HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

NDALICHAKO KUMALIZA MIGOGORO YA WALIMU KWA KUSHIRIKIANA NA WIZARA NYINGINE

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


  Mwenyekiti wa Mkutano wa mawaziri wa Afrika Mashariki wa kujadili namna ya kufanikisha lengo la nne la elimu (SDG4) kati ya malengo 17 ya dunia ya maendeleo endelevu ambaye pia ni Mkurugenzi wa UNESCO Kanda ya Mashariki mwa Afrika, Bi. Ann Therese Ndong-Jatta akiendesha mjadala wa kuhitimisha mkutano huo wa siku mbili wa wadau wa elimu kutoka nchi 13 uliofanyika katika ukumbi wa Julius Nyerere International Conventional Centre (JNICC) jijini Dar es Salaam. (Habari picha na Zainul Mzige)
Mkurugenzi Mwandamizi wa Uendeshaji kutoka Taasisi ya XPRIZE, Matt Keller, iliyona makazi yake nchini Marekani akielezea kuhusu mradi wa XPRIZE unahusisha watoto ambao hawapo shuleni ukiwa na malengo ya kukuza teknolojia ya dunia kwa kutumia uwezo walionao ukilenga watoto wa miaka 5-12 wakati wa kuhitimisha mkutano wa mawaziri wa Afrika Mashariki wa kujadili namna ya kufanikisha lengo la nne la elimu (SDG4) kati ya malengo 17 ya dunia ya maendeleo endelevu uliofanyika jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Profesa Joyce Ndalichako akielezea jitihada zitakazofanywa na serikali ya Tanzania katika kuboresha sekta ya elimu kuelekea utekelezaji wa SDG4 kwenye mkutano wa siku mbili wa mawaziri wa Afrika Mashariki wa kujadili namna ya kufanikisha lengo la nne la elimu (SDG4) kati ya malengo 17 ya dunia ya maendeleo endelevu uliofanyika jijini Dar es Salaam
 Waziri wa Elimu, Rasilimali Watu na Tafiti za Kisayansi wa Mauritius, Leela Dookon Luchoomon (kushoto) akieleza mipango ya serikali yake katika kuboresha elimu wakati wa kuhitimisha Mkutano wa mawaziri wa Afrika Mashariki wa kujadili namna ya kufanikisha lengo la nne la elimu (SDG4) kati ya malengo 17 ya dunia ya maendeleo endelevu uliofanyika jijini Dar es Salaam na kuandaliwa na UNESCO kwa kushirikiana na ILO, UNFPA, UNDP, UNICEF, UN Women, UNHCR pamoja na World Bank.
 Balozi wa Canada nchini Tanzania, Ian Myles akizungumza kwa niaba ya nchi wahisani wakati wa kuhitimisha Mkutano wa mawaziri wa Afrika Mashariki wa kujadili namna ya kufanikisha lengo la nne la elimu (SDG4) kati ya malengo 17 ya dunia ya maendeleo endelevu
 Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi wa Djibouti, Mh. Moustapha Mohamed Mahamoud akiwasilisha mapendekezo ya serikali yake katika kuhitimisha Mkutano wa mawaziri wa Afrika Mashariki wa kujadili namna ya kufanikisha lengo la nne la elimu (SDG4) kati ya malengo 17 ya dunia ya maendeleo endelevu uliofanyika jijini Da es Salaam.
 Waziri wa Elimu na shule za msingi wa Uganda, Mh. Nansubuga Rosemary Seninde (kulia) akitoa mapendekezo ya serikali yake katika kuboresha elimu kwenye mkutano wa siku mbili wa mawaziri wa Afrika Mashariki wa kujadili namna ya kufanikisha lengo la nne la elimu (SDG4) kati ya malengo 17 ya dunia ya maendeleo endelevu uliofanyika jijini Da es Salaam. Kushoto ni Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe Riziki Pembe Juma.

Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Mh. Mhandisi Stella Manyanya (kulia) na Naibu Katibu Mkuu wa wizara hiyo Dkt. Leonard Akwilapo wakiandika mapendekezo muhimu yaliyokuwa yakiwasilisha kwenye mkutano wa mawaziri wa Afrika Mashariki wa kujadili namna ya kufanikisha lengo la nne la elimu (SDG4) kati ya malengo 17 ya dunia ya maendeleo endelevu uliofanyika jijini Da es Salaam.

 Sehemu ya mawazi wa elimu kutoka Kenya, Uganda, Sudan Kusini, Ethiopia, Somalia, Comoro na Djibouti walioshiriki kwenye mkutano wa mawaziri wa Afrika Mashariki wa kujadili namna ya kufanikisha lengo la nne la elimu (SDG4) kati ya malengo 17 ya dunia ya maendeleo endelevu uliofanyika jijini Da es Salaam.
  Sehemu ya wadau wa sekta ya elimu kutoka nchi 13 walioshiriki kwenye mkutano wa siku mbili wa mawaziri wa Afrika Mashariki wa kujadili namna ya kufanikisha lengo la nne la elimu (SDG4) kati ya malengo 17 ya dunia ya maendeleo endelevu uliofanyika jijini Da es Salaam.
 Mwenyekiti wa Mkutano wa mawaziri wa Afrika Mashariki wa kujadili namna ya kufanikisha lengo la nne la elimu (SDG4) kati ya malengo 17 ya dunia ya maendeleo endelevu ambaye pia ni Mkurugenzi wa UNESCO Kanda ya Mashariki mwa Afrika, Bi. Ann Therese Ndong-Jatta akifuatilia mijadala mbalimbali iliyokuwa ikiwasilishwa na wadau wa sekta ya elimu wakati wa mkutano huo uliofanyika jijini Da es Salaam.
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Zulmira Rodrigues (katikati) akibadilishana mawazo na baadhi ya washiriki wa wa mkutano wa siku mbili wa mawaziri wa Afrika Mashariki wa kujadili namna ya kufanikisha lengo la nne la elimu (SDG4) kati ya malengo 17 ya dunia ya maendeleo endelevu uliofanyika jijini Da es Salaam.
 Baadhi ya wafanyakazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) walioshiriki kufanikisha mkutano wa siku mbili wa mawaziri wa Afrika Mashariki wa kujadili namna ya kufanikisha lengo la nne la elimu (SDG4) kati ya malengo 17 ya dunia ya maendeleo endelevu uliofanyika jijini Da es Salaam.
Afisa mipango kutoka UNESCO, Bi Faith Shayo (kushoto) akijadiliana jambo na wafanyakazi wenzake wakati wa mkutano wa siku mbili wa mawaziri wa Afrika Mashariki wa kujadili namna ya kufanikisha lengo la nne la elimu (SDG4) kati ya malengo 17 ya dunia ya maendeleo endelevu uliofanyika jijini Da es Salaam.


Na Zainul Mzige
Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Profesa Joyce Ndalichako amesema kwamba wizara yake itashirikiana na wizara nyingine nchini kuhakikisha kwamba migogoro ya walimu inamalizwa ili kufanikisha utoaji wa elimu kuwa bora na jumuishi.
Kauli hiyo aliitoa wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari katika siku ya pili ya kuhitimisha kwa mkutano ulioshirikisha nchi 13 za Afrika Mashariki kujadili lengo la nne la elimu kati ya malengo 17 ya maendeleo endelevu (SDGs)
Alisema kwamba migogoro ya walimu inayogusa mishahara, marupurupu pamoja na mazingira bora ya kazi linagusa pia Wizara za TAMISEMI na UTUMISHI na kusema kwamba wao kama wasimamizi wa elimu watakachoweza kufanya ni kuzungumza na wenzao kuhakikisha kwamba migogoro hiyo inafutwa ili utoaji wa elimu uendane na mipango ya kitaifa na kidunia ya lengo la maendeleo 2030.
Pamoja na kujibu swali hilo Prof Ndalichako alizungumzia  kwamba walimu walikuwa ni ajenda muhimu  na humo walikubaliana kwamba mwalimu ni kila kitu katika utoaji wa elimu na kuwa hawawezi kufanikiwa katika elimu bora na jumishi bila kuwa na walimu wenye umahiri, wanaowezeshwa kufanya hivyo.
Kutokana na ukweli huo wamejipanga kuhakikisha kwamba walimu wanapata mafunzo bora na kuwakutanisha kubadilishana uzoefu.
Alisema kila nchi itakuwa na mpango mkakati wake na kuonesha viashiria kwamba vinatekelezwa kwa namna gani. Mwisho wa siku mwaka 2030 mataifa yote yanapaswa kuhakikisha kwamba agenda namba 4 ya maendeleo endelevu ya elimu imetekelezwa.
Alisema katika mkutano huo wa siku mbili wa mawaziri wa elimu ulioandaliwa na UNESCO kwa kushirikiana na ILO, UNFPA, UNDP, UNICEF, UN Women, UNHCR pamoja na World Bank wamebainisha kwamba mikakati ya pamoja ni lazima ichukuliwe ili kufanikisha elimu jumuishi yenye usawa na ubora kwa watu wote huku ikitoa fursa ya elimu kwa wakati wote.
Alisema kwamba mkutano ulitambua kwamba elimu haina mwisho, elimu inataka kuwa na mfumo wa kuwa na maendeleo ya kujifunza kwani mambo hayasimami kutokana na kubadilika kwa teknolojia, hivyo elimu inayotolewa haina budi kujazia nafasi hiyo kwa kuwapa uhuru watu kujisogeza zaidi.
Alisema nchi hizo 13 zimekubaliana kwa pamoja kufikia malengo endelevu 2030 kama yalivyosainiwa na kila nchi mwaka 2015 kwa kuweka mikakati ili mataifa hayo yaweze kufikia malengo yanayotakiwa.
Aidha alisema kama walikubaliana kwanza kuimarisha elimu ya awali kwa lengo la kuweka msingi wa kujifunzia, kwani ipo methali inayoaminika kwamba samaki mkunje angali mbichi na taifa likitaka watoto wasome ni lazima kuwaanzia wadogo.

