HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

TANZANIA AND U.S. MOVE TO FINALISE MAJOR INVESTMENT AGREEMENTS




Her Excellency Dr. Samia Suluhu Hassan, President of the United Republic of Tanzania, today held talks with the Acting United States Ambassador to Tanzania, Andrew Lentz, at Chamwino State House to advance key areas of bilateral cooperation and reaffirm the shared commitment to a modern, mutually beneficial partnership.

Ambassador Lentz—accompanied by the Counselor for Political and Economic Affairs—underscored Washington’s determination to reset the relationship and deepen economic, political, and security collaboration with Tanzania.

“The United States is committed to a partnership based not on aid dependency but on shared prosperity,” Ambassador Lentz said.

The discussions centred on ongoing negotiations involving major U.S.-linked strategic investments. Both sides acknowledged that talks on two flagship projects—the LNG Project and Tembo Nickel Project—are now in their final stages, pending formal signing. A third investment, the Mahenge Graphite Project, remains under active technical review.

President Samia welcomed Washington’s renewed commitment and assured the delegation that Tanzania remains focused on completing the remaining procedural steps.

“As a non-aligned nation, Tanzania is open, ready, and committed to working with all partners who respect our sovereignty and share our vision for prosperity,” the President said.

“These strategic projects are of national importance, and we are determined to finalise them so they can unlock jobs, investment, and sustainable prosperity for our people.”

The President highlighted that more than 400 American companies currently operate in Tanzania—reflecting the country’s stability, openness to investment, and strong historical ties with the United States.

Beyond investments, the meeting touched on broader areas of cooperation, including political stability, regional security, economic reforms, private-sector growth, health-sector partnerships, and people-to-people exchanges.

Ambassador Lentz congratulated President Samia for her vision and long-term national planning through Vision 2050, noting the U.S. Government’s readiness to support its implementation and reinforce the President’s 4R philosophy of reconciliation, resilience, reforms, and rebuilding trust.

Both sides agreed that strengthened communication, consistent engagement, and timely action on pending agreements are key to unlocking the full potential of U.S.–Tanzania relations.

This meeting marks a pivotal moment in redefining and revitalising the U.S.–Tanzania relationship. The reaffirmed commitment from both governments signals the emergence of a modern, transparent, private-sector-driven partnership rooted in shared prosperity, mutual respect, and long-term strategic cooperation.

Flagship Projects

1. LNG Project — Estimated Value: USD 42 Billion

A transformative natural gas development involving leading international energy companies. The project aims to unlock Tanzania’s vast offshore gas reserves, boost national revenue, create thousands of jobs, and position the country as a major global LNG supplier.

2. Tembo Nickel Project — Value: USD 942 Million

A major critical-minerals investment in Ngara focused on nickel—an essential component in electric-vehicle batteries. The project will support global clean-energy supply chains, stimulate industrialisation, and expand Tanzania’s export base.

3. Mahenge Graphite Project — Value: USD 300 Million

One of the world’s largest high-grade graphite deposits, positioned to serve the fast-growing battery and renewable-energy sectors. The project will reinforce Tanzania’s role as a leading supplier of battery-grade minerals

TANZANIA NA MAREKANI ZASONGA MBELE KUKAMILISHA MAKUBALIANO MAKUBWA YA UWEKEZAJI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekutana na kuzungumza na Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Mhe. Andrew Lentz, Ikulu Chamwino, mkoani Dodoma, tarehe 08 Desemba, 2025. Pamoja na mambo mengine walijadiliana kuhusu ushirikiano wa kiuchumi, siasa, kijamii pamoja na miradi mbalimbali ya maendeleo baina ya Tanzania na Marekani.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Mhe. Andrew Lentz, Ikulu Chamwino, mkoani Dodoma, tarehe 08 Desemba, 2025.

Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, leo amefanya mazungumzo na Kaimu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Andrew Lentz, katika Ikulu ya Chamwino, kujadili maeneo muhimu ya ushirikiano na kuimarisha dhamira ya pamoja ya kujenga ushirikiano wa kisasa na wenye manufaa kwa pande zote mbili.


Balozi Lentz aliyefuatana na Mshauri wa Masuala ya Kisiasa na Uchumi—amesisitiza dhamira ya Washington kuhuisha mahusiano na kuongeza kina la ushirikiano wa kiuchumi, kisiasa na kiusalama kati ya mataifa haya mawili.

“Marekani imejitolea kujenga ushirikiano usiotegemea misaada, bali unaojengwa juu ya ustawi wa pamoja,” alisema Balozi Lentz.

Mazungumzo yamejikita katika hatua za majadiliano ya miradi mikubwa inayoongozwa na kampuni za Marekani. Pande zote mbili zimekubaliana kuwa majadiliano ya miradi miwili ya kimkakati—Mradi wa LNG na Mradi wa Tembo Nickel yamefikia hatua za mwisho kabla ya kutiwa saini rasmi. Uwekezaji wa tatu, Mradi wa Mahenge Graphite, unaendelea kufanyiwa uchambuzi wa kiufundi.

Rais Samia ameukaribisha upya msimamo wa Marekani na kuhakikishia ujumbe huo kuwa Tanzania itaendelea kusimamia hatua zote zilizobaki ili kukamilisha taratibu na kufungua njia ya utekelezaji wa miradi hiyo.

“Kama taifa lisilofungamana na upande wowote, Tanzania iko wazi, tayari na imejitoa kufanya kazi na washirika wote wanaoheshimu uhuru wetu na kushiriki katika dira yetu ya maendeleo,” alisema Rais.
“Miradi hii ni ya umuhimu mkubwa kwa taifa, na tumejidhatiti kuikamilisha ili iweze kufungua ajira, uwekezaji, na ustawi endelevu kwa wananchi wetu.”

Rais pia alibainisha kuwa zaidi ya kampuni 400 za Marekani kwa sasa zinafanya shughuli zao nchini Tanzania kiashiria cha uthabiti wa nchi, mazingira mazuri ya uwekezaji na historia ya muda mrefu ya ushirikiano wa kiuchumi kati ya mataifa haya mawili.

Mbali na uwekezaji, mazungumzo yamegusa maeneo mapana ya ushirikiano ikiwemo utulivu wa kisiasa, usalama wa kikanda, mageuzi ya kiuchumi, ukuaji wa sekta binafsi, ushirikiano katika afya na programu za kubadilishana uzoefu kati ya wananchi wa nchi hizi mbili.

Balozi Lentz amempongeza Rais Samia kwa maono na mipango madhubuti ya muda mrefu kupitia Vision 2050, na kusisitiza kuwa Serikali ya Marekani iko tayari kuunga mkono utekelezaji wake pamoja na kuimarisha falsafa ya 4R ya Rais maridhiano, ustahimilivu, mageuzi na kujenga upya imani katika utawala.

Pande zote zimekubaliana kuwa mawasiliano ya karibu, ushirikiano wa mara kwa mara, na hatua za haraka katika kukamilisha makubaliano yaliyosalia ni muhimu katika kufungua uwezo kamili wa uhusiano kati ya Tanzania na Marekani.

Kikao hiki kinawakilisha hatua muhimu katika kufafanua upya na kuhuisha mahusiano kati ya Tanzania na Marekani. Dhamira ya pamoja iliyothibitishwa na serikali zote mbili inaashiria mwanzo wa ushirikiano wa kisasa, wazi, unaoongozwa na sekta binafsi ukijengwa juu ya ustawi wa pamoja, kuheshimiana na ushirikiano wa muda mrefu wa kimkakati.

Miradi Mikuu ya Kimkakati
1. Mradi wa LNG — Thamani Inayokadiriwa: Dola Bilioni 42
Mradi mkubwa wa kugundua na kuchakata gesi asilia unaohusisha kampuni kubwa za kimataifa za nishati. Mradi huu unalenga kufungua hazina kubwa ya gesi iliyopo baharini, kuongeza mapato ya taifa, kuunda maelfu ya ajira na kuiweka Tanzania katika ramani ya dunia kama mchezaji muhimu wa LNG.

2. Mradi wa Tembo Nickel — Thamani: Dola Milioni 942
Uwekezaji mkubwa wa madini muhimu eneo la Ngara unaolenga nikeli—kiungo muhimu katika utengenezaji wa betri za magari yanayotumia umeme. Mradi huu utaimarisha minyororo ya kimataifa ya nishati safi, kuchochea viwanda na kuongeza pato la mauzo ya nje.

3. Mradi wa Mahenge Graphite — Thamani: Dola Milioni 300
Chanzo kikubwa duniani cha madini ya graphite yenye ubora wa juu, yenye umuhimu katika uzalishaji wa betri na teknolojia za nishati jadidifu. Mradi huu utaimarisha nafasi ya Tanzania kama mtoa huduma mkuu wa malighafi muhimu za viwanda vya kisasa vya betri.

TBN YATOA UFAFANUZI KUHUSU TAARIFA ZA UZUSHI ZINAZOSAMBAZWA MITANDAONI KUHUSU MKUTANO ULIOFANYIKA IKULU



* Mtandao wa Wanablogu Tanzania (TBN) Unatoa Ufafanuzi Kuhusu Mkutano wa Ikulu

 Mtandao wa Wanablogu Tanzania (TBN) unapenda kutoa ufafanuzi rasmi na kuweka mambo wazi kufuatia taarifa zisizo sahihi na zinazoleta utata zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu mkutano uliofanyika hivi karibuni Ikulu.

TBN inakanusha vikali madai yanayosambazwa na baadhi ya watu wanaojiita wanaharakati, wakidai—bila uthibitisho wowote—kuwa wanahabari wa maudhui ya mtandaoni waliitwa Ikulu jijini Dar es Salaam kwa lengo la “kupewa maelekezo” kuhusu maandamano yanayodaiwa kupangwa kufanyika tarehe 9 Desemba.

Kusudi Halisi la Mkutano

TBN inathibitisha kuwa madai haya si sahihi na yamekuwa yakipotoshwa.

Kusudi la kweli na la moja kwa moja la wito wa Ikulu lilikuwa hili: Mkurugenzi mpya wa Mawasiliano Ikulu, Bw. Bakari Machumu, alifanya mkutano wa utambulisho rasmi na wadau muhimu wa sekta ya habari, akianza na wanahabari wa maudhui ya mtandaoni.

Mkutano huu ulikuwa ni hatua muhimu ya kuweka msingi wa ushirikiano na mawasiliano bora. Hakukuwa na ajenda iliyofichwa, wala mchezo wa nyuma ya pazia. Taarifa zozote zinazozungushwa kinyume na ukweli huu zinapaswa kuchukuliwa kama za uzushi na zisizo na msingi.

Wito wa Utulivu na Maadili

TBN inasikitishwa na kitendo cha kusambazwa kwa kipande kifupi cha video cha mkutano huo na baadhi ya watu, ikiwemo wanasiasa, kwa nia ya kujenga utata na kashfa kutoka kwenye kikao cha kawaida cha kiutendaji.

Tunasisitiza umuhimu wa kukuza utamaduni wa majadiliano ya kitaifa yenye staha na ukweli. Vitendo vya kubuni uongo na kupotosha taarifa vinadhoofisha tasnia ya habari na jitihada za kujenga uelewa katika jamii.

TBN inatoa pongezi kwa Bw. Machumu kwa kuonyesha nia ya kushirikiana na wadau wote wa habari. Tunamsihi aendelee na utendaji wake, huku tukiamini kuwa uwazi na utulivu ndio silaha bora dhidi ya upotoshaji.

Tunawaomba wananchi na wadau wote kutanguliza hekima, ukweli, na uzalendo na kukataa taarifa zozote zinazoweza kuleta mgawanyiko au kuchochea taharuki nchini.

