HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » JENGO LA PPF TOWER LASHIKA MOTO ASUBUHI HII

Habari  kutoka  jijini Dar es Salaam ambazo  zimetua  katika  mtandao huu hivi punde na  kurushwa moja kwa moja na kituo cha radio Nuru Fm 93.5 Mhz  kupitia mwandishi  wetu Dotto Mwaibale  zinadai   kuwa  jengo la PPF TOWER lililopo katikati ya  jiji la Dar es Salaam kwa  sasa  linaendelea kuteketea kwa  moto .

Tukio  hilo  limetokea majira ya saa 1.30 asubuhi  ya leo baada ya  walinzi  wa  jengo hilo  kushuhudia moshi mzito  ukitoka kutoka ndani ya  jengo hilo katika ghorofa  ya mwisho na hivyo kulazimika  kutoa taarifa  vikosi vya zimamoto .

Hata  hivyo  inadaiwa  kuwa  kikosi cha  jeshi la zimamoto na uokoaji  wamefika mapema zaidi  eneo la tukio  na askari  wake  kufanikiwa  kupanda hadi  juu ya ghorofa  hiyo ambako moto huo  ulianzia kuwaka ili kujaribu kuzima japo shida kubwa ni mpira wa maji kufika katika eneo hilo.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: