HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » BREAKING NEWS: WAZIRI MKUU PINDA AMESEMA KWAMBA RAIS KIKWETE AMEKUBALI KUTENGUA NYADHIFA ZA MAWAZIRI WANNE KUFUATIA RIPOTI YA 'OPERESHENI TOKOMEZA'

 
Waziri Mkuu wa Tanzania Mizengo Pinda amesema kwamba Rais Kikwete amekubali kutengua nyadhifa za mawaziri wanne kufuatia ripoti ya 'Operesheni Tokomeza' iliyotolewa mapema leo bungeni.
 Waziri mkuu anaongea kwa kujumuhisha kwa mawaziri waliosalia na anaanza kwa kauli zake za kuzunguuuka na kuomba radhi kwa waliotendwa na operation tokomeza. Anachojaribu kusema kama serikali wanatafakari na watafanyia kazi kama serikali kwani operationi ilikuwa chini ya wizara tatu. Na anaendelea kutazama na kuangalia na anapendekeza iundwe tume ya kuthibitisha hayo kama alivyoshauri Mwanasheria mkuu wa serikali.

 Mawaziri hao waliotenguliwa nyadhifa zao ni: Mhe. David Mathayo David wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Balozi Khamis Kagasheki wa Maliasili na Utalii, Mhe. Emmanuel Nchimbi wa Mambo ya Ndani na Mhe. Shamsi Vuai Nahodha wa Ulinzi. Mhe. Kagasheki alitangaza kujiuzulu mapema kabla uamuzi huo uliotangazwa na Waziri Mkuu
 

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: