Rais Jakaya Mrisho Kikwete
akiwa na Bibi yake Rais wa Marekani, Mh. Barack Obama, Mama Sarah Obama
walipokutana leo kwenye hoteli ya Villa Rosa Kempiski jijini Nairobi,
Kenya, wakati Rais Kikwete akijiandaa kurejea nchini. Mama Sarah Obama
anatarajia kuzindua taasisi ya kusaidia elimu kijijini Kogelo nchini
Kenya, alikozaliwa Baba yake na Rais Obama wa Marekani itakayofahamika
kama (Sarah Obama foundation) ambapo atajenga shule kuanzia za awali
mpaka sekondari. Rais kikwete sasa hivi yuko mjini Kondoa kuendelea na
ziara yake ya Mkoa wa Dodoma. (PICHA NA IKULU)
-




No comments:
Post a Comment