HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » SAKATA LA WAFANYA KAZI WA MIGODINI HUKO AFRIKA YA KUSINI BADO HAKIJAELEWEKA

Wafanyikazi wa Lonmin
Wachimba migodi waliofika kazini lakini pasipo kufanya kazi 
Wafanyikazi wa migodi nchini Afrika Kusini wameanza kurudi mmoja mmoja katika migodi ya dhahabu nyeupe, platinum, ambako polisi waliwafyatulia risasi wenzao na kusababisha vifo vya watu 34 Alhamisi iliyopita.
Hata hivyo idadi ya wachimba migodi hao haijatosha kiasi cha shughuli za uchimbaji migodi kuendelea kikamilifu.
Kampuni ya Lonmin ilitangaza kwamba imeanza tena shughuli zake, lakini ukweli ni kwamba ni chini ya thuluthi moja tu ya wafanyakazi waliofika katika migodi, na kazi haijaanza.
Kampuni pia ilitangaza kwamba imetenga muda wa wafanyakazi wote kurudi kazini, na kuongezea muda huo hadi Jumanne.
Imetisha kwamba watakaoshindwa kufanya hivyo, basi watafutwa kazi.
Rais Jacob Zuma alitangaza wiki nzima ya maombolezi kufuatia vifo vya wachimba migodi waliouawa.
Vile vile alitaka uchunguzi kamili kufanyika.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: