Shughuli ya kuhesabu kura
Siku nne baada ya kupiga kura wakenya wangali kujua mshindi, wa urais,
baadhi ya yaliyojitokeza hadi sasa ni pamoja na malalamishi ya muungano
wa CORD wake Raila Odinga kutaka tume ya uchaguzi kusitisha shughuli ya
kuhesabu kura wakidai kufanyika udanganyifu.
Nayo tume ya uchaguzi yasema idadi
kubwa ya kura zilizoharibika ilitokana na hitilafu katika mtambo wake
ambao ulikuwa unaongeza idadi ya kura hizo mara nane
Hadi kufikia sasa Uhuru Kenyatta ana kura 5,004,406 Raila Odinga ana kura 4,442,923
Wakenya wakiwa katika kipindi kigumu na cha
wasiwasi kwani imechukua Tume ya Uchaguzi muda wa siku nne tangu kuanza
shughuli ya kuhesabu kura na bado mshindi hajajulikana.
Kumekuwa na kila aina ya matukio katika muda huo
wote. Tayari mashirika ya kijamii yameitaka mahakama kusitisha shughuli
inayoendelea ya kuhesabu kura inayofanywa na tume ya uchaguzi.Muungano
wa CORD unaoongozwa na tume ya uchaguzi, umelalamika ukisema shughuli
hiyo ina mizengwe na wanataka ianzishwe upya.
Tupe maoni yako kwenye ukurasa wetu wa
Bofya
Facebook kuhusu yanayojiri Kenya na tutauweka ujumbe wako kwenye mtandao wetu
Bofya
bbcswahili.com
16:10 Mwandisi wa BBC Ann Mawathe
ambaye yuko mjini Kisumu ngome ya Raila Odinga anasema kuna hali ya
utulivu watu wameanza kurejea kazini na ingawa bei ya bidhaa imeanza
kuwa ghali kutokana na wafanyabiashara kuwa na hofu kwenda maeneo jirani
kununua vyakula hadi matokeo yatakapotangazwa.
15:55 Hadi sasa Uhuru Kenyatta ana kura 5,115,704 huku Raila Odinga akiwa na kura 4,513,223. Zaidi ya kura milioni kumi zimehesabiwa huku matokeo yakitarajiwa kutoka maeneo bunge mangine chini ya thelathini
15:49Nyora Wahome kwenye ukurasa wa
Bofya
facebook anasema amechoka kusubiri kwani amengoja saana
15:40Dennis Tsunami Mbaka anasema kupitia
Bofya
facebook mataraiio ya wakenya ni mengi na licha ya kuzuka
mambo mengi wakati huu wa uchaguzi hususan matokeo ya uchaguzi wa urais
yakisubiriwa, anachotaka ni mchakato mzima kukamilika bila tashwishi na
anaitakia nchi yake mustakabali mwema
15:32 Kuhusu kesi ambayo mashirika ya kijamii
yameishtaki tume ya uchaguzi na kuitaka ikomeshe shughuli inayoendelea
ya kuhesabu kura za urais, ni mapema mno kwa hilo. Duru za kisheria
zinasema kuwa kesi hiyo ina misingi duni kwani wanapaswa kusubiri
matokeo rasmi ya uchaguzi kutangazwa ndiposa waende mahakamani
15:25 Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Isaack Hassan anatarajiwa kuhutubia waandishi wa habari wakati wowote kuanzia sasa
15:21Hanif Mohammed akiwa mjini Mombasa ameandika kwenye ukurasa
Bofya
facebook akizungumzia matokeo ya uchaguzi kwa sasa ya
wagombea wakuu kuwa wanakanganywa na hesabu ya kura hizi ila anachoomba
tu ni kuwepo amani
15:14 Sebastian Sabato kwenye ukurasa wa
Bofya
facebook anasema, ijapokuwa ninasubiri matokeo kwa hamu na gamu, kwa upande mwingine shughuli zangu zinaendelea kama kawaida.
BBC SWAHILI
BBC SWAHILI



No comments:
Post a Comment