Mamlaka ya
Bandari Tanzania kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii
pamoja na vyombo vingine vya Dola, tarehe 2 Januari 2014 majira ya saa
tatu asubuhi kwenye Bandari ya Dar es Salaam, imekamata meno 81 ya tembo
yenye uzito wa kilo 303 sawa na tembo 41. Aidha, magamba 120 ya
kakakuona na mazao ya bahari nayo yamekamtwa.
Hii ni baada ya Askari wa Bandari kutilia shaka mizigo iliyokuwa kwenye gari ikiingizwa bandarini. Meno ya tembo yaliyokamatwa bado ni mapya ikiwa na maana tembo hao wameuawa katika kipindi kizichozidi mwezi mmoja uliopita.
Wizara inasikitishwa sana na vitendo hivi viovu vya ujangili ambavyo vimetokea ndani ya muda mfupi. Tayari watuhumiwa wawili wanashikiliwa na Polisi kufuatia tukio hilo. Majina yao yanahifadhiwa kwa lengo la kutovuruga upelelezi.
Serikali inasisitiza tena kwamba imejizatiti kupambana na vitendo vya ujangili katika mapori yote na maeneo yote ya mipaka ya nchi yetu. Pia, Serikali inapanua wigo wa upelelezi kuhakikisha wote waliohusika wanapatikana na kufikishwa katika vyombo vya sheria.
Hii ni baada ya Askari wa Bandari kutilia shaka mizigo iliyokuwa kwenye gari ikiingizwa bandarini. Meno ya tembo yaliyokamatwa bado ni mapya ikiwa na maana tembo hao wameuawa katika kipindi kizichozidi mwezi mmoja uliopita.
Wizara inasikitishwa sana na vitendo hivi viovu vya ujangili ambavyo vimetokea ndani ya muda mfupi. Tayari watuhumiwa wawili wanashikiliwa na Polisi kufuatia tukio hilo. Majina yao yanahifadhiwa kwa lengo la kutovuruga upelelezi.
Serikali inasisitiza tena kwamba imejizatiti kupambana na vitendo vya ujangili katika mapori yote na maeneo yote ya mipaka ya nchi yetu. Pia, Serikali inapanua wigo wa upelelezi kuhakikisha wote waliohusika wanapatikana na kufikishwa katika vyombo vya sheria.
Imetolewa na:
Chikambi K. Rumisha
Msemaji wa Wizara ya Maliasili na Utalii
Januari 2, 2014
Chikambi K. Rumisha
Msemaji wa Wizara ya Maliasili na Utalii
Januari 2, 2014




No comments:
Post a Comment