Ecobank yasherehekea miaka 40 kwa kampeni ya “Gutuka na Ecobank”



Meneja Mwandamizi wa Kitengo cha Wateja Binafsi Ecobank Tanzania, Innocent Urio (wa pili kulia) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kampeni maalum ya “Gutuka na Ecobank”  inayolenga kuhamasisha Watanzania kuthamini utamaduni wa kuweka akiba.
Mkuu wa Kitengo cha Wafanyabiashara Wadogo na Wakati (SME) Ecobank Tanzania, Juma Hamisi (katikati) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kampeni maalum ya “Gutuka na Ecobank” ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 40 ya huduma zake barani Afrika na miaka 15 tangu kuanza kwa huduma zake hapa nchini Tanzania.
Mkuu wa kitengo cha masoko na mawasiliano Ecobank Tanzania, Furaha Samalu (kulia) akizungumza jambo wakati wa uzinduzi wa kampeni maalum ya “Gutuka na Ecobank” ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 40 ya huduma zake barani Afrika na miaka 15 tangu kuanza kwa huduma zake hapa nchini Tanzania.
Mchekeshaji maarufu nchini Tanzania Maxwell Machange "Mzee Shayo" (wa kwanza kushoto) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu namna alivyojipanga kuifikisha kampeni kwa wananchi wakati wa uzinduzi wa wa kampeni maalum ya “Gutuka na Ecobank”
Mkutano ukiendelea 

Ecobank Tanzania imezindua kampeni maalum ya “Gutuka na Ecobank” ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 40 ya huduma zake barani Afrika na miaka 15 tangu kuanza kwa huduma zake hapa nchini Tanzania.

Uzinduzi wa kampeni hiyo umefanyika Septemba 10, 2025 na itadumu kwa miezi mitatu, ambapo wateja watakaoweka akiba kupitia akaunti ya Supa Seva watapata nafasi ya kushinda zawadi mbalimbali ikiwemo pikipiki za miguu mitatu (Gutas) na pesa taslimu  hadi shilingi milioni moja. 

Akizungumza na waandishi wa habari, Meneja Mwandamizi wa Kitengo cha Wateja Binafsi, Innocent Urio amesema kampeni hiyo inalenga kuhamasisha watanzania kuthamini utamaduni wa kuweka akiba.

“Kupitia kampeni hii, wateja wetu watajipatia zawadi, lakini muhimu zaidi ni kujifunza thamani ya akiba kwa maisha yao ya kifedha,” alisema Urio.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Wafanyabiashara Wadogo na Wakati (SME), Juma Hamisi, alisisitiza kuwa wafanyabiasha sasa wana nafasi ya kunufaika na kampeni ya Gutuka na Ecobank ambapo mteja atakayefungua akaunti ya Supa Seva inampa mteja riba hadi asilimia 5 kwa robo mwaka bila makato ya mwezi, fursa ya kutoa pesa bure mara moja kila mwezi na huduma ya Lipa Namba bure kwa wateja wa SME na kadri mteja anavyoweka akiba zaidi, ndivyo anavyozidisha nafasi ya kushinda zawadi kubwa.

“Gutuka na Ecobank ni zawadi kwa wateja wetu kutokana na uaminifu wao katika safari ya miaka 40 barani Afrika na miaka 15 nchini Tanzania. Ni hatua ya kujenga utamaduni wa kuweka akiba kwa maisha bora kifedha,” alisema Hamisi.

NBAA YAWANOA WATAHINIWA MITIHANI CPA


Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) imeendesha warsha kwa njia ya mtandao pamoja na mafunzo ya ana kwa ana kwa wanafunzi wanaotarajia kufanya mitihani ya Bodi, ikilenga kuongeza ufanisi na maandalizi bora kwa watahiniwa wake.

Akizungumza wakati wa kufungua warsha hiyo kwa niaba ya  Mkurugenzi Mtendaji, Peter Lyimo, Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Elimu ya Taaluma na Mafunzo, , alisema kuwa warsha hiyo imelenga kuwanoa wanafunzi wa ngazi mbalimbali kupitia mbinu bora za kujibu mitihani, hasa kwenye maeneo yenye changamoto kubwa kwa watahiniwa.

“Yapo masomo ambayo kiwango cha ufaulu kimekuwa kidogo. Hivyo tumewaleta walimu kutoka vyuo na Taasisi mbalimbali ili watoe uzoefu na mbinu sahihi kwa watahiniwa, ili waweze kujiandaa vizuri,” alisema Lyimo.

Aidha, Lyimo alifafanua kuwa mbali na wanafunzi waliounganishwa kupitia mtandao, pia kulikuwa na kundi la wanafunzi waliofika moja kwa moja katika ofisi za Bodi (NBAA) kupata mafunzo hayo ya kitaalamu ana kwa ana. Hatua hii inalenga kuongeza ufanisi na kuwawezesha wanafunzi kuuliza maswali kwa urahisi zaidi na kupata mrejesho wa moja kwa moja kutoka kwa walimu.

Aliwasisitiza wanafunzi kuepuka kujiandaa kwa mazoea au kiholela na badala yake kutenga muda wa kutosha kujifunza, akibainisha kuwa kuna tofauti kubwa kati ya mitihani ya vyuoni na mitihani ya Bodi.

“Tumewasisitiza sana namna ya kujiandaa. Waweke muda wa kutosha kwenye kujifunza kwani mitihani ya Bodi inahitaji umakini mkubwa na maandalizi ya kitaalamu zaidi,” aliongeza.

Kwa mujibu wa Lyimo, NBAA imejipanga kuhakikisha kiwango cha ufaulu kinapanda katika mitihani yake mbalimbali, sambamba na kuongeza uelewa wa watahiniwa, ili baada ya kumaliza mitihani waweze kuwa wataalamu waliobobea kwenye uhasibu na ukaguzi.

Bodi hiyo imesisitiza kuwa hatua hii ni sehemu ya mkakati wake wa kuhakikisha kila mtahiniwa anapata maandalizi stahiki na changamoto zinazowakabili zinapatiwa suluhisho la kudumu.
Mkurugenzi wa Kurugenzi ya Elimu ya Taaluma na Mafunzo Peter Lyimo akizungumza wakati wa ufunguzi wa warsha kwa njia ya mtandao pamoja na mafunzo ya ana kwa ana kwa wanafunzi wanaotarajia kufanya mitihani ya Bodi
Mfanyakazi wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), Sawa Ngendabanka akiwakaribisha wanafunzi wanaotegemea kufanya mitihani mbalimbali ya Bodi ambao walikuwa wakisikiliza Warsha hiyo kwa njia ya mtandao.
Mkufunzi CPA Rashid Mganwa akitoa elimu kuhusu namna ya kujiandaa na kufanya masomo ya B2 na C1 kwa wanafunzi wanaotegemea kufanya mitihani ya Bodi waliokuwa wanafuatilia kwa njia mtandao.
Mkufunzi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, CPA Dkt. Emmanuel Christopher akitoa elimu kuhusu namna ya kujiandaa na kufanya masomo ya B1 na C3 kwa wanafunzi wanaotegemea kufanya mitihani ya Bodi waliokuwa wanafuatilia kwa njia mtandao.


Baadhi ya  wanafunzi wanaotarajia kufanya mitihani ya Bodi wakifuatilia mada pamoja na kuuliza maswai kwa wakufunzi

MABLOGA WASHUKURU UAMUZI WA SERIKALI KUWAPIGA MSASA KUIMARISHA WELEDI WAO



Na Mwandish wetu, Dar es Salaam.

CHAMA cha Mtandao wa Mabloga Tanzania (TBN) kimeshukuru uamuzi wa serikali ya kuwapatia mafunzo maalumu ya kunoa weledi na uzalendo wa wanachama wake kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu. Mabloga zaidi ya 200 wakiwemo wa diaspora walioanzisha Mtandao huo mwaka 2015 watapata mafunzo hayo. 

“Tumekuwa na mazungumzo na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ambao kimsingi ndio wasimamizi wakuu wa maudhui na wametuthibitishia kwamba wapo hatua za mwisho za kutekeleza maagizo ya serikali ya kutoa mafunzo kwa mabloga wote nchini,” alisema Mwenyekiti wa TBN , Beda Msimbe. 

Akifafanua kuhusu mafunzo hayo, Msimbe alisema kwamba lengo kuu la mafunzo ni kuwajengea mabloga weledi, uzalendo, na umakini katika kutambua na kupambana na habari feki, huku wakiwezesha usambazaji wa taarifa sahihi zitakazowawezesha wananchi kufanya maamuzi sahihi katika uchaguzi mkuu ujao. 

“ Tunahitaji kukumbushana kuhusu nchi hii, katiba yetu, amani na umuhimu wa uchaguzi katika demokrasia ya aina yetu.Uamuzi huu wa serikali wa kutupiga msasa ni muhimu sana” alifafanua.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari Mwenyekiti huyo wa TBN, Beda Msimbe, alieleza kuridhishwa na juhudi zinazofanywa na serikali kufanikisha mafunzo. Alisema wameomba mafunzo hayo kipindi cha sasa kwa kuwa wapo wanablogu ambao ni mara ya kwanza kuelekea katika uchaguzi mkuu, na kurejea ombi lao tena wakati wa mkutano wa wadau ulioandaliwa na Wizara ya Habari,Utamaduni,sanaa na michezo. 

Alisema kwamba uongozi wa TBN kwa sasa unafanya kazi kwa karibu na serikali kuhakikisha kuwa zaidi ya wanachama 150 wa chama hicho waliotawanyika nchini kote wanafaidika kikamilifu na mafunzo haya muhimu. 

Msimbe aliwataka mabloga wote nchini kuhakikisha wanawasiliana na Mratibu wa TBN, Bw. Gadiola Emanuel ili kuthibitisha anwani zao na kuhakikisha taarifa zao ziko sahihi kwa ajili ya ushiriki. Pia alitumia fursa hiyo kuwaalika wale wote ambao bado hawajajiunga na TBN kufanya hivyo sasa ili waweze kunufaika na fursa hii muhimu ya mafunzo. 

Chama cha Mabloga Tanzania (TBN) kinajumuisha mabloga wanaotengeneza aina mbalimbali za maudhui, ikiwemo michezo, habari za siasa, afya, uchumi, na habari mchanganyiko. Mafunzo haya yanatarajiwa kuimarisha uwezo wao wa kutoa taarifa zenye ukweli na uhakika, hivyo kuchangia katika mazingira ya uchaguzi yenye uwazi na uwajibikaji. 

NBAA YAZINDUA MFUMO WA KUKUSANYA TAARIFA ZA FEDHA ILI KUSAIDIA WADAU KUFANYA MAAMUZI SAHIHI


Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) imezindua rasmi mfumo mpya wa kukusanya taarifa za fedha zilizokwisha kukaguliwa na Wakaguzi wa Hesabu, ambao utaanza kutumika rasmi kuanzia Julai 1, 2025.

Mfumo huu unalenga kurahisisha upatikanaji wa taarifa sahihi za kifedha kwa matumizi ya mamlaka ya mapato (TRA), taasisi za kifedha, wadau wa mikopo, taasisi za serikali na binafsi, na mashirika mbalimbali, kwa ajili ya kufanya maamuzi muhimu ikiwemo utoaji wa mikopo na tenda kwa wazabuni.

Akizungumza jijini Dar es Salaam alipotembelea banda la NBAA katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba, Mwenyekiti wa Bodi ya NBAA, CPA Prof. Sylvia Temu, alisema mfumo huo ni hatua kubwa katika kuhakikisha taarifa za fedha zinakuwa na uwazi, uaminifu na uhalali wa kitaaluma, hasa kwa wale wanaohitaji kuzitumia katika maamuzi ya maendeleo ya kiuchumi na kibiashara.

“Kuanzia sasa, taarifa zote za fedha zilizokaguliwa zitakuwa zinaletwa moja kwa moja kwenye mfumo wa NBAA. Hii itasaidia taasisi kama TRA, taasisi za fedha, na wadau wengine kuhakikisha taarifa wanazozipokea ni sahihi, zimetolewa na wakaguzi walioidhinishwa, na zinaweza kutumika kama msingi wa kufanya maamuzi makubwa kama utoaji wa mikopo au kandarasi,” alieleza Prof. Temu.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Huduma za Shirika wa NBAA, CPA Kulwa Emmanuel Mandeleja, alisema mfumo huu utarahisisha sana mchakato wa uthibitishaji wa taarifa kwa taasisi mbalimbali, hasa zile zinazohitaji uthibitisho wa hali ya kifedha ya kampuni au taasisi kabla ya kutoa huduma au mikopo.

“Mfumo huu utahakikisha taarifa zote za kifedha zilizokaguliwa zinahifadhiwa sehemu moja salama na ya kuaminika. Hii itasaidia kwa kiasi kikubwa katika kufanya tathmini, kuzuia taarifa za kughushi na kuimarisha mchakato wa maamuzi ya kifedha katika taasisi nyingi,” alisema CPA Mandeleja.

NBAA imetoa wito kwa taasisi zote, watoa huduma za ukaguzi, na wahasibu kuhakikisha wanatumia mfumo huo mpya ipasavyo na kuhakikisha taarifa zote zinaingizwa kwa wakati kama sehemu ya uwajibikaji na weledi wa kitaaluma.

Kwa maelezo zaidi, wadau wanakaribishwa kutembelea banda la NBAA katika jengo la Wizara ya Fedha na Mipango katika viwanja vya Sabasaba au kutembelea tovuti ya NBAA: www.nbaa.go.tz.
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) CPA Prof. Sylvia Temu akizungumza na waandishi wa habari alipotembelea banda la Bodi hiyo lililopo ndani ya  jengo la Wizara ya Fedha.
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) CPA Prof. Sylvia Temu akisaini kitabu cha wageni alipotembelea banda la Bodi hiyo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) CPA Prof. Sylvia Temu akiwa kwenye picha ya pamoja na wafanyakazi wa NBAA alipotembelea banda la Bodi hiyo lililopo ndani ya jengo la Wizara ya Fedha. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa Huduma za Shirika kutoka NBAA CPA Kulwa Malendeja.

NBAA YASHIRIKI MAONESHO YA 49 YA KIMATAIFA YA BIASHARA YA SABASABA 2025



Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) inashiriki Maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya 49 yanayoendelea kwenye Viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam, ikiwa ni jitihada za kuonyesha huduma mbalimbali zinazotolewa na Bodi hiyo pamoja na kutoa elimu kwa wananchi.

Banda la NBAA lipo ndani ya jengo la Wizara ya Fedha linawahudumia wananchi kwa kutoa maelekezo ya usajili wa mitihani katika ngazi mbalimbali za taaluma ya uhasibu, pamoja na kutoa maelekezo kuhusu ulipaji wa ada na huduma nyingine muhimu.

Akizungumza na Michuzi Blog, Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa NBAA, Magreth Kageya alisema kuwa katika kipindi hiki cha Sabasaba Bodi imewasogezea wananchi huduma karibu kwa kutoa huduma zote kama vile usajili wa watahiniwa wa mitihani ya Bodi, usajili wa wanachama wa ngazi mbalimbali, usajili wa Makampuni, usajili wa kozi mbalimbali zinazoendeshwa na Bodi mfano 'Certificate na Diploma ya IPSAS', 'Professional Diploma in Internal Auditing' ambayo ni kozi mpya kwa wanaofanya kazi kwenye idara za ukaguzi wa ndani ili kuwasaidia kuwa na uelewa kwenye masuala ya ukaguzi.

Aidha, Bi. Kageya aliongeza kwamba NBAA kwa sasa inatumia mifumo ya kidijitali kutoa huduma zake, ambapo wananchi wanaweza kufikia huduma hizo kupitia tovuti rasmi ya Bodi ambayo ni www.nbaa.go.tz.

Maonesho haya ya Sabasaba ni fursa kubwa kwa Bodi ya NBAA kuwasiliana moja kwa moja na wananchi na wadau mbalimbali wa taaluma ya uhasibu na ukaguzi, ili kuboresha utoaji wa huduma na kuelimisha kuhusu umuhimu wa taaluma hiyo katika maendeleo ya taifa.

Wafanyakazi wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) wakiwa kwenye picha ya pamoja katika banda la Bodi hiyo lililopo ndani ya jengo la Wizara ya Fedha.


Huduma zikiendelea kwenye banda la NBAA