HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » Majambazi Watano Moshi, Ofisa Uhamiaji Aponea Chupuchupu

Waandishi Wetu, Moshi na Mwanza
SIKU chache baada ya gazeti hili kuripoti kuibuka kwa kundi la majambazi wanaoua kwa kutumia sindano za sumu, kkisha upora wananchi, olisi mkoani Kilimanjaro imejibu mapigo na kuua watu watano wanaotuhumiwa kuwa washirika wa kundi hilo.
Watuhumiwa hao ambao walikutwa na sanduku (Briefcase) lenye mabomba ya sindano na uzi wa kushonea majeraha makubwa, waliuawa usiku wa kuamkia jana katika kile polisi walichoeleza kuwa ni katika harakati za kurushiana risasi na majambazi hao.
Katika tukio hilo, polisi mmoja PC Lameck mwenye nambar G406 alijeruhiwa mguu wa kushoto na chembechembe za risasi zilizokuwa zikifyatuliwa na majambazi hao.
Tukio hilo lililotokea, siku chache baada ya Mbunge wa Vunjo, Augustine Mrema (TLP) kuwataka polisi kujibu mapigo kutokana na kuongezeka kwa vitendo vya ujambazi jimboni kwake, lilitokea Kijiji cha Kyala eneo la Marangu, wilayani Moshi Vijijini.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz alisema licha ya kurushiana risasi, polisi walilazimika kurusha bomu la machozi ndani ya nyumba walimokuwa wamejificha washirika wa kundi hilo.
Boaz alisema baada ya kupekuliwa majambazi hao, walikutwa na bunduki aina ya Shotgun Greener yenye namba 858356 ikiwa na risasi nne na maganda ya risasi, bastola aina ya Browning na risasi mbili na risasi 10 za bunduki aina ya SMG.
Licha ya silaha hizo, majambazi hao walikutwa pia na mapanga na sime zilizokuwa na damu, zana mbalimbali za kuvunjia, mali mbalimbali zinazodaiwa kuporwa kwa watu na nyama za mbuzi na kondoo.
Waliouawa wametambuliwa kuwa ni Paul Baltazar (25), mmiliki wa nyumba walimokuwa wamejificha majambazi hao na Remius Msambure (30), Focaus Mtui (35) na mmoja aliyetambuliwa kwa jina moja la Elias, huku maiti moja ikiwa haijatambuliwa.
Akifafanua kuhusu tukio hilo, Boaz alisema juzi saa 7:00 usiku wa kuamkia jana, polisi walipokea taarifa kuwa Kijiji cha Kitowo Marangu, kundi la majambazi watano lilikuwa limevamia duka la mfanyabiashara aliyetajwa kuwa ni Gaudence Temu.
Katika tukio hilo, majambazi hao walimjeruhi kwa mapanga mlinzi aitwaye Hamis Mnyaru (25) kabla ya kuwashambuliwa walinzi wa jadi maarufu kama Sungusungu waliotajwa kuwa ni, Richard Temu (33) na Erick Yuda (30) ambao walijitokeza kutoa msaada.
Kamanda Boaz alisema ufuatiliaji wa kina ulifanyika ili kubaini maficho yao na kugundua kuwa, walikuwa wakijificha katika nyumba Kijiji cha Kyala ndipo walipokwenda na kuvamia wakiwataka wajisalimishe lakini wakakataa.
Alisema polisi walilazimika kujibu mapigo na kufanikiwa kuwaua kwa risasi watuhumiwa watano wakati wakijaribu kutoroka kutoka katika nyumba hiyo.
Katika tukio linguine, Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Mwanza, Albert Buchafwe amenusurika kuuawa kwa risasi baada ya kudaiwa kushambuliwa na Mkuu Msaidizi wa Kituo cha Polisi Nyakato, Abubakar Zebo kwa madai kuwa walikuwa wakishambulia jambazi.
Tukio hilo ambalo limethibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Liberatus Barlow linadaiwa kutokea saa 4:13 usiku wakati ofisa wa uhamiaji akiwa njiani kuelekea nyumbani kwake, alikutana na gari ndogo aina ya Suzuki lililomwashia taa likimuashiria kusimama.
Akielezea mkasa huo, Buchafwe alisema baada ya kuwashiwa alipochunguza kwa makini gari hilo alibaini kuwa ni lile linalotumika na ofisa huyo wa polisi, hivyo alisimama na kujitambulisha kwake akiwa ndani ya gari lakini aliamuriwa kuzima taa za gari lake na kutoka ndani.
“Nilitii nikazima taa, lakini nilisita kutoka katika gari langu, nilijitambulisha kwamba ni ofisa uhamiaji na kumtaja jina ofisa huyo (wa polisi), ambaye aliendelea kunilazimisha kushuka ndani ya gari huku nikiona akijiweka sawa ikiwamo kuandaa bastora tayari kushambulia,” alisema.
Alisema wakati akiwa bado anajitambulisha, alishuka askari aliyekuwa na sare katika gari hilo la ofisa wa polisi akiwa na silaha ya SGM, hali ambayo ilimlazimu kugeuza gari haraka na kukimbia huku gari lake likishambuliwa nyuma kwa risasi.
Buchafwe alisema amepata na mashaka na tukio hilo kutokana na askari huyo aliyehusika kuwa na uhusiano wa karibu na mkewe, ambaye wamekuwa na ugomvi naye pamoja na kesi ya kutalikiana mahakamani na kwamba, huenda halikuwa la bahati mbaya.
“Nina kesi na mke wangu mahakamani,ofisa huyu wa polisi amekuwa na uhusiano wa karibu na mke wangu ambaye tunashtakiana mahakamani, inanishangaza mtu ambaye ananifahamu licha ya kujitambulisha bado alikuwa akishilikilia msimamo wa kunitaka kushuka, nadhani hapa kuna jambo zaidi ya hali ilivyo,” alieleza.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Leberatus Barlow alikiri kuwapo kwa tukio hilo na kwamba, ana uhakika ni bahati mbaya kwani jeshi lake lilipata taarifa za Kiintelijensia za kuwapo kwa majambazi wakidaiwa kutumia gari sawa na la ofisa huyo.
“Hili ni tukio la bahati mbaya, jeshi letu lilipata taarifa za Kiintelijensia juu ya kuwapo kwa majambazi na kuamua kuweka mtego, sasa ofisa huyu alifika muda na wakati ambao askari wetu walikuwa eneo hilo na kuingia mtego wetu, alikuja na gari ambalo ni sawa na lile ambalo tulielezwa lingetumika, lakini bahati nzuri mauaji hayakutokea,” alisema.

Imeandikwa na Daniel Mjema, Rehema Matowo, Moshi na Frederick Katulanda, Mwanza

CHAZO: http://www.mwananchi.co.tz

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: