VIJANA WAWILI WAPIGWA BAADA YA KUSEMEKANA WAMEMWIBIA MDADA ENEO LA KIJITONYAMA JIJINI DAR



 Jamaa wawili wanaotuhumiwa kuwa wezi, nusura wauawe kwa kuchomwa moto na raia wenye hasira kali baada ya kula kichapo ‘hevi’ kwa msala wa kukwapua mkoba wa mrembo aliyekuwa ndani ya Bajaj.
 Alisema baada ya kupora mkoba huo walianza kutoka nduki lakini kabla hawajafika mbali, mtu mmoja aliyekuwa na gari, ambaye pia aliona tukio hilo, aliziba njia na kuwafanya vijana hao kutumbukia mtaroni. 

ENDELEA KUSOMA HABARI HII KWA KUBOFYA HAPA CHINI



Katika tukio hilo lililojiri maeneo ya Kijitonyama, Dar, mwanzoni mwa wiki hii, shuhuda aliyeona alisema aliwaona vijana hao wakiwa wamepanda pikipiki wakipora mkoba wa mrembi huyo aliyejitambulisha kwa jina la Magdalena John (21).Msichana huyo alishuka ndani ya Bajaj na kuanza kuwapigia kelele za wizi hivyo kuwafanya wapita njia kuanza kuwapiga kwa kutumia silaha mbalimbali zikiwemo mawe, fimbo na matofali. Waandishi wa habari hii waliowahi kufika eneo la tukio, waliwashuhudia watu hao wakipokea kipigo kikali kilichowafanya wawe hoi.

No comments

Powered by Blogger.