HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

MWALIMU AFARIKI KATIKA MKUTANO WA CHAMA CHAO CHA CWT JIJINI DAR ES SALAAM

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


 Mwalimu Tuhobwike Mwinuka Mwakatumbula enzi za uhai wake.
 Jeneza lenye mwili wa mwalimu Tuhobwike Mwinuka Mwakatumbula likiwa ndani ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Wazo Hili Dar es Salaam leo asubuhi wakati wa ibada ya kuuaga mwili huo.
Binamu wa marehemu, Nobert Nselu (kulia) akimsaidia rafiki wa karibu wa marehemu mama Malugu wakati mwili wa marehemu ukiwasili nyumbani kwake.
 Rafiki wa marehemu mama Malugu (katikati) akisaidiwa.
 Waombolezaji wakiwa msibani nyumbani kwa marehemu 
Wazo Hill.

 Ni huzuni kubwa 
 Wakina mama wakiwa na maua wakati wakisubiri mwili wa marehemu kuingizwa ndani.
 Geneza lenye mwili wa marehemu likiingizwa nyumbani kwake. 
 Mtoto mkubwa wa marehemu Nico Mwakatumbula (katikati), akisaidiwa baada ya kutoa heshima za mwisho kwa mama yake.
 Waombolezaji wakiingiza jeneza lenye mwili wa marehemu katika Kanisa la KKKT Usharika wa Wazo Hill.
 Mwili ukiwa kanisani.
 Mume wa marehemu akiwa na watoto wake. Kutoka kulia ni Gloria, Kelvin na Nico.
 Wanafamilia wakiwa katika ibada hiyo ya kumuaga mpendwa wao.
 Waumini wa kanisa hilo wakiwa kwenye ibada hiyo.N a Dotto Mwaibale

MWALIMU Tuhobwike Mwinuka Mwakatumbula wa Shule ya Msingi Kumbukumbu katika Manispaa ya Kinondoni amefariki dunia wakati akiwa katika mkutano wa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) na viongozi wa Idara ya Elimu wa manispaa hiyo.

Kifo cha mwalimu huyo kimetokea Desemba 1, 2016 Siku ya Ijumaa majira ya jioni wakati viongozi hao walipokuwa wakimalizia ziara yao ya kutembelea shule mbalimbali katika manispaa hiyo.

Akizungumza na Jambo Leo mume wa marehemu Samuel Mwakatumbula alisema mke wake hakuwa na tatitizo lolote la kiafya na siku ya tukio hilo aliamka salama na kumuaga kuwa anawahi kwenye mkutano huo.

"Siku chache kabla ya kifo chake mke wangu aliniambia alikuwa hajisikii vizuri kwani alikuwa na uchovu wa kawaida" alisema Mwakatumbula.

Mwakatumbula alisema alipigiwa siku na kuambiwa kuwa mke wake alianguka ghafla wakati mkutano ukiendelea na kupoteza fahamu ambapo alikimbizwa Hospitali ya Mount Mkombozi iliyopo maeneo ya Morocco ambapo waliambiwa tayari alikuwa amefariki.

Mwili wa marehemu ulisafirishwa jana kwenda Kiwira wilayani Rungwe mkoani Mbeya kwa maziko yatakayofanyika leo marehemu ameacha mume na watoto watatu, Nico, Kelvin na Gloria.

YALIYOJIRI KATIKA MAZISHI YA MZEE ABOUD JUMBE MWINYI ZANZIBAR LEO

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


 Jeneza lililobeba mwili wa Marehemu Aboud Jumbe likiwasili nyumbani kwa marehemu Migombani, Zanzibar
 Watoto, Ndugu, jamaa na Viongozi mbali mbali wakipokea mwili wa Marehemu Mzee Aboud Jumbe mara baada ya kuwasili nyumbani kwake Migombani ,Zanzibar.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akishiriki dua maalum mbele ya jeneza lenye mwili wa marehemu Mzee Aboud Jumbe Mwinyi ambaye alikuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano na Rais wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar  ,nyumbani kwa marehemu Migombani Zanzibar.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (katikati)akishiriki dua maalum kwenye msiba wa Mzee Aboud Jumbe nyumbani kwa marehemu Migombani , Zanzibar wengine pichani ni Mke wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mama Mwanamema Shein (kushoto) kulia ni mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa.
Viongozi wa kitaifa wakishiriki katika sala ya kumwombea Ras wa Awamu ya Pili wa Zanzibar, marehemu Alhaj Abood Jumbe iliyofanyika kwenye msikiti, Mwembeshauri Zanzibar Agosti 15, 2016. Kutoka kushoto ni Makamu wa Rais, Mstaafu, Dkt. Mohammed Bilal, Rais Mstaafu wa Zanzibar, Aman Karume, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohammed Shein.
Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza lenye mwili wa Rais wa Awamu ya Pili wa Zanzibar, Alhaj Abood Jumbe katika mazishi yaliyofanyika nyumbani kwa marehemu, Migombani Zanzibar Agosti 15, 2016.
Rais wa Zanzibar, Dkt. Ali Mohammed Shein, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Rais Mstaafu wa Zanzibar, Aman Karume, Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi na Makamu wa Rais Mstaafu, Dkt. Mohammed Ghalib Bilai wakiwa katika mazishi ya Rais wa Awamu ya Pili wa Zanzibar, Alhaj Abood Jumbe yaliyofanyika nyumbani kwa marehemu Migombani, Zanzibar Agosti 15, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiweka udongo kwenye kaburi la Rais wa Awamu ya Pili wa Zanzibar Alhaj Abood Jumbe katika mazishi yaliyofanyika nyumbani kwa Marehemu Migombani Zanzibar, Agosti 15, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Makamu wa Rais Mstaafu, Dkt. Mohammed Ghalib Bilal baada ya mazishi ya Rais wa Awamu ya Pili wa Zanzibar, Alhaj Abood Jumbe yaliyofanyika nyumbani kwa marehemu, Migombani Zanzibar Agosti 15, 2016.