HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

Safari ya Himid Mao kutimkia Ulaya imekwiva

Mchezaji wa Azam FC, Himid Mao

Kiungo wa Klabu ya Azam FC, Himid Mao ambaye mwanzoni mwa mwezi huu alienda nchini Denmark kufanya majaribio na Klabu ya Randers FC, ndoto ya kiungo huyo ya kucheza soka la kulipwa ipo karibu kutimia kwani mabosi wa Klabu hiyo na wa Azam FC wamekutana jijini Dar es salaam kufanya mazungumzo ya mwisho kuhusu usajili wake.
Hatua hiyo imekuja baada ya Himid kufuzu majaribio ya siku 10 aliyoenda kufanya katika timu hiyo inayoshiriki Ligi Kuu ya Denmark, mapema mwezi huu.
Ofisa Habari wa Klabu ya Azam FC, Jaffar Idd amesema kuwa kwa sasa wapo kwenye mazungumzo na mabosi hao wa Randers baada ya kuwapa habari kwamba kiungo wao amefuzu majaribio yake.
Tupo kwenye majadiliano na wao, tunasubiri kusikia ofa yao na kama tukikubaliana basi Himid ataenda kujiunga nao kwa sababu wametuambia tayari amefuzu, hivyo mazungumzo yaliyopo sasa ni baina yao na sisi”, alisema Jaffar Idd kwenye mahojiano yake na Gazeti la Championi.
Kwa upande mwingine Kocha wa Azam FC, Aristica Cioaba amesema kuwa kama dili hilo litafanikiwa, basi anamtakia kila la heri kiungo huyo.

AZAM FC YATWAA UBINGWA WA MAPINDUZI CUP 2017 KWA KUITANDIKA SIMBA 1-0

Shuti la ‘mwendokasi’ la umbali usiopungua mita 25 la kiungo Himid Mao limetosha kuamua matokeo ya mchezo wa Fainali ya Mapinduzi uliofanyika mjni Zanzibar.

Miamba hiyo ya Ligi Kuu Tanzania Bara iliichapa Simba bao 1-0 na kutosha kutangazwa mabingwa wapya wa Kombe la Mapinduzi.

Wakinolewa na kocha wa vijana wa Azam, Idd Cheche aliyechukua kwa muda mikoba ya Zeben Hernandez aliyetimuliwa kwa matokeo mabaya, Azam FC iliibuka na ushindi wa bao la dakika ya 13 lililofungwa na kiungo huyo wa Taifa Stars, Himid.

Ushindi huo pia umeifanya Azam FC kutwaa taji la tatu la Kombe la Mapinduzi baada ya awali kulitwaa miaka ya 2011 na 2012.

Katika mashindano hayo, beki wa Simba, Method Mwanjali amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa Mapinduzi Cup, tuzo ya kipa bora imekwenda kwa Aishi Manula wa Azam FC, timu bora ya vijana ni Taifa Jang’ombe.

Mfungaji bora ni kiungo wa Yanga, Saimon Msuva, aliyeweka kimiani mabao manne, wakati mwamuzi bora wa mashindano hayo akichaguliwa kuwa Mfaume Ali.

Mapinduzi Cup Fainali leo nani kuibuka kidedea kati ya Simba au Azam FC?

Fainali za 11 za michuano ya Kombe la Mapinduzi Cup zinatarajiwa kupigwa leo kwenye dimba la Amaan Visiwani Zanzibar kwa kuzikutanisha timu za Simba na Azam zote za Dar es Salaam.


Mchezo huo unaotarajiwa kuanza Saa 2:15 usiku wa leo, utakuwa ni wa pili kuzikutanisha timu hizo katika fainali ya michuano hiyo.
Awali zilikutana katika fainali ya mwaka 2012 na Azam FC ikaibuka na ushindi wa mabao 2-1 na kutwaa taji lake la kwanza kati ya mawili ya Kombe la Mapinduzi, linguine likija mwaka 2013 baada ya kuifunga Tusker katika fainali.
Simba ndiyo mabingwa mara nyingi wa taji hilo, mara tatu baada ya kulitwaa katika miaka ya 2008 ikiifunga Mtibwa Sugar katika fainali, 2011 ikiwafunga mahasimu, Yanga na 2015 wakiwafunga Mtibwa Sugar.
Kocha wa Simba Joseph Omog, amepania kulitwaa taji hilo, kwa lengo la kuondoa ukame wa makombe ambayo umeikumba klabu hiyo kwa misimu minne iliyopita pasipo kubeba ubingwa wowote
Azam mara zote ilizoingia fainali ilitwaa taji hilo, wakati Simba mwaka 2012 na 2014 ilicheza mechi ya mwisho na kufungwa na kukosa Kombe hilo.
Kuelekea mchezo wa leo, kila timu iko vizuri baada ya rekodi nzuri katika mechi zilizopita, Simba wakiwatoa wapinzani wa jadi, Yanga kwa penalti 4-2 baada ya sare ya 0-0 kwenye Nusu Fainali na Azam wakiitoa Taifa Jang’ombe kwa bao 1-0.
Timu zote ziliongoza makundi yao, Simba A lilikuwa na timu tano kwa pointi zake 10 na Azam B lililokuwa na timu nne kwa pointi zake saba.

PICHA:YANGA YAKUBALIKICHAPO CHA BAO 4- 0 KUTOKA KWA AZAM


 Timu ya soka ya Yanga ya Dar es Salaam, imebugizwa mabao 4-0 na Vijana wa Chamazi, Azam Fc kwenye pambano la shoka katika michuano ya kombe la Mapinduzi kwenye uwanja wa Aman mjini Unguja usiku huu Januari 7, 2017.  Magoli ya Azam Fc yalifungwa na Boko  dakika ya 2,  Yahaya Mohamed dakika ya  55,  Joseph Mahundi  dakika ya 80 na  Enoc dakika ya 85.(PICHA NA OTHMAN MAPARA WA ZANZINEWS).













Azam FC ya watimua makocha wao kutoka nchini Hispania

Uongozi wa klabu ya Azam FC, unapenda kuufahamisha umma kuwa umefikia makubaliano ya pande mbili ya kusitisha mikabata ya makocha wake kutoka nchini Hispania.

Jopo hilo la makocha linaundwa na Kocha Mkuu Zeben Hernandez, Msaidizi wake, Yeray Romero, Kocha wa Makipa Jose Garcia, Kocha wa Viungo, Pablo Borges na Mtaalamu wa tiba za Viungo, Sergio Perez.
Uamuzi huo umefikiwa na Bodi ya Wakurugenzi wa timu hiyo jana, na umetokana na mwenendo mbaya wa Azam FC kwenye Ligi Kuu ya Tanzania Bara , ambayo imefikia raundi ya pili hivi sasa.
Azam FC inawatakia kila la kheri na mafanikio mema makocha hao huko waendako na inawashukuru kwa mchango wao wote walioutoa kwenye timu kwa kipindi chote walichokaa, ikiwemo kuwapa taji la kwanza la Ngao ya Jamii mwaka huu kwa kuifunga Yanga kwa mikwaju ya penalti 4-1 kufuatia sare ya mabao 2-2.
Wakati huu ambapo uongozi wa Azam FC upo katika mchakato wa kusaka kocha mpya, kikosi hicho kitakuwa chini ya makocha wa timu ya vijana ya timu hiyo, Idd Cheche na Kocha wa Makipa, Idd Abubakar, ambao walianza kazi jana jioni kukiandaa kikosi kuelekea mchezo wa leo dhidi ya Tanzania Prisons.
Azam FC inapenda kuwaambia mashabiki wake kuwa wawe watulivu katika kipindi hiki kwani uongozi umefanya uamuzi sahihi kwa ajili ya kuinyanyua timu juu ili hatimaye ushiriki wetu wa michuano mbalimbali uweze kuwa ni wa kiwango cha juu tofauti na hali ilivyokuwa sasa.
Hernandez anaondoka Azam FC akiwa ameingoza timu hiyo kwenye mechi 18 rasmi ambazo ni za mashindano, 17 za ligi na moja ya Ngao ya Jamii, amefanikiwa kushinda mechi nane, sare sita na kufungwa mara nne.

FARID: SIYO KWELI KUWA AZAM FC ILIKUWA INANIBANIA KWENDA HISPANIA

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Farid Mussa wakati akiongea na waandishi wa habari
Mchezaji wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, Farid Mussa, ameweka wazi kuwa mabingwa hao hawajambania kwenda nchini Hispania kucheza soka la kulipwa kama ilivyoripotiwa na vyombo mbalimbali vya habari.
Kwa kuudhihirishia umma, Mussa amejitokeza hadharani na kupinga madai hayo akidai kuwa muda wowote kuanzia sasa atakwenda nchini humo kujiunga na Club Deportivo Tenerife inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza baada ya kupata ‘Visa’ maalumu ya kuingia nchini akiwa kama mfanyakazi.
“Kwanza napenda kumshukuru Mungu baada ya kupata visa, haikuwa kazi rahisi namshukuru Meneja Mkuu Abdul (Mohamed) kapigania hadi suala hili limekamilika, cha kwanza nilikuwa ninawaomba Watanzania wajue kuwa Azam haikuwa inanibania ni masuala tu ya visa yalikuwa yakisumbua ubalozini.
“Mara baada ya kupata visa ya kufanya kazi muda wowote ninaweza kuondoka kuanzia Januari,” alisema Farid wakati akizungumza mbele ya waandishi wa habari wakati wa zoezi la kutambulishwa wachezaji wapya waliosajiliwa na timu hiyo.
Taarifa hizo zilianza kutolewa kwenye vyombo vya habari, kufuatia suala la Farid kwenda Hispania kuwa kimya lakini ukweli wa mambo ni kuwa visa hiyo ndio iliyokuwa ikikwamisha dili hilo.
Naye Ofisa Habari wa Azam FC, Jaffar Idd, akitolea ufafanuzi suala hilo alisema kuwa lengo la uongozi huo lilikuwa ni kinda huyo kuondoka mapema kuelekea nchini humo, lakini suala kubwa lilikwamisha ni visa hiyo ya kufanya kazi nchini Hispania.
“Uongozi wa Azam FC ulikuwa sambamba na Tenerife kuhakikisha Farid anaondoka, lakini tunashukuru suala hilo limekamilika kwa asilimia 98, lakini ni kwamba Farid muda wowote kuanzia sasa Mungu akijaalia ndani ya wiki mbili zijazo au wiki moja anaweza kuondoka kutoka Tanzania kuelekea Hispania,” alisema.
Azam FC inaamini ya kuwa kuondoka kwa nyota huyo wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kutafungua milango kwa wachezaji wengine ndani ya timu hiyo na Taifa kwa ujumla kuweza kupata nafasi ya kucheza soka la kulipwa barani Ulaya.

TFF yazibariki Yanga na Azam michuano ya Afrika

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.



 Shirikisho la Soka nchini TFF limetoa leseni ya awali kwa vilabu vya Yanga na Azam FC ambazo zinashiriki mashindano ya kimataifa hapo mwakani.



Afisa habari wa TFF Alfred Lucas amesema, leseni hiyo ni uthibitisho kuwa wana vigezo vyote vinavyowafanya kushiriki michuano ya ligi kuu pamoja na mashindano ya kimataifa.



Vigezo hivyo ni pamoja na umiliki wa klabu wa mtu mmoja, uwanja wa nyumbani wa kuchezea, uwanja wa kufanyia mazoezi na timu ya vijana ambayo inapata huduma zote ikiwemo matibabu pamoja na ushiriki wake katika mashindano mbalimbali ya vijana.



Alfred amesema, leseni hiyo imetoka mara baada ya vilabu hivyo kujaza fomu ambazo zinaonyesha wachezaji pamoja na benchi la ufundi litakalotumika katika mashindano ya kimataifa na jana ilikuwa mwisho kuwasilisha fomu ambapo Yanga itashiriki mashindano ya Klabu bingwa Afrika huku Azam FC ikishiriki Kombe la Shikisho Afrika.

Iwapo klabu mojawapo au zote zitakuwa na mabadiliko kati ya wachezaji au kocha zitalazimika kulipia faini ili kuongeza au kufanya marekebisho ya aina yoyote.

Alfred amesema, mara baada ya kupata leseni hiyo Shirikisho la Soka barani Afrika CAF watakuja kwa ajili ya kufanya uthibitisho ambao utasaidia vilabu hivyo kupata leseni ya CAF na watakuwa katika maandalizi huku wakisubiri kupangwa kwa ratiba ya mashindano yanayotarajiwa kuanza kutimua vumbi mapema mwakani.

AGYEI ASAINI MIAKA MITATU AZAM FC

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.



UONGOZI wa Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam FC, unayofuraha kuwaataarifu wapenzi wa soka kuwa jioni ya leo umefanikiwa kuingia mkataba wa miaka mitatu na kiungo mshambuliaji kutoka Ghana, Enock Atta Agyei.

Agosti mwaka huu, Azam FC tuliingia makubaliano maalumu na Medeama ya Ghana juu ya kumsajili kinda huyo anayetimiza umri wa miaka 18 mwakani baada ya benchi la ufundi kuridhishwa na uwezo wake na sasa amejiunga rasmi kwenye viunga vya Azam Complex.

Agyei anasaini mkataba tayari kabisa kuanza kuitumikia Azam FC katika mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) mwakani pamoja na michuano mingine ikiwemo Kombe la Shirikisho Afrika.


Tunaamini ya kuwa ujio wa nyota huyo wa timu ya Taifa ya Vijana ya Ghana chini ya miaka 17, utazidi kuipa nguvu timu yetu kuelekea kwenye michuano inayotukabili mbeleni, hivyo tunapenda kumtakia mafanikio mema kwa kipindi chote atakachokuwa akiipigania jezi ya Azam FC.

Azam FC tunapenda kuwafahamisha mashabiki wetu kuwa tutaendelea kukifanyia marekebisho kikosi chetu kuelekea usajili wa dirisha dogo, lengo ni kukipa nguvu kikosi hicho ili kifanye vizuri zaidi katika michuano ya hapa nchini pamoja na ile ya Kimataifa.

Lengo kubwa la Azam FC ni kuendelea kuwafurahisha mashabiki wetu kwa kupata matokeo bora uwanjani, na tunaamini ya kuwa, benchi zuri la ufundi tulilokuwa nalo, wachezaji wazuri walioko kikosini na wengine watakaokuja kuongeza nguvu, wote kwa pamoja wataweza kutuvusha kuelekea safari ya mafanikio msimu huu.

Hivyo, tunawaomba mashabiki wetu kuvuta subira na kuendelea kuisapoti timu kwani tunaamini ya kuwa nyie ndio nguzo muhimu ya 12 uwanjani katika kuwapa hamasa wachezaji ya kupata matokeo bora pamoja na kuijenga timu kiujumla. 


Wakati huo huo, leo tumewapokea wachezaji saba waliokuja kwenye majaribio ya kujiunga na Azam FC, ambao ni mabeki wa kati Mbimbe Aaron Nkot (Cameroon), Kone Nabil Ibrahim (Ivory Coast), kiungo mkabaji Kingue Mpondo Stephane (Cameroon),

Wengine ni washambuliaji Yaya Awaba Joel (Cameroon), Samuel Afful, Benard Ofori (wote Ghana) na Konan Oussou kutoka Ivory Coast. 

Imetolewa na Uongozi Azam FC