HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » MSANII JOHN MAGANGA KUZIKWA JUMANNE R.I.P BROTHER

Marehemu John Steven enzi za uhai wake

TASNIA ya filamu nchini Tanzania, jana imefikwa na msiba mwingine Mkubwa wa Msanii wa Filamu, John Stephano Maganga aliyefariki katika Hospitali ya Muhimbili alikokuwa akipatiwa matibabu baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa viongozi wa Wasanii zinasema kuwa Mipango ya mazishi inafanyika Nyumbani kwao Mwananyama A jirani na Kopakabana Bar  jijini Dar es Salaam.

Marehemu John anaetarajiwa kuzikwa siku ya jumanne Makaburi ya Kinondoni Dar es Salaam, alianza kujiingiza katika sanaa ya uigizaji mwaka 2001 chini Thea na Deo Shija na ilipofika mwaka 2008 alianza kuigiza filamu na hadi mauti yanamfika alikuwa njiani kutoa Filamu yake.

Aidha Wasanii wote wanataarifiwa kufika katika Kikao Maalum Nyumbani kwa John Stephan oleo Saa tisa alasiri kwaajili ya kupanga mikakati, ya mazishi.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: