Mahakama hiyo imeamuru Mubarak kuachiliwa huru kutokana na mashitaka ya rushwa yaliyokuwa yanamkabili.
Lakini bado haijajulikana kama ataachiliwa baadaye jumatano ya leo.
Upande wa mashitaka unatarajiwa kukata rufaa.
Kiongozi huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 85
anakabiliwa pia na kesi ya kushiriki kwenye mauwaji ya malefu ya raia
walioandamana kwenye vuguvugu la mapinduzi lililomtoa madarakani mwaka
2011.
Alifungwa kifungo cha maisha jela mwaka jana, lakini alikata rufaa na kushinda na kesi yake kutakiwa kusikilizwa upya.
BBC SWAHILI
No comments:
Post a Comment