HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

WAZIRI SIMBACHAWENE AAGIZA WAHITIMU CHUO CHA SERIKALI ZA MITAA HOMBOLO WAPEWE KIPAUMBELE

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Bw. George Simbachawene akisalimiana na Rais wa Serikali ya Wanachuo Chuo Kiongozi cha Mafunzo ya Serikali za Mitaa (Hombolo), Bw. Kelvin Mbuta hivi karibuni mjini Dodoma. Pembeni ni Kaimu Mkuu wa Chuo hicho, Dkt. Martin Madale.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Bw. George Simbachawene akizungumza na Uongoza na Wawakilishi wa Serikali ya Wanachuo ya Chuo Kiongozi cha Mafunzo ya Serikali za Mitaa (Hombolo)mjini Dodoma hivi karibuni.

Na Mwandishi Wetu, Dodoma
 SERIKALI imeziagiza Halmashauri,Miji na Majiji nchini kutoa kipaumbele cha ajira kwa wahitimu wa chuo  Kiongozi cha Mafunzo ya  Serikali za Mitaa(LGTI) ambao mafunzo wanayopata  yanalenga kuongeza  na  kuleta ufanisi katika serikali za mitaa nchini.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais  Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), George Simbachawene amesema hivi karibuni kuwa  Chuo  Kiongozi cha  Mafunzo ya Serikali za Mitaa (Hombolo) kipo mahusiusi kwa ajiri ya kutoa mafunzo  kwa ajili ya wafanyakazi  wanaoajiliwa kwenye serikali za mitaaa nchini.

“Naagiza kunapokuwa na nafasi za kazi kwenye halmashauri, miji na hata majiji ni vyema wahitimu wa chuo hiki wakapewa kipaumbele. Ni vizuri wakapata nafasi ya kushindanishwa na wengine kwani hawa ni walengwa,”  alisema Waziri Simbachawene  wakati alipokutana na viongozi na wawakilishi wa chuo hicho mjini Dodoma.

Bila kumung’unya maneno, Waziri Simbachawene alisema wahitimu kutoka chuo Kiongozi cha Serikali za Mitaa ndiyo wabobezi kwenye taaluma za serikali za mitaa na hivyo kuwa kwenye nafasi nzuri ya kuleta ufanisi zaidi.

“Ni vizuri tukakumbuka kuwa chuo hiki kilianzishwa na serikali kwa lengo la kuwaandaa wafanyakazi wa kada zote katika serikali za mitaaa,” alisema na kuongeza kuwa serikali itaendelea kukijengea uwezo chuo hicho ili kiweze kutoa wahitimu bora.

Waziri Simbachawene aliuagiza uongozi wa chuo hicho kutosita kutoa taarifa yeyeto endapo chuo kinapokuwa na upungufu wa watumishi.

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Chuo hicho, Dkt. Martin Madale alimshukuru Waziri Simbachawene kwa kuwa karibu na chuo  na pia kufuatilia maendeleo na  ustawi.

“Kwa niaba ya Bodi, Menejimenti, Wafanyakazi na wanachuo wote wana imani kubwa na uongozi wako kwani umekuwa karibu sana nasi na pia umekuwa msaada mkubwa katika utatuzi wa changamoto mbalimbali zinazokikabili chuo,” alisema Dkt. Madale.

Alimwomba waziri kukisaidia chuo  kupata kompyuta zaidi, viti na vifaa mbalimbali ilikukabiliana na ongezeko la idadi ya wanafunzi wanaoomba kujiunga na chuo hicho kwa sasa.

Naye Rais wa Serikali ya wanachuo, Bw. Kelvin Mbuta alimwomba waziri kusaidia kufikisha ombi la wanachuo serikalini kuhusu mikopo kama wanachuo wa vyuo vingine wanavyopata.

“Nipo hapa kwa niaba ya wanachuo ambao wameniagiza kilio chao kuhusu mikopo. Tunakuomba Mheshimiwa waziri utusaidie tupate mikopo kwaajili ya kujikimu kwani kuna wachuo wengi wanetoka kwenye familia maskini sana,” alisema.

Chuo Kiongozi cha Mafunzo ya Serikali za Mitaa maarufu kama Chuo cha Hombolo kina wanachuo zaidi ya 3,000 ambao wapo katika Kampasi Kuu ya Hombolo ambayo ipo pembeni kidogo mwa Mji  wa Dodoma na ile Kampasi ya Mjini.

Chuo kinatoa  programu  sita  za Stashahada (Diplomas)  na program sita za Cheti(Certificates) katika Usimamizi wa Raslimali Watu (Human Resource Management), Serikali za Mitaa na Utawala(Local Government and Administration)Uhasibu na Usimamizi wa Fedha Serikali za Mitaa(Local Government Accounting and Finance),Usimamizi wa Kumbukumbu na Nyaraka(Records and Archive Management),Manunuzi (Procurement)na Maendeleo ya Jamii (Community Development).

Serikali yatoa ajira kwa walimu 3,081

Serikali imesema jumla ya walimu 3,081 wakiwemo walimu 7 wa shule ya Sekondari Omumwani Kagera, wameajiriwa, hivyo bado kuna nafasi ya walimu 1.048 kati ya nafasi 4,129 za walimu wa Sayansi na Hisabati zilizotolewa kibali cha ajira.

Taarifa hiyo imetolewa leo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) George Simbachawene alipokuwa  akizungumza na Waandishi  Habari,ofsini kwake ambapo amewataka walimu wote walioajiriwa wanatakiwa kuripoti katika vituo vyao vya kazi kuanzia tarehe 18 hadi 25 mwezi huu.

Amesema walimu walioajiriwa  wamepangwa moja kwa moja na TAMISEMI katika halmashauri zote nchini ambazo zina upugufu wa walimu wa Sayansi na Hisabati.

Simbachawene amesema kati ya walimu hao walioajairiwa walimu 1,537 ni wa Shahada  na walimu 1,544 ni wa Stashahada.

“Sehemu kubwa ya walimu wa Shahada wamepangwa  kwenye shule za kidato cha tano na sita na wachache kwenye shule za kidato cha kwanza hadi cha nne’’ alisema.

Simbachawene amekiri  kuwa kuna upungufu wa walimu 26,026 wa masomo Sayansi na Hisabati katika shule mbalimbali za sekondari nchini.

“Moja ya changamoto kubwa ambazo zinaikabili sekta ndogo ya elimu ya sekondari ni upungufu wa walimu wa Sayansi na Hisabati upungufu uliopo  katika shule 3,602 ni 26,026 sawa na asilimia 60.14 ya walimu 43,248 wanaohitajika” amesema Simbachawene

Amesema walimu wanaohitajika kwa masomo hayo ni walimu 43,248 lakini waliopo kwa sasa ni 17,252 pekee.

Amesema kwa sasa serikali ina shule za sekondari 3,602 na kati ya hizo shule 333 ni za kidato cha tano na sita huku zingine 54 za kidato cha tano zimeanzishwa .

Aidha amesema shule hizo za sekondari kwa upande wa masomo ya Sanaa ina ziada ya walimu 7,463 ambapo waliopo ni walimu 63,240 na wanaohitajika ni walimu 55,777.

“Kutokana na ziada hiyo ya walimu wa Sanaa serikali imeanza kuchukua hatua yawahamisha walimu hao katika shule za msingi ili kuziba upungufu wa walimu katika shule hizo’’ alisema.

