headlines

HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» » » Viongozi Wawili CHADEMA Wavuliwa Uanachama
VIJIMAMBO

Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema, Patrick Ole Sosopi, ametangaza kuwafuta uanachama wanachama wawili wa chama hicho.

Waliofutwa uanachana ni pamoja na aliyekua Naibu Katibu Mkuu Bara, Getrude Ndibalema na Mwenyekiti wa Bavicha mkoa wa Kilimanjaro, Dickson Kibona.

Akizungumza jana Mei 21, katika mkutano na waandishi wa habari jijini Arusha, Ole Sosopi alisema kwamba uamuzi huo umekuja baada ya kufuata taratibu zote za kuwahoji kupitia tume iliyoundwa.

Alisema viongozi hao wamehojiwa baada ya kuwepo tuhuma za usaliti ambalo ni kosa kubwa kwenye chama hicho.

Sosopi amesema Bavicha imeridhia kuwaondoa wanachama hao baada ya kujiridhisha kwa makosa waliyoyafanya.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: