HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » MKUU WA MKOA WA GEITA ATANGAZA KUJITOLEA KUWA BALOZI WA KAMPENI YA FISTULA KUMALIZA TATIZO HILO IFIKAPO 2016


Mkuu wa Mkoa wa Geita, Bw. Said Mgalula, akimkabidhi kipaza sauti Balozi wa Chapa Vodacom, Msanii Mwana FA, ili awashushie mistari wakazi wa mji huo waliojitokeza kwenye kampeni ya uelimishaji jamii kuhusu fistula na kwamba matibabu yake yanapatikana bila malipo kwenye hospitali ya CCBRT kwa gharama za Vodacom na Vodafone ya Uingereza.
Mkuu wa Mkoa wa Geita akiteta jambo na MwanaFA kwenye kampeni ya Fistula Inatibika

Balozi wa Chapa Vodacom, Mwana FA, akiwahamasisha wakazi wa Geita kuunga mkono kampeni ya kumaliza tatizo la fistula ifikapo mwaka 2016 inayofadhiliwa na Vodacom na Vodafone ya Uingereza kupitia hospitali ya CCBRT.
Balozi wa Chapa Vodacom, Msanii Mwana FA, akichana mistari mbele ya wakazi wa Mji wa Geita waliofika katika kampeni ya uelimishaji umma kuhusu fistula na kusambaza ujumbe wa 'fistula inatibika, jitokeze upate matibabu bila ua malipo'. Mwana FA yupo kwenye msafara wa kueneza ujumbe huo kwa mikoa ya Kagera, Geita, Shinyanga, Singida, Dodoma, Morogoro na Pwani kwa ufadhili wa Vodacom.
Meneja wa Vodacom Mwanza, Victoria na mwenzake wa Misungwi, Gift wakihifadhi nambari maalum ya kupiga bure 0800752227 kwa masuala yoyote yanayohusu fistula baada ya kutangazwa kwenye kampeni ya kuwaelimsisha wakazi wa mji wa Geita kuelekea kilele cha siku ya fistula duniani Mei 23. Nambari hiyo ni kwa wateja wa Vodacom pekee.Vodacom na Vodafone ya Uingereza hugharamia matibabu bila malipo kwa wagonjwa wote wa fistula wanaoitibiwa katika hospitali ya CCBRT.
Muuguzi na Mnasihi wa CCBRT, Theodola Millinga, akielimisha wakazi wa Geita kuhusu fistula na namna ya kupata matibabu yake bila malipo kwenye hospitali ya CCBRT kupitia ufadhili wa Vodacom na Vodafone ya Uingereza. Zoezi hilo ni sehemu ya kampeni ya kusambaza ujumbe wa 'Fistula inatibika, jitokeze upate matibabu bila ya malipo' inayondelea mikoani kwa ufadhili wa Vodacom na Vodafone ikishirikiana na CCBRT.
Mkazi wa Geita (kushoto), akiuliza swali kuhusu fistula wakati wa kampeni ya kufikisha ujumbe wa Fistula inatibika jitokeza upate matibabu bila ya malipo kwenye hospitali ya CCBRT kwa ufadhili wa Vodacom na Vodafone ya Uingereza. Zoezi hilo ni sehemu ya kampeni ya kusambaza ujumbe kuhusu fistula inayoendelea mikoani kwa ufadhili wa Vodacom na Vodafone ikishirikiana na CCBRT kuelekea siku ya fistula duniani Mei 23.
Mkuu wa Mkoa wa Geira Said Magalula (katikati), Balozi wa Chapa Vodacom Mwana FA na Meneja Uhusiano wa Mambo ya nje wa Vodacom, Salum Mwalim wakifurahia moja ya tukio wakati wa kampeni ya kuelimisha wakazi wa Geita kuhusu fistula na kufikisha ujumbe wa 'Fistula inatibika, jitokeze upate matibabu bila ya malipo' iliyoendeshwa mjini Geita ikiwa ni sehemu ya shughuli za kuelekea siku ya fistula duniani Mei 23. Vodacom na Vodafone hufadhili matibabu kwa wanawake wenye fistula kwenye hospitali ya CCBRT.
Shuhuda wa fistula akitoa ushuhuda wa jinsi alivyoteseka na fistula kwa mika minne kabla ya Vodacom kufadhili matibabu yake kwenye hospitali ya CCBRT. Ushuhuda huo ulitolewa wakati wa kampeni ya kuelimisha wakazi wa Geita kuhusu fistula na kufikisha ujumbe wa 'Fistula inatibika jitokeza upate matibabu bila ya malipo'.

 Mkuu wa Mkoa wa Geita akizungumza na wananchi wake kwenye kampeni ya Fistula Inatibika
 Mkuu wa Mkoa wa Geita pamoja na timu nzima inayoshiriki katika msafara wa Fistula Inatibika


Kampeni ya Fistula inatibika inaendelea kutoka Geita kuelekea Singida kupitia Sengerema kwa kutumia kivuko cha MV Misungwi
.............................................
Geita yaguswa na kampeni ya fistula
Katika kuelekea kuadhimisha siku ya Fistula Duniani, 23/5/2013, Vodacom kwa kushirikiana na taasisi ys CCBRT wameandaa safari ya kuzunguka nchi nzima inayofahamika kama ‘Fistula Inatibika’ kutokea Bukoba hadi Dar es Salaam kwenye kilele cha maadhimisho ya siku hiyo kwenye viwanja vya CCBRT yatakayopokelewa na Rais Jakaya Kikwete.

Safari hiyo ambayo inahusisha pia kupita kwenye sehemu mbalimbali kuwapa wananchi ujumbe kuwa Fistula inatibika, itajumuisha pia kukusanya ujumbe kutoka kwa familia zilizoathirika na Fistula kupeleka kwa Rais hapo tarehe 23 ya mwezi huu.
Msafara huo utakaochukua jumla ya siku saba, unaongozwa na mwanamuziki wa kizazi kipya, Hamis Mwinjuma maarufu kama Mwana FA, ambaye atakuwa akiwapa elimu kuhusiana na Fistula wananchi wa sehemu tofauti tofauti watakaopitiwa na msafara huo.


Picha: Msafara wa Fistula ukiwa Geita

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: