Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweha saini kitabu cha maombolezo
alipokwenda kuhani msiba wa Askari wa Usalama Barabarani aliyegongwa na gari
baada ya msafara wa Rais kupita jana WP 2942 Koplo Elikiza nyumbani kwa
marehemu sehemu za Ununio (Picha na Ikulu)
Rais
Jakaya Mrisho Kikwete akiwafariji mume wa marehemu na watoto pamoja na
IGP Saidi Mwema alipokwenda kuhani msiba wa Askari wa Usalama Barabarani
aliyegongwa na gari baada ya msafara wa Rais kupita jana WP Koplo
Elikiza nyumbani kwa marehemu sehemu za Ununio
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpa mkono wa pole mume wa
marehemu alipokwenda kuhani msiba wa Askari wa Usalama Barabarani aliyegongwa
na gari baada ya msafara wa Rais kupita jana WP Koplo Elikiza nyumbani kwa
marehemu sehemu za Ununio

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib
Bilal, akiweka saini katika kitabu cha maombolezo ya msiba wa aliyekuwa
askari wa Usalama Barabarani, WP Elikizaeli Lokisa Nnko, aliyefariki
dunia kwa kugongwa na gari na dereva ambaye hadi sasa hajajulikana
wakati akiwa katika majukumu yake ya kikazi eneo la Bamaga Mwenge jijini
Dar es Salaam jana.Picha na Ofisi ya Makamu Wa Raisi

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib
Bilal, akimfariji Prince David, mtoto wa aliyekuwa askari wa Usalama
Barabarani, marehemu WP Elikizaeli Lokisa Nnko, aliyefariki dunia kwa
kugongwa na gari na dereva ambaye hadi sasa hajajulikana wakati akiwa
katika majukumu yake ya kikazi eneo la Bamaga Mwenge jijini Dar es
Salaam jana.

Kutoka (kulia) ni Mume wa Marehemu, David Erasto Luharara, watoto wa
marehemu, Prince David na Abdulhaman David, wakiwa na huzuni.


Baadhi ya waombolezaji wakiwa nyumbani kwa marehemu kuomboleza msiba huo.





No comments:
Post a Comment