collect water or firewood. 
Two thirds of illiterate adults in the world are women. One in three women is subject to physical violence in the private sphere, and the wage gap between men and women, for equal work and with equal skills, is a fact across the world. For UNESCO, the main engine for change rests on education, training, and the possibility given to all girls and women of pursuing careers in research, politics and culture. Equality also lies in ridding the media and collective imagination of prejudice by highlighting the women scientists, artists and politicians who are moving humanity forward in all fields.
 On the occasion of this 2017 International Women’s Day, UNWOMEN and UNESCO call on all to make a commitment to women’s’ rights, and thereby enhance rights and dignity for all.

AFISA MAENDELEO JIJI LA TANGA AFUNGUA KONGAMANO LA WANAWAKE LA JIJIN HILO AWATAKA KUTUMIA FURSA ZA KIUCHUMI KUJIPATIA MAENDELEO

 Afisa Maendeleo ya Jamii wa Jiji la Tanga,Mwatumu Dossi akifungua kongamano la Wanawake Jijini Tanga ambalo lilikuwa na lengo kuu la kujadili masuala mbalimbali ya kiuchumi kwa wanawake ikiwemo fursa za kiuchumi sambamba na kupambana na dawa za kulevya kwa jamii lililofanyika ofisi ya mkuu wa mkoa wa Tanga leo.
 Afisa Maendeleo ya Jamii wa Jiji la Tanga, Mwatumu Dossi  wa pili kutoka kulia akiteta jambo na Mkurugenzi wa Taasisi ya Tree of Hope ya Jijini Tanga, Fortunata Manyeresa wakati wa kongamano la wanawake Jijini Tanga kuelekea siku ya wanawake dunia kushoto ni Rehema na Yahaya Seumbe ambaye ni Afisa kutoka Ofisi ya Maendeleo ya Jamii kwenye Jiji la Tanga wakifuatilia kongamano hilo.
 Baadhi ya Wakina wanawake jijini Tanga  wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa kwenye kongamano hilo
 Sehemu ya Umati wa wanawake wakifuatilia kwa umakini kongamano hilo la wanawake wa Jiji la Tanga kuelekea siku ya wanawake Dunia ambapo kilele chake itakuwa ni Machi 8 mwaka huu
 Baadhi ya waandishi wa habari jijini Tanga wakifuatilia kwa umakini kongamano hilo wa kwanza kulia ni Burhan Yakub wa gazeti la Mwananchi,Bertha Mwambele wa TBC TV na Sussan Uhinga wa Clous TV
 Sehemu ya wakina wanawake Jijini Tanga wakifuatilia kwa umakini kongamano la wanawake kuelekea siku ya wanawake ambapo kilele chake ni Machi 8 mwaka huu
 Afisa Maendeleo ya Jamii wa Jiji la Tanga,Mwatumu Dossi akizungumza na waandishi wa habari jijini Tanga kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake Dunia Machi 8 mwaka huu mara baada ya kufungua kongamano la wanawake Jijini Tanga.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Tree of Hope ya Jijini Tanga, Fortunata Manyeresa akizungumza na waandishi wa habari jijini Tanga baada ya kumalizika kwa kongamano hilo ambapo alisema kuelekea siku ya wanawake kutafanyika shughuli mbalimbali za kijamii
Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha

WAZIRI MWIJAGE AZINDUA AWAMU YA PILI YA MAFUNZO YA WAJASILIAMANI WASICHANA YA TAASISI YA MANJANO

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage  akipokelewa na Mwasisi wa Taasisi ya Manjano na Mmiliki wa Shear Illusions, Shekha Nasser mara baada ya kuwasili kwa ajili ya ufunguzi wa mafunzo kwa wanawake ikiwa ni awamu ya pili.
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage akipata maelezo kutoka kwa Mwasisi wa Taasisi ya Manjano na Mmiliki wa Shear Illusions, Shekha Nasser  kuhusu darasa linalotumika katika ufundishaji wa wasichana hao leo katika ofisi ya Shear Illusion iliyopo jengo la Millenium Tower jijini Dar
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage akizungumza na wanafunzi wa Manjano Academic mara baada ya kufika na kujionea mafunzo hayo leo katika ofisi ya Shear Illusion jijini Dar
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage akizungumza wakati wa uzinduzi wa programu ya kuwawezesha wanawake kiuchumi ijulikanayo kama "Manjano Dream Makers" kwa awamu ya pili iliyozinduliwa leo na waziri huyo katika ukumbi wa LAPF Millenium Towers jijini Dar es Salaam leo.
Mwasisi wa Taasisi ya Manjano na Mmiliki wa Shear Illusions, Shekha Nasser akizungumza kuhusu uzinduzi rasmi wa program ya ajira kupitia tasnia ndogo ya urembo pamoja na kufanya utambulisho kwa wageni waalikwa.
Afisa Kutoka TFDA Bi. Grace Shimwela akizungumzia umuhimu wa kupata vibali vya urembo "Cosmetics and Personal Care" kwa wanawake walioko na ambao wamemaliza progamu mbalimbali za mafunzo kutoka kwa Manjano Dream Maker ili kuwasaidia pale wanapoanza kujitegemea
Jokate Mwegelo akizungumza jambo kwenye ufunguzi huo
Mshiriki mmoja aliyenufaika na Taasisi ya Manjano, Josephine Rwetela akizungumzia umuhimu wa kutengeneza ajira kupitia Tasnia ndogo ya Urembo nchini.
Mkurugenzi wa GS1 Tanzania, Fatma Khange akitoa maneno ya shukrani kwa wageni waalikwa pamoja na wanawake wanaoshiri kwenye mafunzo hayo yaliyoziduliwa leo na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage.
Baadhi ya washiriki walioudhuria katika uzinduzi huo
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage akimkabidhi cheti Mkurugenzi Mtendaji 8020 Fashion na Mentor wa Taasisi ya Manjano Foundation, Shamim Mwasha
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage akimkabidhi cheni Mentor wa Taasisi ya Manjano Foundation, Mboni Masimba
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage  akimkabidhi cheti Mentor wa Taasisi ya Manjano Foundation, Mariam Marion Ndaba
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage  akiwa kwenye picha ya pamoja na Manjano Academic
Mgeni rasmi Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage akiwa kwenye picha ya pamoja na Mentor wa Taasisi ya Manjano Foundation.
Mgeni rasmi Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Mh. Charles Mwijage akiwa kwenye picha ya pamoja na Dream Makers.


Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii
Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji ,Charles Mwijage amewataka watanzania kuwekeza katika mfumo unaoweza kutoa ajira za moja kwa moja kwa vijana kama ilivyo katika kampuni ya Manjano Foundation.

Mwijage amesema hayo mapema leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akifungua mafunzo ya wanafunzi 30 juu ya masuala ya urembo yanayoendeshwa ta tasisi ya Manjano Foundation ya hapa hapa nchini.

“huyu ni moja ya wawekezaji ambao wanapaswa kuungwa mkono na kila mmoja kwani ameamua kuwekeza kwa kutengeneza bidhaa ambazo zinatumia malighafi kutoka hapa hapa nchini na kuamua kuwawezesha wanawake wadogo kupata mafunzo hili waweze kuingiza pesa kupitia bidhaa hizo” amesema Waziri Mwijage.

Mwijage ameongeza kuwa mbali na Manjano foundation kutoa elimu ya ujasiliamali kwa wasichana hao pia ipo katika mpango kabambe wa kujenga kiwanda mjini kibaha ambapo tayari wameshapata ekeri tatu kwa ajili yakujenga Godown ambalo litasaidia kufanya uzalishaji.

Kwa upande wake mkurugenzi wa Manjano Foundation Shekha Nasser amesema kuwa wasichana ambao wanapata mafunzo kutoka tasisi hiyo wanaweza kuingiza kiasi cha Milioni mbili mpaka tatu kwa mwezi.

Aidha ametaja kuwa program hiyo katika mwaka hu itaweza kuwafikia wanawake katika mikoa mitano nchini hili waweze kujikwamua kiuchumi.