KONGAMANO LA WANAWAKE KUHUSU KATIBA MPYA
WANAWAKE
kutoka mikoa yote nchini wamepata fursa ya kushiriki Kongamano la
kwanza la Kitaifa la wanawake kujadili masuala muhimu ya haki za wanwake
wanazotaka ziingie kwenye Katiba mpya.
Kongamano
hilo liloandaliwa na Mfuko wa Wanawake Tanzania (WFT), linafanyika kwa
siku tatu kuanzia 22-24 Oktoba 2012 jijini Dar es salaam, ambap[o
watajadili kwa kina na kuchambua mapungufu ya katiba inayotumika hivi
sasa na kuwekeana maazimio ya masuala yatakayotakiwa kuingizwa kwenye
mahudhui ya Katiba mpya inayotarajiwa kuanza kutumika ifikapo 2014.
Mkurugenzi Mtendaji wa WFT Mary Rusimbi akichangia mada
Washiriki wa Kongamano la masuala ya Haki za Wanawake na Katiba Tanzania lililoandaliwa na Mfuko wa wanawake Tanzania (WFT).
Pamoja na mambo mengine, mada zinazotolewa kwenye Kongamano hilo ni Umuhimu wa katiba katika maendeleo ya wanawake, mapungufu ya Kijinsia Katika Katiba iliyopo, haki za msingi za mwanamke za kuzingatia Katika katiba mpya, masuala muhimu ya kuzingatia katika haki za wanawake na kuwekeana mikakati ya kutumia vizuri fursa ya mchakato wa uuandwaji wa katiba mpya.
Pamoja na mambo mengine, mada zinazotolewa kwenye Kongamano hilo ni Umuhimu wa katiba katika maendeleo ya wanawake, mapungufu ya Kijinsia Katika Katiba iliyopo, haki za msingi za mwanamke za kuzingatia Katika katiba mpya, masuala muhimu ya kuzingatia katika haki za wanawake na kuwekeana mikakati ya kutumia vizuri fursa ya mchakato wa uuandwaji wa katiba mpya.
Post a Comment