MFANYABIASHARA AFARIKI KWA KUPIGWA RISASI JIJINI DAR ES SALAAM

542239_526484784032714_436209060_n Mfanyabiashara wa jijini Dar es salaam anayejulikana kwa jina la Ayoub Mlay ameuwawa kwa kupigwa risasi usiku wa kuamkia leo  katika klabu ya  AMBROSIA CLUB iliyoko Kunduchi jijini Dar es salaam.
Kamanda wa polisi mkoa wa Kinondoni Charles Kenyela ameithibitishia Fullshangweblog  kwa njia ya simu, kutokea kwa tukio hilo , huku akisema uchunguzi zaidi unaendelea kujua chanzo cha kupigwa risasi kwa mfanya biashara huyo
Kamanda Kenyela ameongeza kwamba watu hao walikuwa wakinywa ndipo mojawapo alipochukua bastola yake na kumpiga mwezake Ayoub Mlayambaye alifariki usiku wa kuamkia leo

No comments

Powered by Blogger.