HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » Meseji ya Mauaji ya Barlow Yanaswa

Kamanda Barlow 

Kupatikana kwa wauaji hao, kumetokana na simu ya Mwalimu Dorothy Moses kupitia ujumbe wa simu aliokuwa akiwasiliana na wahusika.


Siku moja baada ya Jeshi la Polisi kutoa taarifa ya awali ya uchunguzi wa mauaji ya kifo cha aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Liberatus Barlow, ujumbe mfupi wa simu ya mkononi kwa ajili ya kutekeleza mauaji hayo imenaswa.
Kamanda Barlow aliuawa usiku wa manane alipokuwa akitoka kwenye kikao cha harusi ya ndugu yake. Alifikwa na mauti hayo baada ya kupigwa risasi akimsindikiza Mwalimu Doroth Moses.
Habari zilizopatikana kutoka kwa baadhi ya makachero jijini Mwanza zinaeleza kuwa, ukweli wa mauaji hayo umebainika na kwamba watuhumiwa waliokamatwa wanahusika moja kwa moja na mpango kamili wa mauaji hayo.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, inadaiwa kuwa Kamanda aliuawa baada ya mmoja wa wahalifu aliyekuwa akikabiliwa na kesi nzito (jina tunalihifadhi) kutoa kiasi cha fedha kupitia kwa mtu wake wa karibu ili kutekeleza mpango wa mauaji ya kulipiza kisasi.
Kupatikana kwa wauaji hao, kumetokana na simu ya Mwalimu Dorothy Moses kupitia ujumbe wa simu aliokuwa akiwasiliana na wahusika.
Hata hivyo, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Lilian Matola alipoulizwa kuhusiana na tukio hilo,  alisema taarifa siyo za kweli na kusisitiza kwamba taarifa aliyoitoa DCI Robert Manumba ndiyo sahihi.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: