MABLOGA WASHUKURU UAMUZI WA SERIKALI KUWAPIGA MSASA KUIMARISHA WELEDI WAO
By: VIJIMAMBO on July 18, 2025 / comment : 0 Habari
Na Mwandish wetu, Dar es Salaam.
CHAMA cha Mtandao wa Mabloga Tanzania (TBN) kimeshukuru uamuzi wa serikali ya kuwapatia mafunzo maalumu ya kunoa weledi na uzalendo wa wanachama wake kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu. Mabloga zaidi ya 200 wakiwemo wa diaspora walioanzisha Mtandao huo mwaka 2015 watapata mafunzo hayo.
“Tumekuwa na mazungumzo na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ambao kimsingi ndio wasimamizi wakuu wa maudhui na wametuthibitishia kwamba wapo hatua za mwisho za kutekeleza maagizo ya serikali ya kutoa mafunzo kwa mabloga wote nchini,” alisema Mwenyekiti wa TBN , Beda Msimbe.
Akifafanua kuhusu mafunzo hayo, Msimbe alisema kwamba lengo kuu la mafunzo ni kuwajengea mabloga weledi, uzalendo, na umakini katika kutambua na kupambana na habari feki, huku wakiwezesha usambazaji wa taarifa sahihi zitakazowawezesha wananchi kufanya maamuzi sahihi katika uchaguzi mkuu ujao.
“ Tunahitaji kukumbushana kuhusu nchi hii, katiba yetu, amani na umuhimu wa uchaguzi katika demokrasia ya aina yetu.Uamuzi huu wa serikali wa kutupiga msasa ni muhimu sana” alifafanua.
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari Mwenyekiti huyo wa TBN, Beda Msimbe, alieleza kuridhishwa na juhudi zinazofanywa na serikali kufanikisha mafunzo. Alisema wameomba mafunzo hayo kipindi cha sasa kwa kuwa wapo wanablogu ambao ni mara ya kwanza kuelekea katika uchaguzi mkuu, na kurejea ombi lao tena wakati wa mkutano wa wadau ulioandaliwa na Wizara ya Habari,Utamaduni,sanaa na michezo.
Alisema kwamba uongozi wa TBN kwa sasa unafanya kazi kwa karibu na serikali kuhakikisha kuwa zaidi ya wanachama 150 wa chama hicho waliotawanyika nchini kote wanafaidika kikamilifu na mafunzo haya muhimu.
Msimbe aliwataka mabloga wote nchini kuhakikisha wanawasiliana na Mratibu wa TBN, Bw. Gadiola Emanuel ili kuthibitisha anwani zao na kuhakikisha taarifa zao ziko sahihi kwa ajili ya ushiriki. Pia alitumia fursa hiyo kuwaalika wale wote ambao bado hawajajiunga na TBN kufanya hivyo sasa ili waweze kunufaika na fursa hii muhimu ya mafunzo.
Chama cha Mabloga Tanzania (TBN) kinajumuisha mabloga wanaotengeneza aina mbalimbali za maudhui, ikiwemo michezo, habari za siasa, afya, uchumi, na habari mchanganyiko. Mafunzo haya yanatarajiwa kuimarisha uwezo wao wa kutoa taarifa zenye ukweli na uhakika, hivyo kuchangia katika mazingira ya uchaguzi yenye uwazi na uwajibikaji.
NBAA YAZINDUA MFUMO WA KUKUSANYA TAARIFA ZA FEDHA ILI KUSAIDIA WADAU KUFANYA MAAMUZI SAHIHI
By: VIJIMAMBO on July 07, 2025 / comment : 0 Habari
NBAA YASHIRIKI MAONESHO YA 49 YA KIMATAIFA YA BIASHARA YA SABASABA 2025
By: VIJIMAMBO on June 30, 2025 / comment : 0
Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) inashiriki Maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya 49 yanayoendelea kwenye Viwanja vya Sabasaba jijini Dar es Salaam, ikiwa ni jitihada za kuonyesha huduma mbalimbali zinazotolewa na Bodi hiyo pamoja na kutoa elimu kwa wananchi.
Banda la NBAA lipo ndani ya jengo la Wizara ya Fedha linawahudumia wananchi kwa kutoa maelekezo ya usajili wa mitihani katika ngazi mbalimbali za taaluma ya uhasibu, pamoja na kutoa maelekezo kuhusu ulipaji wa ada na huduma nyingine muhimu.
Akizungumza na Michuzi Blog, Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano wa NBAA, Magreth Kageya alisema kuwa katika kipindi hiki cha Sabasaba Bodi imewasogezea wananchi huduma karibu kwa kutoa huduma zote kama vile usajili wa watahiniwa wa mitihani ya Bodi, usajili wa wanachama wa ngazi mbalimbali, usajili wa Makampuni, usajili wa kozi mbalimbali zinazoendeshwa na Bodi mfano 'Certificate na Diploma ya IPSAS', 'Professional Diploma in Internal Auditing' ambayo ni kozi mpya kwa wanaofanya kazi kwenye idara za ukaguzi wa ndani ili kuwasaidia kuwa na uelewa kwenye masuala ya ukaguzi.
