Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla ametoa onyo kali kwa wanataalum wa sekta ya afya kuacha mara moja vitendo vya kupokea na kuomba rushwa kwani endapo watabainika hatua kali zitachukuliwa dhidi yao.
Dk. Kigwangalla emesema hayo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa kuadhimisha siku ya kinywa na meno duniani yaliyofanyika katika viwanja vya shule ya tiba ya kinywa na Meno, Muhimbili.
Ambapo amesema kuwa kwa utawala huu wa sasa Serikali ya awamu ya tano ni dhama nyingine na hawatamvumilia mtu.
“Ninaona tu, bado kuna wachache wanaojihusisha na vitendo vya kuomba rushwa hapa na pale. Kwa dhama hizi ukikutwa hatutakuurumia na hatutamuurumia mtu kwa hili. Tunapaswa kuweka maslai mapana kwa wananchi tunaowahudumia kwenye mioyo yetu” alieleza Dk. Kigwangalla.
Maadhimiho hayo kwa mwaka huu yenye kauli mbiu “Afya njema ya kinywa ni afya ya mwili mzima” kilele chake kinatarajiwa kufikia tamati Mkoani Morogoro ambapo kwa siku zote hizi hadi kilele, Madaktari watatembelea shule maalum kadhaa za ikiwemo ya Mtoni Maalum, Sinza Maalum, Buguruni Maalum na zingine za Mkoa wa Shinyanga na Morogoro ambapo pia watafanya uchunguzi na matibabu ya bure katika siku zote hizo.
Awali katika ufunguzi huo, kulitanguliwa na matembezi maalum ya KM 10, yaliyoongozwa na Naibu Waziri Dk. Kigwangalla ilikuhamasisha afya njema ya kinywa na mwili katika mapambano hayo.
Tazama MO tv, kuona video hiyo hapa:
No comments:
Post a Comment