Aidha  mataifa hayo yamekubaliana upimaji wa wanafunzi kufanyika kwa ajili ya kujifunza, ukilenga kutumia matokeo kuandaa mafunzo kwa wanafunzi. Upimaji uoneshe eneo la ambalo walimu watalazimika kufanya kazi ya ziada ili wanafunzi wao waelewe.
Mfumo wa sasa wa kupima umelenga kujua watoto wangapi wamefaulu na wangapi wamefeli.
Ndalichako alisema ni vyema upimaji huo kutumika kuimarisha mafunzo ya walimu.
Jambo la tatu ambalo walikubaliana ni kuhakikisha kwamba mtoto wa kike anasoma na wale wenye mazingira hatarishi pia; na bila kujali kujali mazingira yao nchi zinatakiwa kuweka mikakati ya  elimu iliyobora kwa wote.
"Suala muhimu katika elimu ni kupanga mipango sahihi. Takwimu sahihi ni changamoto kutokana na ukweli kuwa takwimu hazipatikani kwa wakati au hazina usahihi au hazifanyiwi uchambuzi katika kufanya maamuzi vizuri, " alisema Prof Ndalichako.
Pia mataifa hayo yakiwemo Tanzania, Kenya, Uganda, Sudan Kusini, Ethiopia, Somalia, Comoro na Djibouti yamesisitiza haja ya kuimarisha elimu nje ya mfumo rasmi na kwa kuwa kuna mfumo wa elimu wa kujiendeleza wa wakati wote mfano wa uhasibu.
Alisema inafaa kuimarisha mifumo ya elimu nje ya mfumo rasmi bila kusahau elimu ya watu wazima. Pia wametaka watoto wanaolikoroga kwa sababu moja au nyingine na kujikuta hawapati masomo ni vyema wakarudishwa shuleni kuendelea na masomo hivyo ipo haja ya kutengeneza mfumo wa kupata elimu kwa staili hiyo.

"Katika hili tumekubaliana watoto walionje ya shule wanarudi shuleni au wanatengeneza mfumo wa kupata elimu" alisema na kuongeza kuwa pia ilionekana ipo haja ya kuimarisha elimu na ufundi stadi ili elimu hiyo imwezeshe kujiajiri, kujijenga na kuwa na ujuzi kuendana na soko la ajira.
Aidha alisema kwamba  kunatakiwa kuanzishwa kwa kampeni maalumu ya kufichua wasichana wasiopelekwa shule ili kuwepo mwenedelezo wa kila mtu kuingia shule.
WAKATI huo huo serikali ya Uganda imesema itaongeza nguvu katika shule za awali kuimarisha msingi wa utoaji elimu kwa watu wake.
Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Elimu na shule za msingi wa Uganda, Mh. Nansubuga Rosemary Seninde wakati akizungumza katika mkutano wa mawaziri wa Afrika Mashariki kuhusiana na lengo namba 4 la elimu kati ya malengo 17 ya dunia.
Alisema serikali yake imejikita katika kuhakikisha kwamba waganda wanapata elimu nzuri na yenye ushindani ikihakikisha ujuzi na uzoefu katika ujuzi.
Aklisema nchi yake haiwezi kumpa mtu digrii mpaka awe amefanya “intern” na hilo linasaidia sana kujenga uzoefu wa kile alichosomea.
Alisema ingawa kuna tatizo la bajeti, mipango ni muhimu kuhakikisha kwamba taifa linatoka katika changamoto za utoaji wa elimu bora.

Alisema badala ya kusubiri sera, watendaji wanatakiwa kuangalia maeneo ya kuanzia na kisha kutengenezea taratibu za kubadilishwa kwa sera ili iendane na kasi inayotakiwa.

13 COUNTRIES SITS IN DAR TO DISCUSS EDUCATION

Chair of the Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African in Dar es Salaam and Head Office and country Representative of UNESCO, Zulmira Rodrigues welcomes invited guests, dignitaries and key speakers during Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African in Dar es Salaam. (All photos by Zainul Mzige)

The Minister for Education, Science, Technology and Vocational Training Prof Joyce Ndalichako delivering key note address to officiate Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African in Dar es Salaam.
Unesco Regional Office for Eastern Africa, Director Mrs Ann Therese Ndong-Jatta addressing Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African in Dar es Salaam.
UNHCR Head Regional Services Center, Mrs Victoria Akyeampong, gives her statement at the National Forum Session during the Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African in Dar es Salaam.
Linda Madete from UNESCO Office Dar es Salaam gives out some of the education materials and brochures to invited guests during the Ministerial Sustainable Development Goals numbers 4 that focuses on ensuring inclusive and equitable quality education and promote lifelong learning opportunities for all at the Regional Forum for Eastern African in Dar es Salaam.
The Minister for Education, Science, Technology and Vocational Training, Prof Joyce Ndalichako (far left) arrives at Julius Nyerere International Convention Centre (JINCC )to attend the Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African in Dar es Salaam.
Norwegian Ambassador to Tanzania, Hanne-Marie Kaarstad tete-a-tete with the UNHCR Representative to Tanzania, Chansa Ruth Kapaya at the Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African.
Swedish Ambassador to Tanzania H.E Katarina Rangnitt gives a welcome remark on behalf of Diplomatic Corps at the Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African. Katarina emphasized on the importance of equipping young people with proper education and relevant skills to make them competent.
A cross section of ministers from Eastern Africa, Unesco officials and the SDG4 co- conveners (ILO, UNFPA, UNDP, UNICEF, UN Women, UNHCR and World Bank) listening attentively on various speakers at the ongoing Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African in Dar es Salaam.
Some of the invited dignitaries attending the Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African in Dar es Salaam.
The Minister of State in the President's Office responsible for Regional Administration and Local Government (TAMISEMI), Hon  George Simbachawene and Norwegian Ambassador to Tanzania, Hanne-Marie Kaarstad (right)  follows  the Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African in Dar es Salaam.
Deputy Minister for Education, Science, Technology and Vocational Training Eng. Stella Manyanya exchanging contacts with a disabled teacher Madam Sophia Mbeyela (centre) at the ongoing Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African in Dar es Salaam.
Group Photo.
The Minister for Education, Science, Technology and Vocational Training Prof. Joyce Ndalichako elaborates a point to reporters about the prons and cons of the Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African in Dar es Salaam.
The Minister of State in the President's Office responsible for Regional Administration and Local Government (TAMISEMI), Hon. George Simbachawene making a point during the press conference at the Julius Nyerere International Conference Centre.
 A cross section of Ministers and Journalists.
Zanzibar Minister of Education and Vocational Training Hon.Riziki Pembe shares her experience on how they have prioritized Sustainable Development Goals on Education in the Island.
Minister of Education &Human Resources  Tertiary Education & Scientific Research to the Republic of Mauritius, Leela Dookon Luchoomon gives testimony on her country achievement on education.
Minister of State for Primary Education in Uganda, Hon. Nansubuga Rosemary Seninde explains to reporters what it means to deal with children who do not want to attend schools in a bid to pursue compulsory education for all.
Minister of National Education and Vocational Training in the Republic of Djibouti, Hon. Moustapha Mohamed Mahamoud explaining challenges encounters in the education sector during the press conference.

13 Ministers from Eastern Africa, Unesco and the SDG4 co- conveners (ILO, UNFPA, UNDP, UNICEF, UN Women, UNHCR and World Bank) are in Dar es salaam to identify priorities and policy recommendations for a regional roadmap for the implementation of the SDG4- Education 2030 agenda and linkages with other SDGs;

In two days meeting opened yesterday at Julius Nyerere International Convention Centre (JINCC) various people made different remarks on how to ensure inclusive and equitable quality education and promote lifelong learning opportunities for all.

Opening the floor to welcome all participants including ministers from Comoros, Djibout, Eritrea, Ethiopia, Kenya, Madagascar, Mauritius, Rwanda, Seychelles, Somalia, South Sudan, Tanzania and Uganda, Swedish Ambassador to Tanzania  H.E Katarina Rangnitt spoke about Young people being given proper education with relevant skills to make them competent.

She talked about unlocking the potential of the people by keeping children in school and managing drop out with full knowledge that education is the tool to reach development goals.

“With the growing frustrations among the youth on lack of employment, climate change and disasters she asked participants to come out with practical solutions making sure that nobody is being left behind with a keen attention to kids with disabilities.” She said.

She asked the participants to look at how global SDGs will be achieved in accordance to the national policies targets and plans.

Speaking at the same meeting Mrs Victoria Akyeampong, UNHCR Head Regional Services Center spoke about the need to support people of concern so as to reach the goal as the agenda 2030 spoke about leaving no body behind.

She said refugees and migrants are in dire need of support because of the fragile situation they are. She said less than one percent of those people are enrolled in education. She asked the participants to increase access to refugees through digital education.

She also asked East Africans to look at the best way of including refugees in their national school as is being done in Cameroon Chad and Pakistan.

Unesco Regional Office for Eastern Africa, Director Mrs Ann Therese Ndong-Jatta addressing the forum posed several question to the participants on priorities and what makes good education.

She said the forum was initiated to deal with the missing link by focusing difficult questions which are still puzzling the community.

On education, she asks about the environment, investment and if people are happy with the current education set up. She examined critically what does examinations do to the kids. If it is not only creating competitions and not happiness.

 She wanted the participants to look and come out with the statement what are we supposed to do to have a true education. She said kids and the rest, learning should be joy and not otherwise and teaching should be joy too.

She remembered Mwalimu Nyerere, Tanzania Founding father, for his courage to insist on using local language to teach. She said by using local language as other nation like China and Japanese did we will create confidence to our people and allow mothers to teach their kids.

In her Key note address Hon Prof Joyce The Minister for Education, Science, Technology and Vocational Training, insisted the importance of the platform in transforming the East African society. She said the platform is an important platform and step in the construction of a common vision for the education 2030 agenda.

“This is an important platform and step in the construction of a common vision for the Education 2030 Agenda, and for our countries to share National Road maps, to identify emerging common areas, and to identify common challenges and opportunities", said Ndalichako.

She said Tanzania is ready to engage in achieving the targets of SDG4.
She further added that the successful implementation of the SDG4 like any other programme, depends much on political will and support.

RAIS DKT MAGUFULI MGENI RASMI MAHAFALI YA 31 YA CHUO KIKUU HURIA CHA TANZANIA (OUT)

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.



  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na baadhi ya wahitimu wa  Shahada ya Uzamivu ya Udaktari wa Falsafa  wakati wa mahafali ya 31 ya  Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika kwenye kampasi ya chuo hicho huko huko Bungo, Kibaha,  mkoa wa Pwani leo Novemba 24, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na  baadhi ya wahadhiri wakati wa mahafali ya 31 ya  Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika kwenye kampasi ya chuo hicho huko huko Bungo, Kibaha,  mkoa wa Pwani leo Novemba 24, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akihutubia wakati wa mahafali ya 31 ya  Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika kwenye kampasi ya chuo hicho huko huko Bungo, Kibaha,  mkoa wa Pwani leo Novemba 24, 2016
 Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Profesa, Joyce  Ndalichako  akihutubia wakati wa mahafali ya 31 ya  Chuo Kikuu Huria cha Tanzania yaliyofanyika kwenye kampasi ya chuo hicho huko huko Bungo, Kibaha,  mkoa wa Pwani leo Novemba 24, 2016.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipiga makofi wakati Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Pinda akimtunuku Shahada ya Uzamivu ya Udaktari wa Falsafa mhitimu Hebson Opiyo Andala kutoka Rwanda wakati wa mahafali ya 31 ya chuo hicho yaliyofanyika kwenye kampasi ya OUT huko Bungo, Kibaha,  mkoa wa Pwani leo Novemba 24, 2016
Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Pinda akimtunuku Shahada ya Uzamivu ya Udaktari wa Falsafa mhitimu Philip Filikunjombe wakati wa mahafali ya 31 ya chuo hicho yaliyofanyika kwenye kampasi ya OUT huko Bungo, Kibaha,  mkoa wa Pwani leo Novemba 24, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Profesa, Joyce Ndalichako,    Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Mizengo Pinda,  Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Profesa Samuel Wangwe Makamu Mkuu wa Chuo hicho  Prof. Elifas Bisanda  wakiondoka jukwaa kuu baada ya kuhitimisha mahafali ya 31 ya chuo hicho yaliyofanyika kwenye kampasi ya OUT huko Bungo, Kibaha,  mkoa wa Pwani leo Novemba 24, 2016.

PICHA NA IKULU