HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

Wema Sepetu atoa jibu juu ya shepu yake

Ikiwa ni wiki imepita tangu malkia wa filamu Bongo Wema Sepetu, kuposti picha kadhaa katika mtandao wa kijamii wa Instagram kuonesha umbo lake, mwana dada huyo ameamua kuwajibu wale wanaodhania shepu hiyo sio yake.

Wema ambaye kwa sasa hataki kujihusisha na skendo yoyote ameandika “Shepu ya mwendokasi… Ndo niliojaliwa nayo… Kama imeanzia kiunoni kwenda magotini ndo niliojaliwa nayo… Kama wewe hauna basi mshukuru Allah… Ndo nilivyoumbwa jamani… Sio mimi bali ni Maulana ndo alionibariki nayo… Hata ingekuwa kwanzia kichwa hadi Vidole vya miguuni ni sawa pia… Ndo niliojaliwa nayo.”
“Sometimes najiangalia kwenye kioo sijimalizi… Ndo majaliwa yangu… Ndo yangu basi… Imenizidia… Allah Subhanah wataallah ndo amenipa… Aaaah….!? Sio shepu ya kawaida… Niacheni na Shepu yangu jamani… Ndo nishaimiliki mie… Siwezi kuitoa…. 🙄🙄🙄🙄,” ameandika mrembo huyo.

Ushahidi kesi ya Wema Sepetu wakwama kutolewa

Kesi ya kukutwa na dawa za kulevya inayomkabili Wema Sepetu katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imeahirishwa hadi Julai 10.
Wema ambaye ni mshindi wa taji la urembo, maarufu Miss Tanzania kwa mwaka 2006 na msanii wa filamu, anakabiliwa na kesi hiyo akidaiwa kutumia na kupatikana na bangi.
Wakili wa Serikali, Elizabeth Mkunde mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa alisema kesi ilipangwa leo (Jumatano) kuanza kusikiliza ushahidi wa upande wa mashtaka lakini Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba anayeisikiliza kesi hiyo yupo likizo.
Kutokana na hilo, aliomba iahirishwe hadi Julai 10 ombi lililokubaliwa na mahakama.
Wema na wenzake Angelina Msigwa na Matrida Abbas wanakabiliwa na mashtaka mawili ya kukutwa na dawa za kulevya na kutumia dawa hizo.
Inadaiwa Februari 4, katika makazi ya Wema, Kunduchi Ununio, walikamatwa wakiwa na msokoto mmoja na vipisi vya bangi vyenye uzito wa gramu 1.08.
Wema pia anadaiwa Februari Mosi katika eneo lisilojulikana jijini Dar es Salaam alitumia bangi.

Mbowe afunguka kuhusu yeye na Wema Sepetu

Wema na Mbowe

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe amesema clip ya sauti inayosambaa kwenye mitandao inayomuhusisha yeye na Wema Sepetu si ya kwake na hajawahi kuwa na mahusiano ya kimapenzi na Mrembo huyo.
Kiongozi huyo amekiambia kipindi cha XXL cha Clouds FM, kuwa yeye anachukulia clip hiyo kama taarifa za kawaida za majitaka ambazo zinasambazwa wala hazina ukweli wowote.
“Kitu ambacho naweza kukisema kwa sasa hizo taarifa sio za kweli na timu yangu ya mtandao inajaribu kufuatilia kujua, na ukweli utajulikana muda sio mrefu,” amesema Mbowe.
Alipoulizwa kama anawajua waliofanya kitendo hicho, Mbowe amesema akizungumza sasa atakuwa anaharibu uchunguzi wao.
Pia ameongeza kuwa hajawahi kuwa katika mahusiano ya kimapenzi na Wema Sepetu kama inavyosikika kwenye clip hiyo ya sauti.
“Hapana yule ni kiongozi wa kijamii kwa maana kwamba ni mwanachama wetu aliyejiunga na chama chetu, na wapo wanawake, wasichana, wapo watu wengi kwenye chama chetu ni kwamba kuna mahusiano si kweli ni taarifa tu za upotoshaji,” ameleza Mbowe.

Sakata la Roma: Wema Sepetu na Ray watofautiana mitazamo

Baada ya wasanii Roma Mkatoliki, Moni pamoja na wenzao kuchukuliwa na watu wasiofahamika tangu usiku wa kuamkia juzi  wasanii mbalimbali wamekuwa wakitumia kurasa zao za mitandao ya kijamii kupost juu ya kusikitshwa na kitendo hicho, Wema Sepetu akiwa moja kati yao.

Lakini post ya Wema Sepetu ambayo aliiandika kupitia ukurasa wake wa Instagram imeonesha kutokumfurahisha muigizaji mwenzake Ray Kigosi ambaye amepost pia katika ukurasa wake wa instagram na kueleza kutokufurahishwa na namna Wema alivyoandika kuhusu ishu hiyo.

==> Wema Sepetu aliandika hivi;
"This Is Scary… Ni Janga kubwa sana kwa wasanii, kwa wananchi na Kwa Taifa letu kiujumla… Kinachonishangaza ni kuona baadhi ya wasanii wa Bongo movie wamekazana kupost eti wapo kwa Mkuu wa mkoa wakiongelea WaKorea na Waphilipino…. Mlikumbuka kumuuliza Mheshimiwa alipo Roma na Moni…??? Au ndo mambo ya kila mtu anaangalia lake…. 

"Au labda mpaka atekwe msanii wa Bongo movie pia ndo akili itatukaa sawa…??? Oh God help Us Please… Lakini pia wala sitoshangaa hata kama akitekwa msanii wa bongo movie hakuna atakaehangaika within Us zaidi ya wananchi peke yao na watu wetu wa karibu… Tumejawa sana Unafki…!!! All in All namuonea sana huruma Nancy…. 

"Our prayers are with u mama… Inshallah mumeo atapatikana… Tuzidi kumuomba Mungu…..🙏🏼🙏🏼🙏🏼…. Kabla sijasahau, Tuwage tuna hata fikra za kujua tupo kwenye wakati gani na tupost vitu gani….!!! Yaani mtu kapotea siku ya pili mko busy na kupost Wakorea na Waphilipino…?? 🙄🙄🙄 SMH.. "
This Is Scary... Ni Janga kubwa sana kwa wasanii, kwa wananchi na Kwa Taifa letu kiujumla... Kinachonishangaza ni kuona baadhi ya wasanii wa Bongo movie wamekazana kupost eti wapo kwa Mkuu wa mkoa wakiongelea WaKorea na Waphilipino.... Mlikumbuka kumuuliza Mheshimiwa alipo Roma na Moni...??? Au ndo mambo ya kila mtu anaangalia lake.... Au labda mpaka atekwe msanii wa Bongo movie pia ndo akili itatukaa sawa...??? Oh God help Us Please... Lakini pia wala sitoshangaa hata kama akitekwa msanii wa bongo movie hakuna atakaehangaika within Us zaidi ya wananchi peke yao na watu wetu wa karibu... Tumejawa sana Unafki...!!! All in All namuonea sana huruma Nancy.... Our prayers are with u mama... Inshallah mumeo atapatikana... Tuzidi kumuomba Mungu.....🙏🏼🙏🏼🙏🏼.... Kabla sijasahau, Tuwage tuna hata fikra za kujua tupo kwenye wakati gani na tupost vitu gani....!!! Yaani mtu kapotea siku ya pili mko busy na kupost Wakorea na Waphilipino...?? 🙄🙄🙄 SMH...
A post shared by Wema Sepetu (@wemasepetu) on


==>Ray Kigosi  hakuipenda post hii, hivyo akajibu;
NAFIKIRI NI VEMA MTU KUELEZA HISIA ZAKE JAPO SIO BUSARA KWA MWENYE HISIA HIZO KUZIELEZA BILA WEREDI NAWASIHI WASANII WENZANGU KUPOTEA KWA ROMA ISIWE SABUNI YA KUTAKATISHA UCHAFU WA MTU SOTE TUMESIKITISHWA NA JAMBO HILO NA TUMEONYESHA KWA VITENDO. MIMI NIMEPOST INSHU YA ROMA TANGU JANA USIKU WEMA SEPETU WEWE ULIKUWA HUJAPOST CHOCHOTE TUSEME ULIKUWA HUNA UCHUNGU? ALAFU LEO UNAANDIKA KUWA BONGO MOVIE HAWAPO PAMOJA NA TUKIO LA ROMA HUKU NI KUTUGOMBANISHA NA WANANCHI WANAOTUAMINI. SISI BONGO MOVIE MARA NYINGI SANA TUNAKUWA PAMOJA KWENYE MATUKIO YA BONGE FLEVA TOFAUTI NA WAO. KAMA UNA UGONVI NA MTU HAYO NI MAMBO YAKO BINAFSI ILA USITUFANYE SISI TUONEKANA WABAYA MBELE YA JAMII UTAKUWA KICHAA KAMA USIPOPATA MAUMIVU KWA TUKIO LA ROMA NIMESIKITISHWA SANA POST YAKO @wemasepetu KAMA UNADHANI HUU NI MUDA MUAFAKA WA KUTAFUTIA POINT KATIKA TUKIO LA ROMA MKATOLIKI UMEFELI HILI NI JANGA LETU SOTE. @wemasepetu #(KINA ROMA WAKO WAPI?).

WEMA SEPETU AMJIBU HARMORAPA BAADA YA KUTAKA MAHUSIANO NAYE

Harmorapa na Wema Sepetu

Wema amecharuka katika mtandao wake wa instagram leo ikiwa ni siku chache zimepita tangu msanii huyo anayetamba na ngoma ya 'Kiboko ya mabishoo' kutangaza kuwa anampenda msanii huyo na kwamba anaumizwa na jinsi watu wanavyomuumiza kimapenzi.
Aidha mwanadada huyo amemtaka msanii huyo kupigana jinsi atakavyoweza kulifikisha jina na muziki wake juu pasipo kumtumia yeye kama njia na kuongeza ni kumvunjia heshima mbele ya familia, chama, marafiki pamoja na mpenzi aliyenaye.
"Sijawahi kumchukia yeyote anayehangaika kutafuta riziki yake kwa kuwa nami pia natafuta. Ila mdogo wangu Harmorappa u are getting too much. Pigana na namna utakavyo kupeleka muziki na jina lako juu but get me out of this. Nakuheshimu kama msanii mwenzangu lakini hili la kunadi kunitaka kimapenzi na kuonyesha utayari wa kufanya mambo kadha wa kadhaa kwangu please waambie wengine unaodhani mnawezana ila mimi siyo wa aina hiyo". aliandika Wema.
Katika kuonesha kuwa muigizaji huyo amekerwa na kauli ya Harmorapa, ameongeza kwamba "Do u think na mimi ni wa aina hiyo? Usinidharaulishe.... Nadhani kuna busara ya wewe to look for another one butan not for you and i hope utanipa heshima yangu kama dadaako, msanii mwenzako lets stop there"

LEMA: ASEMA MADIWANI WA CHADEMA WAOGA YUPO TAYARI KUWAKANA MBELE YA WANANCHI

Mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika shule katika viwanja vya Ngarenaro Jijini Arusha.
Wapili kutoka kushoto ni mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema ,wakwanza kulia ni mbunge wa Simanjiro James OLemilya akifuatiwa na aliyeko kulia kwake ni Meya wa jiji la Arusha Kalisti Lazaro, akifuatiwa na Wema Sepetu,na wakwanza kulia ni mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Arusha Derick Magoma
Wema Sepetu akisaliamia wananchi wa jiji la Arusha waliofika kwenye mkutano huo
Mamia ya wananchi waliohudhuria katika mkutano huo leo jijini Arusha.

Na,Vero Ignatus ,Arusha.
Mbunge wa Arusha mjini Godbless Jonathan Lema amefanya mkutano wake wa kwanza kwa kuzungumza na wananchi wa Arusha baada ya kutoika rumande alipokuwa ameshikiliwa kwa miezi minne

Akizungumza katika mkutano huo Lema amesema kuwa madiwani wa chama cha Demokrasia na maendeleo Chadema watakao kuwa waoga yupo tayari kuwakana mbele ya wananchi na kama hawawezi kuwa majasiri waachanae na chama hicho. 

Mkutano huo umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama hicho wakiwemo madiwani wote wa chama hicho katika jiji la Arusha pamoja na wabunge wa simanjiro na yule wa Monduli.

Aidha mbunge huyo amesema kuwa yupo kwenye harakati za kukamisha kukiandika kitabu chake kitakachotoka hivi karibuni chenye historia ya maisha halisi ya wafungwa waliopo gerezani bila hatia,sambamba na wale waliobambikiziwa kesi mbalimbali.

Ameataka madiwani kuwa sambamba na yeye na kuachana na kauli wanayoisema ya kuwa wapo nyuma yake kwa kila kitu anachokifanya .

WEMA SEPETU ATEMBELEA GODBLESS LEMA BAADA YA KUTOKA GEREZANI

Msanii wa filamu nchini Wema Sepetu ambaye hivi sasa amehamia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ametimiza hadi yake kwenda kuonana na Mbunge wa Arusha mjini Mhe. Godbless Lema ambaye amepata dhamani siku ya Ijumaa na kutoka gerezani.

Wema Sepetu juzi alisema atakwenda Arusha kuonana na Mbunge huyo ambaye amekaa ndani kwa zaidi ya miezi mitatu na kusema ni faraja kwao saizi kuona ametoka na kuja kuendeleza mapambano

"Ni faraja kwetu kwamba sasa umerudi mtaani kuendeleza mapambano, kwenye mapambano haya hautakuwa mwenyewe, mdogo wako Wema nitakuunga mkono mpaka kieleweke. For that sake, kesho (jana) i'll be in Arusha kuonyesha Solidarity" alisema Wema Sepetu

Baada ya Wema Sepetu kufanikiwa kuonana na Mbunge wa Arusha Gobless Lema amefunguka na kusema saizi anajisikia furaha na amani kuwa ndani ya chama hicho
"Finally Met my brother, aisee Chadema inanipa furaha mimi. Nina amani ya moyo... Ona Venye nacheka .... It was A Good Day...." aliandika Wema Sepetu

Wema Sepetu aonya watu kumpangia maisha

Nani tena anamchokoza madam Sepenga? Mrembo huyo ameamua kuwaka kwenye mtandao wa Instagram kwa watu wanaofuatilia maisha yake.

Kupitia mtandao huo, Wema ameandika:
Naomba nitoe tamko… Nakipenda Ki-choker changu saaana… And wearing it doesnt make me any less a muslim… Maana mshaanza…! My Daddy Sepetu was A Roman Catholic FYI…!!!🙄🙄🙄 Wote tunamwamini Mungu… So if u cant accept it, Deal with it…! Kupangiwa maisha mnanijua SIPENDI….