Kwa Mapenzi Mema
kama mdau wa blog ako napenda niwajuze Watanzania kuwa kuna wimbi la utapeli hapa mjini dar es salaam
na watu hawa wanatumia majina ya taasisi za TANAPA, TFDA na AGRO CHEMICALS.
wanachokifanya hawa jamaa wanapata contact kupitia Business cards au kadi za harusi sehemu ya RSPV ambapo huwa
kuna namba za simu za wahusika wakuu.
hivyo ukupigia kwa bashasha kana kwamba mnajuana na wana care iliyotukuka adabu wakati wa mawasiliano
baada
ya kujitambilisha kwa kukutaja jina basi nanukuu "tumeona hapa mjini
kizuri ule na ndugu yako sasa kuna wazungu wametoka Norway
wanatafuta dawa ya mifugo aina ya GUSTAVIC ambapo hupatikana TFDA,TANAPA au AGRO CHEMICALS kwa sh za kitanzania Millioni
I.2 kwa ujazo wa Mls 1000 na wao wanataka Mls 10,000 " mwisho wa kunukuu.
sasa watakutaka wewe(target yao) hawataki hawa wazungu wajue hizi sehemu na wao ndo wako nao hao wazungu yaani matapeli sasa
wanataka wewe uende wakakupe pesa ukanunue hizo dawa kwa moja ya sehemu hizo tajwa na wanakupatia namba ya dokta wa kukuuzia
alfu ukizileta kwa wazungu uwaambie umenunua kwa sh millioni 2.5 na faida hiyo watakumegea kwa aslimia kadhaa.
Ni watu wengi wamelizwa hivyo nimeona niwajuze watanzania wengine wawe macho
Mjumbe Mwajuma
Dar es salaam





No comments:
Post a Comment