Mwili wa Hugo Chavez ukiwa umewekwa kwenye jeneza kwa ajiri ya kuagwa kabla ya mazishi (1954 - 2013)
Rais
wa Argentina Cristina Fernandez,kushoto , Makamu wa Rais wa Venezuela
Nicolas Maduro, wapili kushoto, Rais wa Uruguay Jose Mujica,watatu
kushotot, Rais wa Bolivia Evo Morales,wa nne kushoto,na mke wa Rais wa
Uruguayan and Mujica's wife, Uruguaya Senator Lucía Topolansky wa
kwanza kulia wakiwa mbele ya jenela lililobeba mwili wa rais Hugo Chavez
Rais wa Cuba Raul Castro akimfariji mtoto wa Marehemu Rosa Virginia Chavez
Rais wa Iran Mahmoud Ahmadinejad akiongea na waandishi wa habari baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa Caracas
Rais wa Cuba Raul Castro (katikati) akitoa heshima kwa mwili pembeni yake ni mtoto wa Rais Hugo Chaves (Rosa Virginia Chavez) na Makamu wa Rais wa Venezuela Nicolas Maduro
Rais
wa Brazil Dilma Rousseff, na Rais wa zamani wa Brazil Luiz Inacio
Lula Da Silva wakitoa heshima zao kwa mwili wa Rais Hugo Chavesof
Venezuela's late President Hugo Chavez.
Mishumaa imewashwa katika uwanja wa Simon Bolivar huko Sabaneta katika mji aliozaliwa Rais Hugo Chavez
Rais wa Ecuador Rafael Correa, kushoto wakiwa na mkewe Anne Malherbe, wakitoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa Rais Hugo Chavez
Kaka
wa Rais Hugo Chavez Adan wa kwanza kushoto, Mama wa Rais Hugo Chavez
Elena Frias wa tatu kushoto, Baba wa Rais Hugo Chavez Hugo wa pili kulia wakiwa mbele
ya Jeneza
..................................
Watu wa rika zote wapata nafasi ya kutoa heshima kwa mwili wa Rais Hugo Chavez
Watu walipoteza fahamu baada ya kutizama mwili wa Hugo Chavez
Picha kwa hisani ya - EPA, AP, AFP/ Getty Image,Guardian.co.uk, miamiherald.com, abc.net.
.........................................
Serikali ya Venezuela imetangaza siku saba zaidi za maombolezi kabla
ya kufanyika maziko ya marehemu rais wa nchi Hito Hugo Chavez baadaye
leo.Serikali hiyo imeongeza muda wa maombolezi kufuatia kufurika zaidi watu wanaotaka kutoa heshima zao za mwisho kwa marehemu.
Makamu wa rais , Nicolas Maduro, amesema kuwa mwili wa bwana Chavez
utakaushwa na baadae kuwekwa ndani ya kaburi la vioo ambapo utakuwa
ukionekana.
Amesema kuwa serikali imeamua kuchelewesha
uamuzi wa mazishi yake kwasababu zaidi ya raia milioni mbili wamekuwa
wakipanga mstari kwa saa nyingi kwa ajili ya kupokea jeneza la chavez
linalopita.
Maafisa wanasema kuwa bwana Maduro ataapiishwa kama rais wa mpito baadaye leo na uchaguzi kufanyika baadaye. Hugo Chavez, aliyeongoza Venezuela kwa miaka 14, alifariki baada ya kuugua Saratani kwa zaidi ya miaka miwili. Zaidi ya viongozi 30 kutoka nchi mbali mbali
wanatarajiwa kuhudhuria mazishi ya Chavez baadaye leo akiwemo rais wa
Iran,Mahmoud Ahmadinejad, rais wa Cuba Raul Castro na rais wa Belarus
Alexander Lukashenko.
Rais Ahmadinejad amemsifu Chavez kama mpigania haki na kiongozi mwenye kuleta mageuzi. Wabune wawili wa bunge la Congress la Marekani
watawakilisha nchi hiyo katika mazishi haya ikikumbukwa kuwa Chavez
alikuwa mkosoaji mkubwa wa Marekani.
BBC SWAHILI




















No comments:
Post a Comment