HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

RIDHIWANI KIKWETE AUSHANGAA UKIMYA WA MWIGULU NCHEMBA

Mbunge wa jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete anamshangaa Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba kuendelea kukaa kimya juu ya matatizo ya kiusalama kwa wananchi yanayoendelea nchini wakati yeye ndio kiongozi mwenye dhamana ya kulitatua hilo.

Akiongea bungeni Jumanne hii, mbunge huyo amesema, “Kumekuwa na malalamiko mengi sana, tumeshuhudia malalamiko mengine yanahitaji majawabu kama siyo majibu ya haraka ili kuondoa hizi sintofahamu walizonazo wananchi.”
“Niwaombe sana hakuna sababu ya mtu kama Mhe. Waziri Mwigulu kuendelea kukaa kimya wakati wananchi wanalalamika juu ya hali yakiusalama katika maisha yao,” ameongeza.
“Mimi binafsi niishauri serikali yangu kwamba unapojibu jambo lolote lile unatoa hali ya wasiwasi,” amesisitiza.

RAIS MAGUFULI AMTEUA MAMA SALMA KIKWETE KUWA MBUNGE


VIDEO: RIDHIWANI KIKWETE AFAFANUA KWANINI ILIKUWA NI AIBU KWA TFF NA WAZIRI, DIAMOND KUKABIDHIWA BENDERA KWENDA GABON

Ridhiwani Kikwete aliingia kwenye headlines mwanzoni mwa mwezi uliopita pale alipoandika post Instagram akisikitishwa na kitendo cha Diamond kukabidhiwa bendera na Waziri wa michezo, Nape Nnauye kwenda kutumbuiza kwenye ufunguzi wa kombe la mataifa ya Afrika, nchini Gabon.


Mbunge huyo wa Chalinze, amedai kuwa, post yake haikumlenga Diamond, bali aliwapa ujumbe shirikisho la soka Tanzania, TFF na Waziri Nape.


“Kilichonifanya niandike ile meseji ni baada ya kuona kwamba mashindano yanayoenda kufanyika ni ya mpira wa miguu, sisi tunayo timu ya taifa ya mpira wa miguu, lakini to our surprise, badala ya kutoa bendera kwa timu ya mpira wa miguu, tunawapa waburudishaji kwa maana ya wanamuziki kama Diamond,”
Ridhiwani alisema kwenye mahojiano na The Beauty TV.


“Matarajio yetu sisi ni kumuona kapteni wa taifa ndiye anayepokea bendera na sio wanamuziki,” ameongeza. “Pia watu wa TFF, kwamba nao wanashangilia yale anayoyafanya waziri?” Hivi vitu lazima tuwe serious.”
“Diamond yeye nampongeza sana, kwa hatua aliyofika, anafanya kazi nzuri, na ndio maana watu wamemuona, wamempa nafasi ya kwenda kutumbuiza ambayo sisi kama watanzania we feel proud. Lakini the bottom line ni kwamba, nini agenda kubwa inayomfanya Diamond aende Gabon? Ni mpira wa miguu, Diamond si mchezaji wa mpira wa miguu, hata kama labda anashabikia mpira wa miguu, lakini yeye ni mshabiki tu, wanaoenda kushiriki pale ni wachezaji.”
Ridhiwani amekiri kuwa kitendo hicho kilimsikitisha na ndio maana hakupenda kukaa kimya.
“Si kwamba sikupenda kwasababu amepewa Diamond, hapana, sikupenda kwa sababu, matarajio ya mimi mpenzi wa mpira ni kumuona kapteni wangu wa timu ya taifa anapokea bendera kwa niaba ya watanzania wote, anakwenda kutuwakilisha kule, hata kama tutashindwa, hata kama tutafanikiwa lakini anayetakiwa kwenda kule ni kapteni wa timu ya mpira wa miguu kwenda kutuwakilisha kama taifa na si vingine.”

