HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » Mkutano Wa AAPAM Waalezwa Kuwa Na Mafanikio Makubwa


Mkutano wa 34 wa jumuiya ya Afrika ya Utawala wa Umma na Usimamizi Bora (AAPAM) umeelezwa kuwa wa mafanikio makubwa zaidi tokea kuanzishwa kwa Taasisi hiyo mwaka 1976.

Wajumbe wa mkutano wa siku tano wa AAPAM wamesema idadi ya washiriki mwaka huu wamekuwa wengi kupita mikutano mengine yote iliyofanyika kabla kutokana na kila nchi kuwa na hamu ya kutuma wajumbe wake Zanzibar.

Wamesema kuwa licha ya idadi kubwa ya wajumbe, wameridhishwa na maandalizi mazuri yaliyofanywa na Serikali na wanategemea mkutano huo utaleta mabadiliko makubwa ya utumishi ya umma kwa nchi za Afrika kutokana na wataalamu wengi wa ngazi za juu kushiriki mkutano huo na kutoa mada zao. 

Wajumbe hao ambao wamepata nafasi ya kutembelea sehemu mbali mbali za mjini na mashamba wamesema Zanzibar inanafasi kubwa ya kupiga hatua katika masuala ya kiuchumi na kijamii iwapo itaweza kutumia ipasavyo rasilimali ilizonazo ikiwa ni pamoja na bandari, fukwe, matunda, bahari na ardhi yenye rutuba.

Meneja utawala wa kampuni kubwa nchini Lesothu, Majid Maan amesema anashangazwa kusikia kwamba Zanzibar haisafirishi samaki wala matunda nje ya nchi wakati sehemu zote walizopita zimezungukwa na miti ya matunda.

“Sisi kule Lesothu na baadhi ya nchi jirani tunahitaji sana maembe na ndizi na Zanzibar matunda haya yapo ya kutosha kwanini Wafanyabiashara wa hapa wasijitoe kutafuta soko sehemu hizi,” aliuliza Meneja Majid.

Alitoa rai kwa Serikali kupitia Wizara inayohusika na Biashara kutumia Umoja wa nchi za Kusini mwa Afrika SADDEC na Jumuia nyengine za Magharibi na Kusini mwa Afrika kujitangaza na amesema anauhakika mazao ya Zanzibar yananafasi kubwa ya kupata soko la uhakika.

Baadhi ya wajumbe wameishauri Serikali kuanzisha uvuvi wa bahari kuu baada ya kushuhudia wavuvi wengi wa Bandari ya Nungwi wakirudi kuvua wakiwa na samaki wadogo huku visiwa vya Zanzibar vikiwa vimezungukwa na bahari kuu yenye samaki wengi wakubwa.

Mkutano huo unatarajiwa kufungwa kesho wakati wa mchana na kabala ya kufungwa rasmi itatangazwa nchi itakayo kuwa mwenyeji wa mkutano ujao wa 35.
 
IMETOLEWA NA HABARI MAELEZO ZANZIBAR

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: