HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » JESHI LA POLISI LAKAMATA WAGANGA 225 WANAOPIGA RAMLI CHONGANISHI

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Jeshi la Polisi nchini Tanzania limewakamata wapigaramli chonganishi 225 katika mikoa ya mbalimbali ya Tanzania ikiwa ni pamoja na mikoa ya Tabora, Geita, Mwanza, Simiyu, Shinyanga ambapo kati yao 97 tayari wamefikishwa mahakamani kwa makosa mbalimbali ikiwemo kukutwa na vifaa vya uganga ambavyo vingine ni nyara za serikali kama vile ngozi ya Kenge, meno ya Ngiri, mikia ya Tumbili, miguu ya Ndege.

Akiongea leo jijini Dar es Salaam, Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Advera John Bulimba amesema watu hao wamekamatwa kufuatia msako unaoendelea katika mikoa hiyo pamoja na mikoa ya Kagera, Katavi na Rukwa, ambako pia watu hao wamekamatwa na mikia ya nyumbu, ngozi ya Simba, ngozi ya Fisi, ngozi ya Digidigi na wengine kufanya uganga bila kibali.

Advera amesema Jeshi la polisi litaendelea na juhudi za kukomesha matukio ya kihalifu yaliyoibuka hivi karibuni ya kuwaua na kuwajeruhi watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino) kwa visingizio vya imani potofu za ushirikina, katika mikoa yote ili kuhakikisha mtandao mzima unaojihusisha na matukio hayo unakamatwa wakiwemo waganga wa jadi wanaopigaramli chonganishi.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: