Chama
cha Majaji Wanawake Tanzania (Tawja) kimesema rushwa ya ngono bado ni
tatizo kubwa ambalo limeshamiri katika ofisi nyingi hapa nchini.Mwenyekiti wa chama hicho, Angela Kileo alisema hayo jijini Dar es Salaam jana wakati wa warsha ya wadau wa utoaji haki na utokomezaji wa matumizi mabaya ya madaraka yanayoambatana na rushwa ya ngono.
Alisema baadhi ya waajiri wamekuwa wakitumia madaraka yao vibaya
kuomba rushwa ya ngono na kuahidi kutoa ajira, kupandisha cheo, au
kuongeza posho.
Alisema waathirika wakubwa wa tatizo hilo ni wanawake maofisini, viwandani, mashuleni, vyuoni, majumbani na sehemu nyingine za uzalishaji na utoaji huduma.
Alisema vitendo hivyo vimekuwa vikifanyika kwa usiri mkubwa na kwamba licha ya kuwadhalilisha wanawake, lakini pia vinawaathiri kimwili na kisaikolojia.
Kileo aliongeza kuwa, licha ya athari zinazowapata kutokana na tatizo hilo, lakini wengi wao huogopa kuripoti katika vyombo husika kwa kuhofia kupoteza ajira.
Alisema waathirika wakubwa wa tatizo hilo ni wanawake maofisini, viwandani, mashuleni, vyuoni, majumbani na sehemu nyingine za uzalishaji na utoaji huduma.
Alisema vitendo hivyo vimekuwa vikifanyika kwa usiri mkubwa na kwamba licha ya kuwadhalilisha wanawake, lakini pia vinawaathiri kimwili na kisaikolojia.
Kileo aliongeza kuwa, licha ya athari zinazowapata kutokana na tatizo hilo, lakini wengi wao huogopa kuripoti katika vyombo husika kwa kuhofia kupoteza ajira.
Alisema kutokana na tatizo hilo kuwa kubwa, kuna kila sababu ya
kuangalia kuboresha sheria ili kuwalinda wanawake, pamoja na jamii
kushirikiana katika kutokomeza tatizo hilo.
CHANZO:
NIPASHE



No comments:
Post a Comment