RIDHIWANI KIKWETE AFUNGUKA KUHUSU BIFU ZILIZOPO KWENYE MUZIKI

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Mbunge wa Jimbo la Chalinze na mtoto wa Rais mstaafu wa Tanzania wa awamu ya nne, Mhe. Ridhiwani Kikwete amefunguka kuhusu bifu za wasanii zinazoendelea kwenye muziki hapa nchini.
Ridhiwani ameiambia Bongo5 wakati wa uzinduzi wa video mpya ya Belle 9 ‘Give It To Me’ Jumamosi hii uliofanyika kwenye beach yake maeneo ya Kawe jijini Dar kuwa wasanii wanatakiwa waache malumbano na waangalie kwenye kujiwezesha zaidi ili waweze kuwa juu kuliko walipokuwa jana.
“Mimi ningewaambia hawa vijana wetu ambao hasa wameanza malumbano kwenye muziki. Tumeshuhudia nchi ikimpoteza mwanamuziki mzuri kama Tupac na Notorious B.I.G kwa sababu ya mambo ya kijinga jinga na yasiyofaa kama haya, wajifunze katika hayo,” alisema Ridhiwani.
“Waache kuangalia nani anafanya nini, waangalie wao wanajiwezeshaje kuwa bora kuliko walivyokuwa jana, watafanikiwa,” ameongeza.

Chanzo: Bongo 5

PICHA: MSANII WA BONGOMOVIE JACKLINE WOLPER AITEMA CHADEMA

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Mwigizaji wa filamu nchini Tanzania Jackline Wolper aliyakuwa akimuunga mkono Edward Lowassa katika uchaguzi Mkuu 2015, ametangaza kujiunga na CCM rasmi jana 
Wolper alikaribishwa na mwenyekiti aliyemaliza muda wake Dkt Jakaya Kikwete baada ya kutangaza kujiunga na CCM.
Kitendo hicho kilifanyika katika Mkutano Mkuu Maalum wa CCM uliofanyika jana Julai 23, mkoani Dodoma.

RAIS DK. MAGUFULI ACHAGULIWA KWA KISHINDO KUWA MWENYEKITI MPYA WA CCM LEO MJINI DODOMA

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


 Mwenyekiti Mstaafu wa CCM, Jakaya Kikwete akimkabidhi moja ya vitendea kazi, Mwenyekiti mpya wa CCM, Rais Dk. John Magufuli baada ua Wajumbe wa mkutano Mkuu wa CCM, kumpitisha asilimia kwa mia ya kura, katika kumchagua leo katika ukumbi wa Dodoma Convetion.
 Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akimpongeza Mwenyekiti mpya wa CCM Rais Dk. John Magufuli baada ya wajumbe wa Mkutano Mkuu maalum wa CCM kumchagua kwa kura asilimia mia kwa mia.
 Mweneyekiti wa CCM mstaafu Rais Mstaafu Jakaya Kikwete na Mwenyekiti Mpya wa CCM Rais Dk. John Magufuli wakipunga mkono baada ya Magufuli kutawazwa rasmi kushika nafasi hiyo leo mjini Dodoma
 Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara Rais wa Zanzibar Dk. Ali Mohammed Shein akimpongeza Rais Dk John Magufuli baada ya kutawazwa rasmi kuwa Mwenyekiti mpya wa CCM lo mjini Dodoma. Katikati ni Mwenyekiti Mstaafu wa CCM Rais Mstaafu Jakaya Kikwete
Mwenyekiti mpya wa CCM, Rais Dk. John Magufuli akitoa hotuba yake, baada ya kutawazwa kushika nafasi hiyo kwa kupata kuta asilimia mia kwa mia zilizopigwa na wajumbe wa mkutano mkuu maalum wa CCM uliofanyika leo mjini Dodoma, Picha zote na Bashir Nkoromo)

