MBUNGE
wa Ubungo (Chadema) John Mnyika amewasilisha kwenye ofisi za Bunge
kusudio la muswada binafsi wa kubadili sheria moja ya vipengele
vinavyosimamia kanuni za mafao kwa Taasisi ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii
kuhusu kusimamishwa kwa fao la kujitoa.
Mnyika
aliwasilisha kusudio hilo kwa Katibu wa Bunge jijini Dar es Salaam jana
akisema amefanya hivyo baada ya kubaini Serikali iko usingizini licha ya
kuahidi kufanya marekebisho ya sheria hiyo.
Mbunge huyo
alieleza hayo jana kupitia taarifa yake kwa gazeti hili akisema
anatarajia kuwasilisha katika Bunge lijalo muswada binafsi wa sheria ya
Marekebisho ya sheria za hifadhi ya jamii kwa hati ya dharura
akizingatia kanuni ya 81 ya Kanuni za Kudumu za Bunge toleo la 2007.
“Lengo la Muswada huu ni kufanya marekebisho yenye kuboresha mfumo wa utoaji wa mafao nchini ikiwemo kuwezesha kutolewa kwa fao la kujitoa na mafao mengine muhimu ambayo hayatolewi katika utaratibu wa sasa wa mifuko mbalimbali ya hifadhi ya jamii,” alisema Mnyika.
“Lengo la Muswada huu ni kufanya marekebisho yenye kuboresha mfumo wa utoaji wa mafao nchini ikiwemo kuwezesha kutolewa kwa fao la kujitoa na mafao mengine muhimu ambayo hayatolewi katika utaratibu wa sasa wa mifuko mbalimbali ya hifadhi ya jamii,” alisema Mnyika.
Mnyika
alisema amefikia uamuzi huo kwa kuwa mpaka sasa zimebaki siku chache
Mkutano wa Tisa wa Bunge kuanza wakati Serikali imekaa kimya licha ya
kuahidi kuwa itapeleka marekebisho ya Sheria ya Hifadhi ya Jamii
Bungeni.
“Mpaka sasa Serikali haijaitisha mkutano na wafanyakazi pamoja na wadau wa jamii kupokea mapendekezo, hali ambayo inaashiria upo uwezekano muswada huo usiwasilishwe kwa wakati,” alisema Mnyika.
“Mpaka sasa Serikali haijaitisha mkutano na wafanyakazi pamoja na wadau wa jamii kupokea mapendekezo, hali ambayo inaashiria upo uwezekano muswada huo usiwasilishwe kwa wakati,” alisema Mnyika.
Taarifa hiyo
iliongeza kuwa kufutwa kwa mafao ya kujitoa msingi wake haupo kwenye
marekebisho ya sheria yaliyofanyika Aprili13 mwaka huu pekee bali ni
udhaifu katika mfumo mzima wa kisera na kisheria wa hifadhi ya jamii
nchini, hali ambayo inahitaji wadau kutaka mabadiliko.
“Kufuatia
kuanza kutumika kwa Sheria hiyo (ya 13 Aprili 2012) maombi mapya ya
kujitoa yamesitishwa kwa kipindi cha miezi sita hadi pale miongozo
itakapotolewa ili kuwezesha Mamlaka na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kutoa
elimu kwa wadau
CHANZO: Mwananchi




No comments:
Post a Comment