SIMBACHAWENE - WALIMU WALIOHAMISHWA KIUONEVU WALIPWE

SERIKALI imetoa siku 30 kwa halmashauri nchini kuwalipa walimu wote waliohamishwa kwa uonevu na kupiga marufuku tabia ya kuhamisha walimu kwa kukomoana.
Pia walimu wakuu na wakuu wa shule waliokaa muda mrefu vituoni watahamishwa ndani ya miezi mitatu na uhamisho huo utafanywa na Wizara.
Kauli hiyo ilitolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), George Simbachawene wakati akifungua mkutano mkuu wa maofisa elimu wa mikoa na wilaya.
Alisema walimu wote waliohamishwa kwa mtindo wa uonevu, wakuu wa shule wahakikishe wanalipwa fedha zao.
“Unamhamisha mtu bila kuwasiliana na Hazina. Mmekuwa kama kiwanda cha kuzalisha madeni ya serikali, halmashauri zinazalisha sana madeni mtalipa nini, kuhamisha mtu bila utaratibu ni kuongezea serikali madeni,” alisema.
Alisema kumekuwa na tabia ya kukomoana na maofisa elimu wanawake wamekuwa wanahamisha walimu wenzao bila kujali mazingira yake.
“Maofisa elimu wa mikoa hayo yanatokea kwenu msiamue mambo kijeshi watumishi wana haki zao, heshimuni sheria, watoto wa kike ndio wananyanyaswa kupita kiasi wanapelekwa sehemu ambayo wanashindwa kumudu mazingira na kubaki wakifikiria kuacha kazi tu.Ninatoa siku 30 walimu wote waliohamishwa walipwe;” alisema.
Aidha waziri huyo amesema walimu wakuu na wakuu wa shule waliokaa vituo vyao vya kazi muda mrefu watahamishwa.
“Utakuta mwalimu miaka 20 yuko shule moja, hamuoni hayo? Lakini naelewa kuwagusa wengine ni shida na uhamisho huo utafanywa na Wizara, huu ni utumishi wa umma hawana hatimiliki ya kukaa shule moja muda mrefu lazima waondolewe,” alisema.
Waziri Simbachawene alisema serikali imeanza kupunguza walimu wa ziada wa masomo ya sanaa na kupelekwa shule za msingi.
Alisema wameanza na shule za Mkoa wa Arusha ambapo walimu 700 wa sanaa wamepelekwa kufundisha shule za msingi.
“Meru walimu 400 hawana kazi wanakaa bure tutawapeleka shule za msingi ili kukabiliana na upungufu,” alisema.
Pia alisema kumekuwa na upungufu wa madarasa 127,000 nchi nzima na kutaka serikali za mitaa kushirikisha wananchi kuchangia nguvu zao.
Awali, Mwenyekiti wa Umoja wa Maofisa Elimu Mikoa na Wilaya (REDEOA), Mayasa Hashim alisema wataendelea kuwatumikia Watanzania kwa juhudi zao zote.

CHANZO: HABARI LEO

13 COUNTRIES SITS IN DAR TO DISCUSS EDUCATION

Chair of the Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African in Dar es Salaam and Head Office and country Representative of UNESCO, Zulmira Rodrigues welcomes invited guests, dignitaries and key speakers during Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African in Dar es Salaam. (All photos by Zainul Mzige)

The Minister for Education, Science, Technology and Vocational Training Prof Joyce Ndalichako delivering key note address to officiate Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African in Dar es Salaam.
Unesco Regional Office for Eastern Africa, Director Mrs Ann Therese Ndong-Jatta addressing Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African in Dar es Salaam.
UNHCR Head Regional Services Center, Mrs Victoria Akyeampong, gives her statement at the National Forum Session during the Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African in Dar es Salaam.
Linda Madete from UNESCO Office Dar es Salaam gives out some of the education materials and brochures to invited guests during the Ministerial Sustainable Development Goals numbers 4 that focuses on ensuring inclusive and equitable quality education and promote lifelong learning opportunities for all at the Regional Forum for Eastern African in Dar es Salaam.
The Minister for Education, Science, Technology and Vocational Training, Prof Joyce Ndalichako (far left) arrives at Julius Nyerere International Convention Centre (JINCC )to attend the Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African in Dar es Salaam.
Norwegian Ambassador to Tanzania, Hanne-Marie Kaarstad tete-a-tete with the UNHCR Representative to Tanzania, Chansa Ruth Kapaya at the Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African.
Swedish Ambassador to Tanzania H.E Katarina Rangnitt gives a welcome remark on behalf of Diplomatic Corps at the Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African. Katarina emphasized on the importance of equipping young people with proper education and relevant skills to make them competent.
A cross section of ministers from Eastern Africa, Unesco officials and the SDG4 co- conveners (ILO, UNFPA, UNDP, UNICEF, UN Women, UNHCR and World Bank) listening attentively on various speakers at the ongoing Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African in Dar es Salaam.
Some of the invited dignitaries attending the Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African in Dar es Salaam.
The Minister of State in the President's Office responsible for Regional Administration and Local Government (TAMISEMI), Hon  George Simbachawene and Norwegian Ambassador to Tanzania, Hanne-Marie Kaarstad (right)  follows  the Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African in Dar es Salaam.
Deputy Minister for Education, Science, Technology and Vocational Training Eng. Stella Manyanya exchanging contacts with a disabled teacher Madam Sophia Mbeyela (centre) at the ongoing Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African in Dar es Salaam.
Group Photo.
The Minister for Education, Science, Technology and Vocational Training Prof. Joyce Ndalichako elaborates a point to reporters about the prons and cons of the Ministerial SDG4 Regional Forum for Eastern African in Dar es Salaam.
The Minister of State in the President's Office responsible for Regional Administration and Local Government (TAMISEMI), Hon. George Simbachawene making a point during the press conference at the Julius Nyerere International Conference Centre.
 A cross section of Ministers and Journalists.
Zanzibar Minister of Education and Vocational Training Hon.Riziki Pembe shares her experience on how they have prioritized Sustainable Development Goals on Education in the Island.
Minister of Education &Human Resources  Tertiary Education & Scientific Research to the Republic of Mauritius, Leela Dookon Luchoomon gives testimony on her country achievement on education.
Minister of State for Primary Education in Uganda, Hon. Nansubuga Rosemary Seninde explains to reporters what it means to deal with children who do not want to attend schools in a bid to pursue compulsory education for all.
Minister of National Education and Vocational Training in the Republic of Djibouti, Hon. Moustapha Mohamed Mahamoud explaining challenges encounters in the education sector during the press conference.