JK KUKABIDHI KIJITI LEO KWA DKT JOHN POMBE MAGUFULI

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


 Mwenyekiti wa CCM ambaye leo anatarajiwa kukabidhi kijiti kwa Mwenyekiti Mpya,Rais wa awamu ya nne Dkt Jakaya Kikwete,akifafanua jambo wakati akisoma hotuba yake ya Mwisho katika kiti hicho.PICHA NA MICHUZI JR -DODOMA.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisoma hotuba yake fupi mbele ya Wajumbe na kumkaribisha Mwenyekiti wa CCM ambaye leo anatarajiwa kukabidhi kijiti kwa Mwenyekiti Mpya,Rais wa awamu ya nne Dkt Jakaya Kikwete.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitoa ratiba na miongozo mbalimbali kwa Wajumbe wapatao zaidi ya 2000 wa mkutano Mkuu Maalum wa CCM ambao tayari wako ndani ya ukumbi wa Dodoma Convetion Center (DCC) kukamilisha mchakato wao wa kumchagua Mwenyekiti mpya wa chama hicho cha CCM.
Sehemu ya Meza kuu kama ionekanavyo pichani tayari wamekwisha ingia ndani ya ukumbi wa Dodoma Convetion Center (DCC) kukamilisha mchakato wao wa kumchagua Mwenyekiti mpya wa chama hicho cha CCM.Pichani kulia ni Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana,Mwenyekiti wa CCM ambaye leo anatarajiwa kukabidhi kijiti kwa Mwenyekiti Mpya,Rais wa awamu ya nne Dkt Jakaya Kikwete,Makamu Mwenyekiti Zanzibar Rais Dkt Shein pamoja na Mwenyekiiti mtarajiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli.
 Baadhi ya Viongozi wakuu wa Wastaafu wa chama cha CCM na Serikali kwa ujumla wakifuatilia yanayojili ukumbini .
 Wajumbe wapatao zaidi ya 2000 wakifuatilia hotuba iliyokuwa ikisomwa na Mwenyekiti ambaye leo anaachia kiti hicho na kukabidhi kwa Mwenyekiti mpya Dkt John Pombe Magufuli,katika mkutano Mkuu Maalum wa CCM unaofanyika ndani ya ukumbi wa Dodoma Convetion Center (DCC),mkoani Dodoma.
Mwanana mahiri wa nyimbo za Taarab kutoka kundi la Tot Plus Khadija Kopa akiimba mbele ya Wajumbe wapatao zaidi ya 2000 wa mkutano Mkuu Maalum wa CCM ambao tayari wako ndani ya ukumbi wa Dodoma Convetion Center (DCC) kukamilisha mchakato wao wa kumchagua Mwenyekiti mpya wa chama hicho cha CCM.
Baadhi ya wageni waalikwa kutoka vyama mbalimbali vya upinzani pia wanahudhuria mkutano huu Maalum wa CCM.Ambapo vyama vya siasa vipatavyo 12 vilialikwa na vyote vimefika katika mkutano huo isipokuwa chama cha CHADEMA.
Baadhi ya Wageni waalikwa wakiwemo mabalozi wa nchi mbalimbali wakiwa ndani ya ukumbi ambapo leo mkutano Mkuu Maalum wa CCM unafanyika kwa ajili ya kumchagua Mwenyekiti mpya wa chama cha Mapinduzi (CCM) kwa miaka kumi,Rais John Pombe Magufuli anatarajiwa kukabidhiwa kijiti hicho kutoka kwa Mwenyekiti ambaye anamaliza muda wake leo, Rais Mstaafu wa awamu ya nne,Dkt Jakaya Kikwete,mkutano huo unafanyika ndani ya ukumbi wa Dodoma Convetion Center (DCC) ulioko nje kidogo ya mji wa Dodoma.
Baadhi ya Wageni waalikwa kutoka sehemu mbalimbali wakiwa ndani ya ukumbi ambapo leo mkutano Mkuu Maalum wa CCM unafanyika kwa ajili ya kumchagua Mwenyekiti mpya wa chama cha Mapinduzi (CCM) kwa miaka kumi,Rais John Pombe Magufuli anatarajiwa kukabidhiwa kijiti hicho kutoka kwa Mwenyekiti ambaye anamaliza muda wake leo, Rais Mstaafu wa awamu ya nne,Dkt Jakaya Kikwete,mkutano huo unafanyika ndani ya ukumbi wa Dodoma Convetion Center (DCC) ulioko nje kidogo ya mji wa Dodoma.

JK AONGOZA KIKAO CHA HALMASHAURI KUU YA TAIFA YA CCM MJINI DODODMA LEO

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


 Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete akifungua Mkutano wa Halmashauri Kuu ya taifa ya CCM mjini Dodoma Julai 21, 2016. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mtarajiwa, Rais John Pombe Magufuli na Wapili kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM, Zanzibar, Rais wa Zanzibar Dkt, Ali Mohamed Shein . Kulia ni Makamu Mwenye kiti wa CCM, Bara, Philip Mangula na wapili kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.
  Mwenyekiti wa CCM, Rais Mstaafu, Jakaya Kikwete akisisitiza jambo mbele ya Wajumbe wa Mutano wa Halmashauri Kuu ya taifa ya CCM mjini Dodoma Julai 21, 2016.