MAHAFALI YA WANAFUNZI WA KIISLAMU JITEGEMEE SEKONDARI
Mbunge wa
Wawi kwa tiketi ya Chama Cha Wananchi (CUF) Hamadi Rashid Mohamed,
akizungumza na wahitimu wa kidato cha sita wa Jumuiya ya Wanafunzi wa
Kiislamu wa Shule ya Sekondari Jitegemee (JIMSA) ya jijini Dar es Salaam
jana wakati wa mahafali yao ya 9 tangu kuanzishwa kwa jumuiya hiyo
ambapo jumla ya wanafunzi 42 wamehitimu masomo yao wakiwa wanaume 26 na
wanawake 16, kulia ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Vijana Bakwata Taifa
Rajab Alqushairiyyu na katibu Omary Msinzia.
Baadhi ya wahitimu wakike wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi kwenye mahafali hayo.
Baadhi ya wahitimu wakiume wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi.
Mbunge wa
Wawi Hamad Rashid Mohamed akiwa kwenye picha ya pamoja na wahitimu hao
wakiislamu wa shule ya sekondari Jitegemee mara baada ya mahafali yao
yaliyoandaliwa na Jumuiya ya wanafunzi wa Kiislamu ya shule hiyo.
Changamoto zinazowakabili zilizoelezwa kwenye risala ya wanafunzi hao
Ni ukosefu wa mwalimu rasmi kwa somo la Islamic Knowledge,
Kutoruhusiwa
kuvaa hijabu ingawa shule zingine za Jeshi hilo kama Makongo na Airwing
wanaruhusiwa kuvaa lakini Jitegemee imekuwa vigumu kuruhusu pamoja na
aliyekuwa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi na Usalama Abdurahmani Shimbo
kwenye mahafali kama hayo alitoa agizo kuwa wanafunzi wakiislamu
waruhusiwe kuvaa hijabu lakini agizo hilo halijatekelezwa.
Jumuiya
ya wanafunzi wa Kiislamu Jitegemee (JIMSA) ilianzishwa 2004 ikiwa na
Jumla ya wanachama 80 mpaka hivisasa inawanachama 233. Kati ya hao
wanaume ni 185 na wanawake ni 48 na maustadh wanaofundisha dini kwa siku
ya alhamisi sita.
PICHA KWA HISANI YA HABARI MSETO
Post a Comment