Mwanafunzi wa chuo kikuu cha Dodoma
anayejulikana kwa jina la Boid Mwakitalima amefariki dunia baada
kugongwa na treni na pia wanafunzi huyo alikuwa mwaka wa tatu.
Taarifa zinaeleza kuwa, mwanafunzi huyo alikuwa anatembea pembezoni mwa reli huku akiwa ameweka "headphone" sikioni, hali iliyomfanya ashindwe kusikia ama kuhisi chochote juu ya muungurumo wa treni hilo mpaka lilipomsogelea karibu na kumsukuma pembeni ambapo aliangukia chuma na kuaga dunia pale pale.
Jeneza lililobeba mwili wa Boid Mwakitalimalikitolewa kwenye ambulance ya chuo kikuu cha Dodoma
Makamu Mkuu wa Chuo kikuu cha Dodoma Prof.Idrisa Kikula akiwasili Collage ya Informatics
Prof. Idrisa Kikula akipokelea kwenye msiba wa mwanafunzi wa Colllage ya Informatics kwa ajiri ya kuuaga mwili wa marehemu
Baadhi ya viongozi wa Chuo kikuu cha Dodoma wakienda kuaga mwili wa marehemu katikakati ni Prof. Idrisa Kikula, mbele ni Mshauri wa wanafunzi ( Dean of Student) Chuo kikuu cha Dodoma, Nyuma ni mshauri wa wanafunzi, Pro.Anatory ( Dean of Students) Collage ya Informatics na Katikati ni Makamu mkuu wa chuo cha Dodoma.
Baada ya ajali hiyo,
mwanafunzi huyo alipelekwa chumba cha kuhifadhia maiti katika
hospitali ya Mkoa wa Domoma, "General hospital" ambapo leo hii
ameagwa na wanafunzi wenzake wa chuo kikuu cha Dodoma na
kusafirishwa kwenda nyumbani kwao Mbeya kwa mazishi.
Wanachuo wakipokezana jeneza lililokuwa limeubeba mwili wa marehemu Boid Mwakitalima kuonesha upendo kwa mwanachuo mwenzao
Wanafunzi wakiuaga mwili wa marehemu kwa huzuni
Baadhi ya wanafunzi waliofika kuaga mwili wa marehemu Boid Mwakitalima
Mkuu wa Collage ya Informatics, Prof. Mvuma, akitoa nasaha zake
Rais wa wanafunzi, Collage ya Informatics akitoa nasaha zake
No comments:
Post a Comment