UPDATES: JULIUS NYAISANGA MTANGAZAJI MKONGWE WA TANZANIA AFARIKI DUNIA

 
Mtandao huu umepata taarifa za kushtua katika tasnia ya habari na utangazaji kutokana na habari za kifo cha Mtangazaji mkongwe nchini Tanzania, Julius Nyaisanga, aliyekuwa mfanyakazi wa Abood Media mjini Morogoro.
Habari kutoka kwa mfanyakazi wa redio hiyo ambaye pia hakupenda kutaja jina lake moja kwa moja kwakuwa sio msemaji wa familia wala redio hiyo zilisema kuwa Nyaisanga maarufu kama Uncle J amefariki.
 
Taaarifa zaidi za msiba huo zinaendelea kusakwa hasa kutoka kwa Chama Cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Morogoro, pamoja na familia yake.

No comments

Powered by Blogger.