HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » UHURU KENYATTA ASHINDA KITI CHA URAIS KENYA

Rais mteule wa Kenya Uhuru Kenyatta


Uhuru Kenyatta na mgombea mwenza wake William Ruto

Wafuasi wa Uhuru Kenyatta walijitokza mapema kusherehekea ushindi wa mgombea wao Uhuru Kenyatta katika eneo bunge la Gatundu(Picha na BBC Swahili)

 MTOTO wa Rais wa kwanza wa Kenya, Marehemu Rais Jomo Kenyatta, ambaye alikuwa anagombea Urais kwa tiketi ya Chama cha TNA, Uhuru Kenyata ameshinda nafasi hiyo baada ya kumwangusha mpinzani wake Raila Odinga.
Mchuano  ulikuwa  mkali  kweli  kweli, lakini  hatimaye  Uhuru Kenyatta ameibuka  mshindi wa  kinyang'anyiri  hicho  kwa  asilimia  50.3  ya  kura  zote  zilizopigwa  huku  Raila Odinga  akijipatia  asilimia 43.28  ya  kura zote

Hadi saa 8:35 usiku wa leo Uhuru alikuwa mbele kwa kura 6,173,433 dhidi ya mpinzani wake Raila Odinga aliyekuwa na kura 5, 340,546 ikiwa ni tofauti ya kura 832,887 na majimbo yaliyo kwisha kutangazwa ni 291/291.

Jumla ya kura zote zilizopigwa na kuhesabiwa  kwa nafasi ya Urais ni kura 12,338, 667 kutoka katika majimbo yote ya Uchaguzi 291 huku kura zilizoharibika zikiwa 108975 na kura halali zikibaki 12,222,980.

Katika kinyang’anyiro hicho Wycliffe Musalia Mudavadi anashika nafasi ya tatu akiwa amejikusanyia kura  483,981 nafasi ya nne ikienda kwa Peter Kenneth mwenye kura 72,786.

Mgombea wa Alliance for Real Change,Mohamud Abduba Dida anashika nafasi ya tano akiwa na kura  52,848 akifuatiwa na Mwana mama Martha Karua wa National Rainbow Coalition mwenye kura 43,881 hadi sasa.
Nafasi ya saba katika wagombea hao Urais inakwenda kwa James ole Kiyiapi wa Chama cha Restore and Build Kenya ambaye ana kura 40,998 huku nafasi ya ya nane na mwisho ikishikwa na Paul Kibugi Muite wa chama cha Safina.
Matokeo hayo yatatangazwa rasmi leo saa 11  asubuhi.
Na Francis Godwin

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: