Habari kutoka jijini Dar es Salaam ambazo zimetua katika mtandao
huu hivi punde na kurushwa moja kwa moja na kituo cha radio Nuru Fm
93.5 Mhz kupitia mwandishi wetu Dotto Mwaibale zinadai kuwa jengo
la PPF TOWER lililopo katikati ya jiji la Dar es Salaam kwa sasa
linaendelea kuteketea kwa moto .
Tukio hilo limetokea majira ya saa 1.30 asubuhi ya leo baada ya walinzi wa jengo hilo kushuhudia moshi mzito ukitoka kutoka ndani ya jengo hilo katika ghorofa ya mwisho na hivyo kulazimika kutoa taarifa vikosi vya zimamoto .
Hata hivyo inadaiwa kuwa kikosi cha jeshi la zimamoto na uokoaji wamefika mapema zaidi eneo la tukio na askari wake kufanikiwa kupanda hadi juu ya ghorofa hiyo ambako moto huo ulianzia kuwaka ili kujaribu kuzima japo shida kubwa ni mpira wa maji kufika katika eneo hilo.
Tukio hilo limetokea majira ya saa 1.30 asubuhi ya leo baada ya walinzi wa jengo hilo kushuhudia moshi mzito ukitoka kutoka ndani ya jengo hilo katika ghorofa ya mwisho na hivyo kulazimika kutoa taarifa vikosi vya zimamoto .
Hata hivyo inadaiwa kuwa kikosi cha jeshi la zimamoto na uokoaji wamefika mapema zaidi eneo la tukio na askari wake kufanikiwa kupanda hadi juu ya ghorofa hiyo ambako moto huo ulianzia kuwaka ili kujaribu kuzima japo shida kubwa ni mpira wa maji kufika katika eneo hilo.
No comments:
Post a Comment