13 Ministers from Eastern Africa, Unesco and the SDG4 co- conveners (ILO, UNFPA, UNDP, UNICEF, UN Women, UNHCR and World Bank) are in Dar es salaam to identify priorities and policy recommendations for a regional roadmap for the implementation of the SDG4- Education 2030 agenda and linkages with other SDGs;

In two days meeting opened yesterday at Julius Nyerere International Convention Centre (JINCC) various people made different remarks on how to ensure inclusive and equitable quality education and promote lifelong learning opportunities for all.

Opening the floor to welcome all participants including ministers from Comoros, Djibout, Eritrea, Ethiopia, Kenya, Madagascar, Mauritius, Rwanda, Seychelles, Somalia, South Sudan, Tanzania and Uganda, Swedish Ambassador to Tanzania  H.E Katarina Rangnitt spoke about Young people being given proper education with relevant skills to make them competent.

She talked about unlocking the potential of the people by keeping children in school and managing drop out with full knowledge that education is the tool to reach development goals.

“With the growing frustrations among the youth on lack of employment, climate change and disasters she asked participants to come out with practical solutions making sure that nobody is being left behind with a keen attention to kids with disabilities.” She said.

She asked the participants to look at how global SDGs will be achieved in accordance to the national policies targets and plans.

Speaking at the same meeting Mrs Victoria Akyeampong, UNHCR Head Regional Services Center spoke about the need to support people of concern so as to reach the goal as the agenda 2030 spoke about leaving no body behind.

She said refugees and migrants are in dire need of support because of the fragile situation they are. She said less than one percent of those people are enrolled in education. She asked the participants to increase access to refugees through digital education.

She also asked East Africans to look at the best way of including refugees in their national school as is being done in Cameroon Chad and Pakistan.

Unesco Regional Office for Eastern Africa, Director Mrs Ann Therese Ndong-Jatta addressing the forum posed several question to the participants on priorities and what makes good education.

She said the forum was initiated to deal with the missing link by focusing difficult questions which are still puzzling the community.

On education, she asks about the environment, investment and if people are happy with the current education set up. She examined critically what does examinations do to the kids. If it is not only creating competitions and not happiness.

 She wanted the participants to look and come out with the statement what are we supposed to do to have a true education. She said kids and the rest, learning should be joy and not otherwise and teaching should be joy too.

She remembered Mwalimu Nyerere, Tanzania Founding father, for his courage to insist on using local language to teach. She said by using local language as other nation like China and Japanese did we will create confidence to our people and allow mothers to teach their kids.

In her Key note address Hon Prof Joyce The Minister for Education, Science, Technology and Vocational Training, insisted the importance of the platform in transforming the East African society. She said the platform is an important platform and step in the construction of a common vision for the education 2030 agenda.

“This is an important platform and step in the construction of a common vision for the Education 2030 Agenda, and for our countries to share National Road maps, to identify emerging common areas, and to identify common challenges and opportunities", said Ndalichako.

She said Tanzania is ready to engage in achieving the targets of SDG4.
She further added that the successful implementation of the SDG4 like any other programme, depends much on political will and support.

WAKUU WA MIKOA NA WILAYA WAPEWA RUNGU LA KUTUMBUA WATUMISHI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa  George Simbachawene amesema kuwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya wanafanya kazi kwa mujibu wa sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Simbachawene ameyasema hayo leo Bungeni, Mjini Dodoma alipokuwa akijibu swali la  nyongeza la Mbunge wa Jimbo la Chemba Juma Nkamia kuhusu Wakuu wa Wilaya na Mikoa kuwa wababe katika maeneo yao ya kazi.

“Wakuu wa Mikoa na Wilaya wanasimamia maeneo yao kwa mujibu wa sheria na wana haki ya kuwachukulia hatua watumishi ambao hawatekelezi majukumu waliyopewa,” alifafanua Simbachawene.

Aliendelea kwa kusema kuwa, hata kama kuna Wakuu wa Mikoa na Wilaya ambao ni wababe katika maeneo yao ya kazi hauwezi kusema kila Mkuu wa Mkoa au Wilaya aliyechukua hatua dhidi ya mtumishi ambaye hawajibiki katika kazi yake ni mbabe au muonevu.

Aidha, Simbachawene amesema kuwa ni wakati sasa wa watumishi wa Umma kutekeleza wajibu wao na kuacha kufanya kazi kwa mazoea. Kwani hakuna kiongozi ambaye ataweza kumchulia hatua mtumishi ambaye anawajibika na kazi zake kama alivyopangiwa.

Vile vile amesema kuwa, wakuu hao wa Mikoa na Wilaya wamekuwa wakifanya kazi nzuri katika maeneo wanayoyasimamia, kutokana na watumishi wengi wa Serikali walikuwa wamejisahau kutekeleza wajibu wao na kufanya kazi kimazoea.

RAIS DKT. MAGUFULI AFUNGUA RASMI AWAMU YA KWANZA YA MIUNDOMBINU NA UTOAJI HUDUMA YA MABASI YAENDAYO HARAKA (BRT) JIJINI DAR ES SALAAM

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika Makhtar Diop wa kwanza kulia wavivuta kitambaa kuashiria ufunguzi rasmi wa Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya Mabasi yaendayo Haraka katika jiji la Dar es Salaam. Wengine katika picha ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais –TAMISEMI George Simbachawene pamoja na  Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipiga makofi pamoja na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais –TAMISEMI George Simbachawene na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa wakati Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika Makhtar Diop wakwanza (kulia) akivuta utepe kuashiria Ufunguzi rasmi wa Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya Mabasi yaendayo Haraka katika jiji la Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiweka kadi ya Kieletroniki katika Mashine ya UDART ilikuweza kupita kama ishara ya Ufunguzi rasmi wa Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya Mabasi yaendayo Haraka katika jiji la Dar es Salaam. Pembeni yake ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais –TAMISEMI George Simbachawene akimuelekeza jambo katika mashine hizo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika Makhtar Diop pamoja na viongozi wengine wakikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya Mabasi yaendayo Haraka katika jiji la Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipita kwenye mashine hizo mara baada ya uzinduzi wa Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya Mabasi yaendayo Haraka katika jiji la Dar es Salaam.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipunga mkono kwa wanahabari mara baada ya kuzindua utoaji huo wa huduma ya usafiri.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia mara baada ya kuendesha gari la Mwendo Kasi katika kituo Kikuu cha Mabasi yaendayo Haraka (BRT) mara baada ya kufungua rasmi Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya Mabasi yaendayo Haraka katika jiji la Dar es Salaam.
 ais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipungia mkono pamoja na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika Makhtar Diop mara baada ya kutoka kukagua moja ya basi linalotumika katika utoaji huduma ya Usafiri wa Haraka (BRT)
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo pamoja na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika Makhtar Diop wakati Msanii Mrisho Mpoto alipokuwa akitumbuiza.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiongea na na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika Mhe. Makhtar Diop kwenye sherehe za ufunguzi rasmi wa Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya Mabasi yaendayo Haraka katika jiji la Dar es Salaam leo Januari 25, 2017.
Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kanda ya Afrika Mhe. Makhtar Diop akiongea machache kwenye sherehe za ufunguzi rasmi wa Awamu ya Kwanza ya Miundombinu na Utoaji Huduma ya Mabasi yaendayo Haraka katika jiji la Dar es Salaam leo Januari 25, 2017.

PICHA NA IKULU

SIMBACHAWENE AWATAKA WATUMISHI KUFANYA KAZI KWA UADILIFU

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


 Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhandisi Mussa Iyombe akifafanua jambo kuhusu utekelezaji wa maagizo ya Viongozi wa juu na kuwatumikia wananchi kwa kupunguza changamoto zilizo katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, mara baada ya Waziri wa Nchi kushoto kwake George Simbachawene  kutoa hotuba yake kwa Baraza la Wafanyakazi lililofanyika katika Ukumbi wa Hazina ndogo mjini Dodoma.
Waziri wa Nchi George Simbachawene akitoa hotuba kwa Baraza la Wafanyakazi lililofanyika katika Ukumbi wa Hazina ndogo mjini Dodoma.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tamisemi akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wanaounda Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Rais TAMISEMI.

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi), George Simbachawene amewataka watumishi wa umma kuhakikisha wanafanya kazi kwa uadilifu na kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma, sambamba na kujiepusha na vitendo vya rushwa kwenye utekelezaji wa majukumu yao.

Akizungumza katika kikao cha baraza la wafanyakazi wa wizara hiyo kilichofanyika mjini Dodoma, Simbachawene amesema watumishi hao wanatakiwa kuwa na utendaji unaojali matokeo na kuepuka utendaji wa mazoea.

Amesema wanatakiwa kuzingatia nidhamu na utendaji wa Watumishi wa Umma,na watambue maadili ni nguzo muhimu ya kuepuka vitendo vya ubadhilifu na rushwa mahali pa kazi.

Hata hivyo, amesema kwasasa inafanya uchunguzi wa tuhuma za rushwa kwenye ofisi hiyo zinazotokana na uhamisho, upangaji wa walimu na michakato ya teuzi mbalimbali.

Waziri huyo amesema kumekuwa na tuhuma kwa baadhi ya watumishi kujihusisha na vitendo vya rushwa na kwamba watumishi watakaobainika kujihusisha na vitendo hivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
                   
Sambamba na hilo, ametaka kila Idara na kitengo kuhakikisha kuwa zinapunguza matumizi yasiyo ya lazima ili kuelekeza rasilimali fedha katika kutekeleza majukumu ya msingi ambayo yataleta tija kwa Taifa.

Simbachawene amewaambia wafanyakazi hao kuwa serikali itaendelea kuboresha maslahi ya wafanyakazi kwa kadri hali ya uchumi itakavyoruhusu.

Waziri Simbachawene aagiza fedha za TASAF zirejeshwe

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. George Simbachawene ameziagiza Ofisi za Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Majiji, Manispaa, Miji na Wilaya kuhakikisha kuwa fedha zilizotolewa kwa kaya zisizokuwa na sifa katika Mpango wa kunusuru kaya maskini unaofanywa kwa uratibu wa Mfuko wa Maendeleo ya jamii (TASAF) kurejeshwa ili ziweze kuwanufaisha walengwa.

Mhe. Simbachawene pia amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri kuwasimamisha kazi Waratibu wote wa TASAF wilaya ili kufanya uchunguzi wa jinsi walivyojihusisha katika kuvuruga utekelezaji wa Mpango wa kunusuru kaya maskini kwa kuandikisha kaya zisizokuwa na sifa na ametaka wale wote watakaobainika kuhusika katika kutenda makosa mamlaka za kinidhamu kuchukua hatua za kisheria haraka iwezekanavyo.

Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari mjini Dodoma leo, Mhe. Simbachawene amesema usimamizi dhaifu wa mpango wa TASAF katika ngazi za halmashauri hususani Waratibu wa Mpango wa TASAF Wilaya wasiokuwa waaminifu katika kutekeleza majukumu yao imesababisha fedha za Mpango wa TASAF kutumiwa na watu wasiokuwa walengwa.

Waziri Simbachawene pia amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri kuwachukulia hatua watumishi wa ngazi za Kata, Mitaa na Vijiji ambao kwa namna moja au nyingine watabainika kuhusika katika kuvuruga Mpango wa kuzinusuru kaya maskini kuchukuliwa hatua za kinidhamu.

Aidha, Mhe. Simbachawene amewataka Wakuu wa Mikoa kujiridhisha katika mikoa yao ikiwa Wakurugenzi watachukua hatua stahiki dhidi ya watumishi wasiokuwa waaminifu na kuwataka kumpelekea taarifa hiyo ndani ya siku kumi na nne kuanzia leo tarehe 25/11/2016.

Mheshimiwa Simbachawene ameitaja mikoa inayoongoza kwa matumizi mabaya ya fedha za Mpango wa kunusuru kaya maskini unaotekelezwa na TASAF kuwa ni Dar es Salaam, Kilimanjaro, Morogoro, , Shinyanga, Arusha, Kigoma, Dodoma, Arusha na Mbeya.