HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

PICHA: JINSI SHABIKI MAARUFU WA YANGA, ALLY YANGA ALIVYOFARIKI KATIKA AJALI YA GARI

Shabiki wa Yanga maarufu kwa jina la Ally Yanga amefariki dunia jana  katika ajali ya gari. Ally Yanga alijizolea umaarufu mkubwa katika tasnia ya soka kotokana na jinsi alivyokuwa akivaa na kujichora pamoja na namna yake ya ushangiliaji anapokuwa uwanjani.

Ajali hiyo iliyohusika katika kifo cha Ally Yanga iiltokea jana  mkoani Dodoma
Klabu ya Yanga kupitia Idara ya Habari na mawasiliano wametuma salamu za rambirambi kwa ndugu na jamaa wa Ally Yanga kufuatia kifo cha mpendwa wao ambapo wamesema kuwa faraja ya Mungu ikawe na familia hiyo katika kipindi hiki kigumu.

“Uongozi wa Yanga SC umepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Ally Yanga, hakika Mungu ni mwema, faraja ya Mungu wetu ikawe kwa familia katika kipindi chote cha majonzi kwa kuondokewa na mpendwa wao.”
Aidha, kwa upande wao, Yanga wamesema kuwa wameachwa na pengo kubwa kutokana kutokana na kupoteza shabiki na mwanachama huyo maarufu.

“Pia nasi Yanga kifo chake kina acha pengo kubwa kwa nafasi yake ambayo ilipelekea kujipatia umaarufu mkubwa na alikuwa balozi mzuri kama mwanachama na shabiki mkubwa wa timu yetu, Bwana alitoa, Bwana ametwaa.”




AJALI YATOKEA DUMILA MMOJA AFARIKI, JONAS MKUDE ANUSURIKA

NAHODHA wa Mabingwa wa kombe la Shirikisho na Kiungo wa timu hiyo, Jonas Mkude ni miongoni mwa watu waliojeruhiwa katika ajali ya gari walilokuwa wakisafiria kutoka Dodoma kwenda Dar es Salaam. Anaandika Mroki Mroki-Mroki Mroki.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka eneo ilipotokea ajali hiyo, Dumila katika shamba la Mitiki, zinaarifu kuwa hakuna watu wawili ambao bado majina yao hajapatikana wameumia na Mkude kupata majeraha madogo na kupelekwa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa matibabu zaidi.

Watu hao walikuwa katika gari aina ya Toyota VX lenye namba za Usajili T 834BLZ na walikuwa wakitokea Dodoma kushuhudia fainali za kombne la Shirikisho la Soka Tanzania uliopigwa jana katika Uwanja wa Jamhuri Mjini Dodoma uliozikutanisha Simba na Mbao.

Simba ilishinda mchezo huo kwa bao 2-1 na kutwaa ubingwa huo na kujipatoia tiketi ya kushiriki Kombe la Shirikisho Barani Afrika.

WATU WATATU WAFARIKI RUFIJI BAADA YA MTUMBWI WAO KUZAMA

Watu watatu wamefariki dunia kwa kuzama majini na mmoja kunusurika kifo baada ya mtumbwi waliokuwa wakivukia kuzama bwawani wilayani Rufiji mkoani Pwani.
Akithibitisha kutokea kwa vifo hivyo, Ofisa Tarafa ya Ikwiriri, Suleimani Mpangile aliwataja marehemu hao kuwa ni Sijali Abdallah (14), Zuberi Penya (11) wakazi wa Umwe Ikwiriri na Salehe Saidi (31) mkazi wa Dar es Salaam.
Mpangile pia alimtaja aliyenusulika kifo kuwa ni Musa Mkamba ambaye alikuwa akiwavusha marehemu hao.
Alisema chanzo cha vifo hivyo ni mtumbwi waliokuwa wakivukia kujaa maji na kuzama jana Jumamosi saa 3 asubuhi katika bwawa hilo la Umwe.

Wachimbaji wawili wafia ndani ya mgodi

Wachimbaji wawili wa madini katika kijiji cha Masuluti mkoani hapa, Haus Kaijage (32) mkazi wa Bukoba na James Mlawa(22) mkazi wa Magulilwa, Iringa wamefariki dunia baada ya kukosa hewa ndani ya mgodi.
Ofisa mtendaji wa kijiji cha Masuluti, Venjaslaus Kiunosile amesema tukio hilo limetokea leo (Ijumaa) saa tano asubuhi.
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Iringa, Julius Mjengi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba tayari miili ya marehemu imetolewa ndani ya mgodi.
Amesema chanzo cha watu hao kupoteza maisha ni kukosa hewa baada ya kuingiza jenereta la kuvuta maji mgodini kwa lengo la kuvuta maji na baada ya kuliwasha walikosa hewa.
Hata hivyo amesema jeshi la polisi linamshikilia mmiliki wa mgodi huo Samweli Msigwa kwa mahojiano
Mganga mfawidhi wa kituo cha afya cha Mgama, Baraka Mwifune amesema uchunguzi wa awali uliofanywa umeonyesha kuwa watu hao walipoteza maisha kwa kukosa hewa.
Mmiliki wa mgodi huo, Msigwa amesema akiwa njiani kuelekea eneo la mgodi kwa ajili ya kusaidia kutengeneza mashine ya kuingiza hewa katika mgodi huo ndipo alipopata taarifa ya wachimbaji hao wawili kati ya sita kupoteza maisha kwa kukosa hewa.

WANAFUNZI WA LUCKY VICENT WALIOPATA AJALI WAPATA VISA YA KWENDA MAREKANI KWA MATIBABU

Mbunge wa Singida Kaskazini,Lazaro Nyalandu amesema Ubalozi wa Marekani umetoa hati ya kusafiria (visa) kwa ajili ya kuwawezesha wanafunzi watatu wa Shule ya Lucky Vincent kupata matibabu nchini Marekani.
Katika ukurasa wake wa Facebook leo Nyalandu amesema waliopata Visa ni wazazi,watoto na wataalamu wawili wa afya ambao watasafiri kwenda Marekani.
"Wote wamepewa visa asubuhi ya leo Ubalozi wa Marekani Dar es Salaam. Akina Mama watatu, watoto wote watatu, na Daktari Moja na Nurse Moja. Kansela wa Ubalozi wa Marekani alinipigia simu asubuhi akiwasubiri katika siku ambayo haikuwa ya kazi,” amesema Nyalandu na kuongeza:
“Mungu ambariki sana kwa moyo huu. Napenda pia kutoa taarifa kuwa ndege yao aina ya DC 8 inatarajiwa kutua Leo usiku saa 2:15 majira ya Afrika Mashariki katika uwanja wa KIA. Mungu wa Watanzania awabariki wote kwa sala na dua zenu kwa ajili ya hawa watoto. Sifa na utukufu kwa Mungu wetu.”
Katika taarifa ya awali kwa vyombo vya habari Nyalandu amesema safari ya kuelekea Marekani itakua kesho asubuhi na ndege itatua Charlotte,New York na kisha wagonjwa pamoja na waliowasindikiza wataingia katika ndege nyingine maalumu ya kubeba wagonjwa hadi katika mji wa Sioux City,Iowa
Watoto hao watatu walijeruhiwa wakati wakiwa katika safari ya masomo wilayani Karatu mkoa wa Arusha jumamosi iliyopita na kusababisha vifo vya wanafunzi 32,walimu wawili na dereva wao.

TRENI YA ABIRIA YAPATA AJALI MOROGORO

Treni ya abiria imepata ajali usiku saa 5 eneo la Stesheni ya Mazimbu Morogoro ambapo mabehewa manne yameegama na matatu yameacha reli.

Ashura Mrisho aliyekuwa anakwenda Tabora amejeruhiwa kwa kuangukiwa na mizigo. Mabehewa 13 yamerejeshwa Morogoro kuwapangia usafiri mbadala 

WATU WATANO WA FAMILIA MOJA WAFARIKI KWA NYUMBA YAO KUANGUKIWA NA MTI .


 Baadi ya wananchi wakiondoa paa la bai ili kuokoa watu waliokuwa kwenye nyumba iliyoangukiwa na mti usiku wa kuamkia leo

Na,Vero Ignatus,Arusha
Kutokana na  mvua inayonyesha mfululizo Mkoani  Arusha imeleta maafa makubwa katika familia ya mzee Jonathani Kalambiya(55) mkazi wa sokoni II katika kijiji cha kinyeresi wilayani Arumeru Mkoani Arusha baada ya mti mkubwa uliong’olewa na maji kuangukia nyumba yake na kuua watoto wake wote watano.



Mkasa huo wa kusikitisha ulitokea jana majira ya saa 7 usiku baada ya mti huo kung’olewa na maji uliangukia nyumba hiyo iliyokuwa jira na mti huo.



Kamanda wa polisi Mkoani Arusha,Charles Mkumbo alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataja watoto waliokufa katika tukio hilo ni pamoja na watoto wawili wanafunzi wa mzee huyo ambaye ni mlinzi wa hospital ya ya Dr Mohamed ya Jijini Arusha.



Mkumbo aliwataka wanafunzi ambao ni watoto wa mzee Kalambwia ambaye siku ya tukio alikuwa kazini ni pamoja na Miliamu Jonathani(16) mwanafunzi wa kidatu cha pili wa shule ya sekondari ya Inaboishu.

Kamanda alimtaja mwanafunzi mwingine ni ambaye ni mtoto wa mzee huyo ni Grolia Jonathani(11) mwanafunzi wa shule ya msingi Kinyeresi iliyoko wilayani Arumeru Mkoani Arusha.



Amesema watoto wengine wa mzee huyo ni pamoja na mtoto wa kwanza wa mzee huyo aliyetambuliwa kwa jina la Giliad  Jonathani(31),Lazaro Lomnyaki (26) na Best Jonathani(20).



Kamanda Mkumbo alisema kuwa mti huo uliokuwa katika mlima wa Lake mana uliangukia nyumba hiyo baada ya kung’olewa na mvua kubwa inayoendelea kunyesha katika Jiji la Arusha na Mkoa kwa ujumla.



Alisema na kuitakia pole sana familia yam zee huyo kwani tukio hilo ni majonzi makubwa sana kwake kwani familia nzima imeondoka na kumtaka kuwa na uvumilivu katika wakati huu mgumu kwake.



Kamanda Mkumbo ametoa wito na ushauri kwa wakazi wa Arusha kuchukuwa tahadhari katika kipindi hiki cha mvua kubwa zinazoendelea kunyesha kwa kukarabati nyumba zao na kuacha kujenga chini ya mti ama kwenye vyanzo vya maji.



Amesema kujenga katika vyanzo vya maji ama chini ya mti ni kujitafutia majanga mengine hivyo ni vema kila mkazi wa Mkoa wa Arusha kuchukuwa tahadhali hiyo.

Aidha kamanda ametoa tahadhari kutokana na habari za uzushizinazoendele kuwa jana kwenye kuaga miili ya wanafunzi kuna mtu alidondoka juu ya mti na kufariki pamoja na mama mmoja mtoto wake mdogo alifariki,amesema habari hizo siyo za kweli wananchi wazipuuze kabisa 
 Mti ulioanguka ukang'ookana shina lake na kuangukia nyumba na kusababisha maafa hayo ya watu watano wa familia moja.
Jitihada za uokozi zikiendelea 
Miili ikiwa imeshapakiwa ndani ya gari la polisi kwenda kuhifadhiwa hospitalini

LOWASSA AWALILIA WANAFUNZI WALIOFARIKI KATIKA AJALI, MAITI 32 ZAPELEKWA MOCHWARI KATIKA HOSPITALI YA LUTHERAN KARATU.

Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa ametuma salamu za rambi rambi kutokana na tukio la watu 32 kufariki dunia katika ajali ya basi.
Waliofariki katika ajali hiyo iliyotokea leo asubuhi Karatu, ni wanafunzi 29, walimu wawili, pamoja na dereva wa gari hilo.
“Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya ajali hiyo, ni ajali mbaya ambayo inaifanya siku hii kuwa mbaya katika historia ya nchi yetu,”alisema
Miongoni mwa wanafunzi waliofariki ni pamoja na wanaume 11 na wasichana 18.
Kadhalika maiti 32 zikiwamo za walimu wawili, dereva mmoja na wanafunzi 29 zimepokelewa sasa hivi katika Hospitali ya Lutheran Karatu.
Tutaendelea kuwapa habari zaidi kuhusu tukio hili.

UPDATES: WANAFUNZI 31 NA WALIMU WAO WADAIWA KUPOTEZA MAISHA KATIKA AJALI YA GARI WILAYANI KARATU LEO

Kamanda wa Polisi, mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo amesema wanafunzi 31 na walimu wao wamefariki katika ajali iliyotokea wilayani Karatu, ulipo mto Mlera.
Mkumbo amesema wanafunzi waliopoteza maisha katika ajali hiyo ni wa shule ya mchepuo wa Kiingereza, iitwayo Luck Vicent ya mjini Arusha.
Kati ya wale waliofariki 28 walikuwa wanafunzi huku watatu wakiwa ni dereva na walimu wao
Ripoti zinasema kuwa basi hilo liliteleza na kukosa mwelekeo ,likatoka katika barabara na kuanguka katika mto katika eneo la Marera eneo la Rhotia, kilomita chache kabla ya karatu katika barabara ya Arusha
Zoezi la uokoaji likiendelea.

MAMIA YA ABIRIA WAKWAMA NJIANI BAADA YA LORI LILILOBEBA MAKAA YA MAWE KUPATA AJALI NAMTUMBO MKOANI RUVUMA.

Watu watatu wamenusurika kufa huku mamia ya abiria wanaosafri kuelekea Dar es Salaam  na mikoa ya Lindi na  Mtwara na wanaotokea mkoa wa Ruvuma wakielekea  mikoa hiyo wakikwama njiani  baada ya roli lililobeba makaa ya mawe aina ya Scania kupinduka na kuziba barabara  katika daraja la Lwinga wilayani Namtumbo  mkoani Ruvuma.
Walionusurika kwenye ajali hiyo akiwemo kondakta wa lori hilo  lililotokea  mkoani Ruvuma likielekea jijini Dar es Salaam  Bw. Charles Ngonyani wanasema ajali hiyo imetokea wakati dereva wao haji mashaka akilikwepa lori  jingine aina ya fuso ndipo likapinduka  na kuziba  barabara.

Kondakta huyo anasema kuwa katika ajali hiyo aliyeumia zaidi ni dereva wao Haji Mashaka aliyelazwa  katika kituo cha afya cha Namtumbo  huku  yeye  na  mwenzake  Charles  Ngaponda wakipata majeraha madogo madogo.

Kwa upande wao abiria wanaosafiri  kuelekea  mikoa ya Dar es Salaam na mikoa ya Lindi na Mtwara na wanaotokea mkoa wa Ruvuma wakielekea mikoa hiyo wanaeleza adha wanayoipata kutokana  na ajali hiyo.

Jeshi la polisi mkoani Ruvuma  limethibitisha kutokea kwa  ajali hiy  huku likisimamia zoezi la kuliondo lori lililoziba  bara bara.

AJALI YA GARI YATOKEA KIMARA SUKA JIJINI DAR ES SALAAM, WAMSHAMBULIA MWANDISHI ALIYEKUWA AKICHUKUA PICHA ZA TUKIO

Gari aina ya Mark II Grand yenye namba za usajili T145 AMZ likiwa limeivaa daladala lenye namba za usajili T992 DGZ lililokuwa limepaki kituoni KIMARA -SUKA jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa mashuhuda waliokuwa wapo eneo la tukio ilionyesha dereva wa gari hilo dogo alikuwa amelewa na ndipo aliposhindwa kukamata breki na kujikuta uvunguni kwa daladala hilo.
Vijana wakijaribu kuiba katika gari ndogo iliyokuwa imepata ajali eneo la Kimara Suka jijini Dar es Salaam.
Vijana ambao walivamia gari ndogo na kuanza kuiba wakishangaa kuona kamera ya Kajunason Blog imetinga eneo hilo na ndipo walipoungana na mwenye gari kumfanyia fujo na kumpiga kwa kumshambulia mwandishi wa habari Cathbert Angelo Kajuna aliyekuwa eneo la tukio. Kwa msaada wa wasamalia wema waliweza kumnasua mwandishi huyo na kuweza kumshika kijana aliyekuwa mmiliki wa gari ndogo ambaye ndiye alitoa amri ya kumshambulia mwandishi wa habari. Kijana aliyemshambulia mwandishi wa habari Cathbert Angelo Kajuna amekatwa na kufunguliwa jarada la KMR/RB/3987/2017 na mpaka sasa anashikiliwa na Jeshi la Polisi kituo cha Mbezi kwa Yusuph.

WATU ZAIDI YA 60 WANUSURIKA KIFO KWENYE AJALI YA BASI NA GARI DOGO

 Watu wawili wamejeruhiwa na wengine zaidi ya 60 wakinusurika kifo baada ya basi la kampuni ya Ruksa Class kugongana uso kwa uso na gari dogo aina ya Toyota Hilux katika eneo la Nhehelegani mkoani Shinyanga.
 Kamanda wa polisi wa mkoa huo, Muliro Jumanne amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo leo (Jumanne) saa 3.00 asubuhi wakati basi hilo likitokea jijini Mwanza kuelekea mkoani Kigoma.
Kamanda Jumanne amewataja waliojeruhiwa kwenye ajali hiyo kuwa ni Benard Bisansaba(45), ambaye ni mchumi wa halmashauri ya wilaya ya Tarime na Kassim Shaaban (41) ambaye ni mwandisi wa halmashauri hiyo.
“Majeruhi wote wamelazwa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga kwa matibabu,” amesema Jumanne. 
Picha zote na Masegwa Blog

WATU 12 YAJERUHIWA KWENYE AJALI YA MABASI NA LORI ENEO LA MLIMA KITONGA

Watu 12 wamejeruhiwa na watatu kati yao wamelazwa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa baada ya kutokea ajali iliyohusisha magari mawili ya abiria na lori moja, katika eneo la Mlima wa Kitonga wilaya ya Kilolo mkoani hapa.
Akizungumza na gazeti hili baada ya kutokea kwa ajali hiyo Saa 7 mchana leo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Julius Mjengi amesema magari yote matatu yaliyohusika kwenye ajali hiyo yalikuwa yakienda jijini Dar es Salaam.
Ameyataja mabasi yaliyohusika kwenye ajali hiyo kuwa ni ya Kampuni ya Happy Nations, Abood na gari moja la mzigo.
Mjengi amesema katika ajali hiyo watu 12 walipata majeraha na watatu kati yao wamefikishwa Hospitali ya Rufaa ya mkoani Iringa kwa matibabu na tisa kati yao walitibiwa na kuruhusiwa kutoka hospitali.
Kamanda huyo ametaja chanzo cha ajali kuwa ni dereva wa gari la Abood lililokuwa nyuma ambaye aliligonga basi la Happynations ambalo nalo gari lilikuwa mbele yake na kusababisha magari yote kuserereka na kutoka pembeni mwa barabara.

Mbunge Paulina Gekul anusurika Kifo, Ziara yaahirishwa

Mbunge wa jimbo la Babati mjini Paulina Gekul amenusurika kifo baada ya gari lake lenye namba za usajili T 189 BHQ kuacha njia na kupinduka vibaya ambapo mbunge huyo alikuwa katika msafara wa naibu waziri wa Mazingira Luhaga Mpina wilayani Babati mkoa wa Manyara.

Baada ya ajali hii kutokea mmbunge Paulina Gekul ambaye ni mmbunge wa babati mjini akakimbizwa hospitali ya mkoa wa manyara na kulazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi I.C.U huku wanahabari wakikatazwa kuingia katika chumba hiki na madakatari ambao wanamuhudumia mbunge huyo 
 
Hata hivyo baada ya ajali kutokea naibu waziri wa mazingira amelazimika kuahirisha ziara yake ya kutembelea maeneo mbalimbali ndani ya mji wa babati huku mpina akiipongeza halmasahauri ya mji wa babati kwa kutambua umuhimu wa kutunza mazingira katika hali ya usafi baada ya kununua gari kwaajili ya kubebea taka lenye thamani ya zaidi ya milioni 200.

GARI LA MBUNGE LAUA, MWENYEWE ANUSURIKA

Mtumishi wa Hospitali ya Wilaya ya Magu mkoani Mwanza, Moses Mjuni amefariki dunia baada ya kugongwa na gari la Mbunge wa Tarime Mjini (Chadema), Esther Matiko katika Kijiji cha Kishamba wilayani humo.
Mkuu wa Wilaya ya Magu, Khadija Nyembo alisema jana kwamba ajali hiyo ilitokea juzi saa mbili usiku, “Gari la mbunge lilimgonga mtumishi wetu wa Hospitali ya Magu ambaye alikuwa anaendesha pikipiki na dereva wa gari hilo amekamatwa yupo polisi,” alisema Nyembo.
Akizungumza kwa simu jana, Matiko alisema ajali hiyo ilitokea takribani kilomita 10 kutoka Daraja la Mto Simiyu wakati akitoka Mwanza ambako walikutana na mwendesha pikipiki na dereva wake, Kelvin Matango alikuwa akimkwepa baada ya kuingia upande wake.
“Nilitoka Mwanza saa 12:00 jioni kwenda jimboni kwangu (Tarime), tulipopita mbele kidogo karibu kilomita10 kutoka daraja la Mto Simiyu, ghafla alijitokeza mwendesha pikipiki akawa anaendesha kwa kuyumbayumba na dereva alishindwa jinsi ya kumkwepa akamgonga, mimi nilikuja kuona yule mtu ameshafariki dunia,” alisema Matiko.
Matiko alisema licha ya kwamba hakupata majeraha, baada ya kutokea ajali hiyo alipelekwa katika Hospitali ya CF ya jijini Mwanza ambako alipewa dawa na kuruhusiwa.
Hata hivyo, Matiko alisema alikuwa akisikia maumivu makali ya mgongo na mbavu hivyo kutakiwa kwenda kufanyiwa vipimo kuona kama atakuwa amepata madhara.
“Nasikia maumivu makali ya mgongo na mbavu za kulia, nahisi mkanda wa gari ulinibana zaidi, nilitakiwa kwenda hospitali ya CF kufanyiwa uchunguzi lakini nimeshindwa kwa sababu hapa tunapozungumza naenda Magu kumaliza masuala ya polisi kwani dereva na gari vipo polisi,” alisema Matiko.
Alisema baada ya kumaliza kushughulikia masuala hayo ndipo atarudi tena hospitali kufanya uchunguzi wa afya yake.

Mmiliki wa Villa Park Makambako afariki kwa ajali mbaya akiwa na mpenzi wake

Gari ya Kizito baada ya kupata ajali

Mmiliki wa kiota cha Villa Park cha mjini Makambako, Kizito, amepoteza maisha kwenye ajali mbaya ya gari iliyotokea Jumapili usiku.

Ajali hiyo inadaiwa kutokea Morogoro. Inasemekana alikuwa na mpenzi wake ambaye kutokana na mwili wake kusagika vibaya alishindwa kufahamika mara moja.

Kizito alikuwa akitoka kwenye mechi ya mpira kati ya Njombe na Kurugenzi na ajali ilitokea saa nane usiku.

Kizito enzi za uhai wake akiwa amesimama pembeni ya gari yake Toyota Harrier iliyopata ajali

MAGARI MANNE YAGONGANA BARABARA YA NYERERE ENEO LA MTAVA JIJINI DAR ES SALAAM NA KUMJERUHI DEREVA TEKSI

 Wananchi wakimuangalia dereva wa teksi aliyejeruhiwa baada ya gari lake lenye namba za usajili T 625 AWS kugongana na gari dogo lenye namba usajili T 214 CFX wakati likiingia barabara ya Nyerere likitokea Jengo la Kibiashara la Quality Centre Dar es Salaam leo asubuhi.
 Mwonekano wa Teksi hiyo namba T 625 baada ya kugongana.
 Wananchi wakiangalia ajali hiyo.
 Wananchi wakiangalia gari dogo aina ya Toyota Corolla lenye namba T 214 CFX baada ya kuyagonga magari namba T 741 DEK na T 596 BCG katika eneo hilo la Mtava.
 Askari wa Usalama Barabarani akipima ajali hiyo.
 Gari dogo aina ya Toyota Corolla lenye namba T 214 CFX likiwa eneo la ajali kabla ya kuondolewa.

Na Dotto Mwaibale
DEREVA wa gari dogo teksi yenye namba za usajili T 625 AWS amenusurika kufa baada ya gari lake alilokuwa akiliendesha kutoka mjini akielekea Uwanja wa Ndege kugongana na gari dogo lenye namba T 214 CFX aina ya Corolla lililokuwa likiingia Barabara ya Nyerere likitokea Jengo la Biashara la Quality Centre eneo la Mtava jijini Dar es Salaam leo asubuhi.

Mashuhuda wa ajali hiyo wakizungumza na waandishi wa habari eneo la ajali walisema ajali hiyo ilisababishwa na gari hilo dogo aina ya Corolla lililokuwa likiingia barabara ya Nyerere bila kuchukua tahadhari.

"Chanzo cha ajali hii ni gari hilo dogo aina ya corolla ambalo liliingia barabara ya Nyerere bila ya dereva wake kuchukua tahadhari na kama dereva wa gari namba T 625 AWS angekuwa katika mwendo wa kawaida madhara yake yasingekuwa makubwa kiasi hicho" alisema shuhuda aliyejitambulisha kwa jina la Mlugulu.

Mlugulu alisema baada ya magari hayo kugongana gari hilo aina ya Corolla liligeuka na kwenda kuyagonga magari mengine namba T 596 BCG na T 741 DEK yaliyokuwa yamesimama yakisubiri kuingia upande ambao lipo Jengo la Kibiashara la Quality Centre.

Katika ajali hiyo gari namba T 625 AWS liliacha njia na kuhamia upande wa pili wa barabara ya kutoka Tazara kwenda mjini.

Baada ya ajali askari wa usalama barabarani walifika na kupima ajali hiyo na kuchukua maelezo ya madereva wote wanne ambapo magari mawili T 214 CFX na T 625 AWS yakiondolewa na  magari ya kukokota magari mabovu (Breck Down) na kupelekwa kituo cha Polisi cha Chang'ombe Temeke jijini Dar es Salaam kwa hatua zingine za kisheria.

BREAKING NEWS:TRENI YA ABIRIA DELUX IMEANGUKA JIONI HII, ILIKUWA IKITOKA KIGOMA KUJA DAR ES SALAAM

NA K-VIS MEDIA/Khalfan Said
TRENI ya mwendo haraka, (DELUX), iliyokuwa ikitokea Kigoma kuja jijini Dar es Salaam, imeanguka eneo la Ruvu mkoani Pwani jioni hii ya Januari 29, 2017.

Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana kutoka eneo la ajali,zinasema takriban mabehewa 10 yameanguka na juhudi za kuwaokoa watu zilikuwa zikiendelea na watu kadhaa walionekana wakiwa wamelala chini wengine hawajiwezi kabisa.
Msemaji wa TRL, Medladjy Maez amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo, na alipoongea na mwandishi wa habari hizi majira ya saa 11;13 jioni, amesema treni hiyo imeanguka na ni mabehewa matano ya abiria yameanguka na moja limeacha njia, lakini hakuwa na taarifa zaidi kwani ndio alikuwa anajiandaa kuelekea eneo la tukio.

“Ni kweli treni yetu ya Delux iliyokuwa ikitokea Kigoma na kutarajiwa kuwasili hapa saa 11:30, imeanguka eneo la Ruvu, na mabehewa matano yameanguka na moja limeacha njia, taarifa zaidi tutazitoa kuhusu walioathirika kwa sasa tunajiandaa kwenda eneo la tukio” Alisema Maez.

Taarifa zaidi zitawajia kadri zitakavyotufikia

BEN WA BONGO MOVIE APATA AJALI MBAYA YA GARI, ALAZWA MUHIMBILI

Msanii mkongwe wa filamu za vichekesho,  Ben Branco Selengo amelazwa katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili baada ya kupata ajali mbaya ya gari siku ya sikukuu ya Christmas.

Muigizaji Mboto ambaye ni rafiki wa karibu wa Ben, kupitia instagram ameandika:
Ajali ulioipata sio ndogo kwetu sisi wanadam, lakin kwa mungu ni ndooogo sana. Naamin ndogo kwa mungu kwasababu utapona kwa uwezo wake mungu. Utapona tu inshaallah (Benn Blanco Selengo)
Akiongea na Bongo5 asubuhi hii ndugu wa karibu wa Ben kupitia simu ya Ben, alidai Ben alipata ajali mbaya ya gari juzi na hali yake bado ni mbaya.
“Ben hali yake siyo nzuri kusema kweli,” alisema dada huyo aliyejitambulisha kwa jina na Sarah. “Alipata ajali ya gari juzi na hapa tunapozungumza bado yupo Muhimbili hospitali.”

AJALI YAUA PADRI NA WAUMINI WATANO

Watu sita wamefariki dunia na wengine wanne kujeruhiwa baada ya magari mawili kugongana uso kwa uso eneo la Kanegere, Kata ya Bukandwe, Wilaya ya Mbogwe mkoani Geita.

Ajali hiyo imetokea jana saa 9.30 alasiri.
Habari zilizopatikana usiku huu, zinadai kuwa miongoni mwa watu waliofariki ni Padri wa Kanisa Katoliki Jimbo la Kahama ambaye aliwabeba abiria wanaosemekana ni waumini wa kanisa hilo ambao baadhi yao pia wamefariki dunia.
Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe, Salum Ndimu amekiri kupokea maiti wanne na majeruhi wanane.

CHANZO: MWANANCHI