Aidha, Bi. Kageya aliongeza kwamba NBAA kwa sasa inatumia mifumo ya kidijitali kutoa huduma zake, ambapo wananchi wanaweza kufikia huduma hizo kupitia tovuti rasmi ya Bodi ambayo ni www.nbaa.go.tz.
Maonesho haya ya Sabasaba ni fursa kubwa kwa Bodi ya NBAA kuwasiliana moja kwa moja na wananchi na wadau mbalimbali wa taaluma ya uhasibu na ukaguzi, ili kuboresha utoaji wa huduma na kuelimisha kuhusu umuhimu wa taaluma hiyo katika maendeleo ya taifa.
Wafanyakazi wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) wakiwa kwenye picha ya pamoja katika banda la Bodi hiyo lililopo ndani ya jengo la Wizara ya Fedha.
Huduma zikiendelea kwenye banda la NBAA
NBAA YATANGAZA MATOKEO YA MITIHANI YA MEI, 2025
By: VIJIMAMBO on June 26, 2025 / comment : 0 Habari
WAZIRI MKUU MAJALIWA AWASISITIZA WATUMISHI WA UMMA KUTOA HUDUMA BORA, TCAA YATOA ELIMU KUHUSU USAFIRI WA ANGA
By: VIJIMAMBO on June 23, 2025 / comment : 0 Habari
NBAA KUANZISHA KANZI DATA ( DATABASE) YA WANAFUNZI WA UHASIBU VYUONI
By: VIJIMAMBO on June 20, 2025 / comment : 0 Habari
Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA) imeweka mikakati ya kuanzisha kanzi data (database) ya wanafunzi wanaosomea masomo ya uhasibu katika vyuo mbalimbali nchini, ili kuwezesha ufuatiliaji wa karibu wa maendeleo yao kitaaluma na kuwasaidia katika maandalizi ya mitihani ya Bodi hiyo.
Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA, CPA Pius A. Maneno, Afisa Tawala na Rasilimali Watu wa NBAA, Bi. Gloria Kaaya, alisema kuwa hatua hiyo inalenga kuongeza ufanisi katika usimamizi wa taaluma ya uhasibu na kuhakikisha kuwa wanafunzi wanapata taarifa sahihi kwa wakati kuhusu masuala ya kitaaluma.
"Tumeanzisha mpango huu ili kuwatambua na kuwafuatilia wanafunzi wote wanaosomea uhasibu vyuoni. Kupitia "database" hii, tutawawezesha kupata taarifa muhimu kuhusu taratibu za mitihani, masharti ya kupata misamaha "exemptions", na muda sahihi wa kuanza mitihani ya kitaaluma baada ya kuhitimu," alisema Bi. Kaaya.
Aliongeza kuwa baadhi ya wanafunzi wamekuwa wakikosa fursa ya kufanya mitihani ya Bodi kwa wakati kutokana na kutokuwa na taarifa sahihi, au kuchelewa kujiandikisha ndani ya muda unaotakiwa, hasa pale inapozidi miaka mitano tangu kumaliza masomo yao.
Kwa mujibu wa NBAA, "database" hiyo pia itarahisisha mawasiliano kati ya Bodi, vyuo vya elimu ya juu na wanafunzi wenyewe, hivyo kuongeza uwazi na ufanisi katika utekelezaji wa majukumu ya kitaaluma nchini.
"Tunataka wanafunzi wote waelewe fursa walizonazo na wajue hatua wanazopaswa kuchukua ili kufikia malengo yao ya kitaaluma. Mfumo huu utasaidia kuongeza idadi ya wataalamu wa uhasibu waliothibitishwa, ambao ni rasilimali muhimu kwa maendeleo ya uchumi wa taifa," alisisitiza.
NBAA imetoa wito kwa taasisi za elimu ya juu kushirikiana na Bodi hiyo katika utekelezaji wa mpango huu kwa kuhakikisha taarifa za wanafunzi zinasajiliwa kwa usahihi, huku ikiwataka wanafunzi kufuatilia matangazo rasmi ya Bodi hiyo kupitia tovuti na mitandao yake ya kijamii.
Afisa Tawala na Rasilimali watu NBAA, Gloria Kaaya akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA, CPA Pius A. Maneno kuhusu mikakati ya kuanzisha kanzi data (database) ya wanafunzi wanaosomea masomo ya uhasibu katika vyuo mbalimbali nchini kwa wakuu wa Idara za Fedha na Uhasibu vyuoni.
Baadhi ya wakuu wa Idara za Fedha na Uhasibu vyuoni pamoja na watumishi wa NBAA wakifuatilia mada
Picha ya pamoja
PAMOJA BLOG

WANAOTUTEMBELEA
ZINAZOSOMWA ZAIDI
-
Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tati...
-
Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tati...
-
Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tati...
-
Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tati...
-
Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tati...
-
November 25th is the International Day for the elimination of Violence against women in the world. The 16 days up to December 10th the Huma...
-
N a Mwandish wetu, Dar es Salaam. CHAMA cha Mtandao wa Mabloga Tanzania (TBN) kimeshukuru uamuzi wa serikali ya kuwapatia mafunzo maalumu ya...
-
Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tati...
-
Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tati...
-
Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tati...
BLOGU MARAFIKI
KUMBUKUMBU
HABARI ZINGINE
