Mkuu wa wilaya ya Mbozi mkoani Mbeya Dr. Michael
Kadege akiongea na wanakijiji cha Mlowo Mbozi
Baadhi ya wanakijiji wa Mlowo
wakimsikiliza mkuu wa wilaya hiyo
Wanausalama wakiwa makini kwa lolote
litakalotokea
Mwanasheria wa halmashauri ya Mbozi akifafanua
moja ya sheria za halmashauri hiyo
Kauli hii ndio ilileta taflani “yeyote
atakaezomea namtupa ndani” hapa ndipo hali ya hewa ilichafuka kwa wanakijiji wa
Mlowo kumsikia mkuu wilaya akitamka hivyo.
Moja ya wanakijiji akimfuata
mkuu huyo kumpokonya kiongeleo yaani kazi kubwa
Baadhi ya wanakijiji hicho cha
Mlowo wakitulizwa na baadhi ya viongozi wa kijiji hicho wapunguze jazba
Wanakijiji wakiondoka kwenye mkutano bila kufikia muhafaka wa jambo lao baada ya kutoelewana na Mkuu wa wilaya
Mkuu wa wilaya akishauriana na
moja ya wanakamati ya ulinzi na usalama maana maelewano hakuna tena
kwenye mkutano huo
Wakuu wakiondoka baada ya mkutano kuvunjika
Kwa ujumla jeshi la polisi
linabebeshwa mzigo ambao sio wake matatizo waanzishe wengine kuja
kutuliza wengine enyi mnaoanzisha matatizo jaribuni kuyamaliza wenyewe maana
hapo mabomu yangepigwa lawama ingekuwa kwa jeshi la polisi
Wanausalama wakiondoka katika
mkutano uliovunjika ( Picha na Mbeya Yetu)
Mkuu wa wilaya ya
Mbozi mkoani Mbeya Dr. Michael Kadege amejikuta kwenye hali ngumu baada ya wananchi
wa kijiji cha Mlowo kumzomea na kuvuruga mkutano wa kijiji ambao ulikuwa na madhumuni ya kutatua mgogoro
uliodumu kwa mwaka mmoja baina ya kijiji hicho na halmashauri ya wilaya
kuhusiana na makusanyo ya ushuru kwa wafanya biashara.
Aidha wananchi hao
wamepinga kitendo cha mkuu wa wilaya kumsimamisha mwenyekiti wa kijiji bwana
Daud Katule kwa tuhuma za ubadhilifu wa fedha za kijiji , kutosoma mapato na matumizi
pia kuchapisha vitabu vya kukusanya pesa na kutowasilisha fedha katika ofisi ya
almashauri.
Kadege amesema sababu
hizo ndizo zilimpelekea kumsimamisha uongozi bwana Katule na kwamba aliitwa
kwenye kamati ya siasa ya chama cha mapinduzi na halmashauri ya wilaya ambapo imedaiwa kuwa alikiri kufuja pesa hizo
na kuahidi atazirejesha lakini hakutekeleza hali iliypolekea kusimamishwa
uongozi tangu Januari 2013.Kufuatia mvutano huo wananchi walifunga ofisi ya
kijiji mwanzoni mwa wiki hii kushinikiza serikali kutatua mgogoro huo.
Mkuu wa wilaya
ameagiza ofisi ifunguliwe mara moja ili shughuli za serikali ziendelee kama
kawaida ambapo ofisi ilifunguliwa saa 10. 00 chini ya mtendaji kata Jackson
Mwana na mtendaji kijiji Judhith mtega.
Hata hivyo mkutano
huo ulidhibitiwa na jeshi la polisi kwa kushirikiana na kamati ya ulinzi na
usalama ya wilaya ambapo wananchi wamebaki hewani kwa kushindwa kutatuliwa
mgogoro huo.



No comments:
Post a Comment