HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » PICHA: FLOYD MAYWETHER AMGARAGAZA PACQUIAO KWA POINT

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.

 Bondia wa Marekani Floyd Mayweather ameshinda pigano lililosubiriwa kwa hamu na  na watu wengi ulimwenguni kote. Bondia Floyd Mayweather ameshinda mchezo huo kwa point 118-110, 116-112, 116-112 kutoka kwa waamuzi wa mchezo huo na kunyakuwa mkanda wa WBC huku akiifanya rekodi yake ya kutopigwa kufikia michezo 48.
  Bondia huyo ambaye hajashindwa alimshinda mpinzani wake raia wa Ufilipino Manny Pacquiao kwa wingi wa pointi.
Pambano hili la kihistoria na lililokuwa likisubiriwa kwa hamu na watu wengi Duniani, liliopigwa leo asubuhi kwa muda wa Afrika ya Mashariki kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa MGM Grand Garden Arena, jijini Las Vegas, Marekani.

ENDELEA KUTAZAMA TUKIO HILI KWA KUBOFYA HAPA CHINI

 Mchezo ulikuwa ni mkali sana na Mabondia wote walikuwa wakirushiana makonde kwa zamu.
 Mashabiki wengi waliojaa katika ukumbi wa MGM Grand Garden Arena mjini Las Vegas walimzoma mara kwa mara Mayweather.
 Kote duniani wateja millioni 3 walilipa kuliona pigano hilo ambalo ndio pigano lililovutia kitita kikubwa cha fedha katika historia ya ndondi.
 Bondia Floyd Mayweather akimsikiliza baba yake wakati wa mapumziko 
 Tiketi nyingi za pigano hilo ziliuzwa katika bei ya makumi ya maelfu ya dola.
 
 
 
 
 Mechi ikiendelea
 Referee wa mchezo huo Kenny Bayless akiendelea kuchezesha pambano hilo lililopigwa leo asubuhi kwa muda wa Afrika ya Mashariki kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa MGM Grand Garden Arena, jijini Las Vegas, Marekani
   Bondia Floyd Mayweather  akishangilia ushindi wake baada ya kumchapa mpizani wake aia wa Ufilipino Manny Pacquiao.
 Manny Pacquiao akiwa katika hali ya sintofahamu baada ya pambano kuisha

 Mabondia Manny Pacquiao(kulia) na Floyd Mayweather(kushoto)  wakifurahi pamoja mara baada ya mpambano lao kuisha
 Bondia Floyd Mayweather akishangilia mara baada ya pambano kuisha

Bondia Floyd Mayweather Jr akiwa na mikanda yake na tuzo aliyoshinda katika michezo mbali mbali 

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: