HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » Wakulima Wa Tumbaku Wakimbia Nyumba Zao


Na John Banda, Manyoni. 

FAMILIA 220 za wanachama wa chama cha Wakulima wa Zao la Tumbaku  wa kijiji cha Msemembo wilayani manyoni mkoani Singida wazimeziacha nyumba zao na kukimbilia mapolini kutokana na Chama cha ushirika cha Msemembo Amcos kuamua kumtumia dalali wa  kampuni ya  Mwankoko Auction Mart Co.LTD ya mjini Singida.
Kukamata mali na nyumba za wakulima hao  kwa madai kuwa wameshindwa kulipa madeni ya mikopo ya fedha katika kipindi cha mwaka 2010/11 walizokopeshwa kwa ajili ya msimu wa kilimo cha zao la tumbaku.
Wakizungumza kwa niaba ya wakulima wezao Wilison Kingo na Shabani Sabuni wasema  kampuni ambayo iliyotumiwa na ushirika huo ni Mwankoko Auction Mart Co.Ltd ya mjini Singida ambayo inashirikiana na viongozi wa ngazi ya juu wa  chama cha ushirika wa
Msemembo Amcos kilichopo kijiji cha Msemembo Wilaya ya Manyoni.
Kingo alisema kutokana kampuni hiyo ya udalali ambayo  waliambatana na Askari wa Jeshi la Polisi waliobeba silaha za moto walipita nyumba hadi nyumba za wanachama na kubadika matangazo yanayowataka wakulima hao kulipa madeni hayo kwa siku 14 zinazoishia Jan 8.2013
“Baada ya kuona kampuni hiyo ya udalali wakiwa na askari wa polisi katika harakati za kuweka matangazo  kwenye nyumba zao, walishikwa na hofu kubwa na kulazimika kukimbilia maporini kwa hofu ya kufilisiwa  nyumba zao na mali”alisema Kingo.
 Wakizungumza zaidi wanachama hao  walisema viongozi hao wametumia mbinu za kuwadharirisha baada ya kungundua kuwepo kwa  ubadhirifu wa fedha miongoni mwa na mali za ushirika  ili kuficha ukweli wa madeni wanayodaiwa na kuamua  kumtumia dalali na polisi kuja kuweka matangazo ya kutaka kufilisi nyumba na mali zao.
Wakulima hao hata hivyo wamesikitishwa na Diwani wa kata hiyo Msemembo Moses Matonya kwa kushindwa kulishughulikia suala hilo lililosababisha wananchi wake kukimbilia maporini ambapo kwa upande wake alimtaka dalali huyo kuhakikisha anakamata nyumba na mali za wanachama hao.
“Diwani huyo amekuwa akimsisitiza dalali wa kampuni hiyo kuhakikisha anakamata mali na nyumba zetu  bila kujali wakulima hao ambao wengi wao wamekimbilia maporini na watoto wengine wakishindwa kwenda shuleni kwa hofu ya kuuzwa nyumba na mali hizo”walisema .
Mapema mwezi wa Desemba  2012 Ofisi ya Mkuu wa wilaya ilipelekewa taarifa kuhusu mgogoro huo kati ya viongozi wa ushirika na wanachama ambapo kwa upande wake aligiza kusitishwa kwa zoezi hilo la dalali la kutaka kukamata nyumba na mali zao.
Kwa mujibu wa barua iliyoandikwa na Katibu Tawala wa Wilaya ya Manyoni Paul Sinje alimtaka Mwenyekiti wa ushirika huo Amos Lameck kufuata mambo yafuatayo yakiwemo ya  kusitisha zoezi hilo,kufanyika kwa mkutano wa wanachama na wakulima wa zao hilo ili kufikia maamuzi ya pamoja.
Aidha Mkuu huyo wa wilaya aliwataka viongozi hao kufuatilia madeni kwa mujibu wa sheria na kanuni walizojiwekea, huku akiagiza Orodha ya wakulima ambao wamelipa  fedha bila ya kupewa risti iwasirishwe kwenye ofisi ya Mkuu wa Wilaya.
“Ofisi ya Wilaya Imebaini makosa uliyofanya katika kufanya kazi hiyo, ita mkutano wa wanachama wote, fuata kanuni na Sheria, Orodha ya waliolipa bila kupewa Risiti iletwe, pia utendaji kazi wa Namna hiyo hautavumiliwa hata kidogo’’. Ilisema sehema ya Barua hiyo ya Tar 3 DES 2012 na Kusainiwa na Afsa Tarafa Paul Sinje
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Ushirika wa Chama cha wakulima wa tumbaku Lameck Amosi alisema kuwa wakulima hao wanadaiwa kiasi cha shilingi zaidi ya million 60 kwa wanachama 108
Alisema kutokana na chama hicho kubanwa na Benki kikitakiwa kulipa deni hilo uongozi wake uliamua kuileta kampuni hiyo ya Udalali ili kuweza kukamata nyumba, mashamba na mali nyingine  ili ziunzwe na kulipa deni hilo lakini siyo kweli wanachama hao hivi sasa wamekimbilia maporini na Barua ya mkuu wa Wilaya.
“Madalali mali nyingi wanapokwenda kufilisi mali ya watedaiwa walio wengi huenda na Polisi kwa ajili ya usalama hivyo uongozi wa ushirika hauhusiki na ujio wa polisi hao na hata Barua ya kuitisha mkutano siyo kweli”, alisema Amosi katika mahojiano kwa njia ya simu.
Mwisho.

HABARI KWA HISANI YA JOHN BANDA

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: