HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

Sikiliza na udownload nyimbo mpya ya Snura Ft. Christian bella - ZUNGUSHA

MAX RIOBA ADAI AMESHINDWA KUFANYAKAZI NA YOUNG DEE KWA KUWA HANA NIDHAM

Young Dee akiwa na boss wake wa zamani Max


Uongozi wa label ya Millian Dollar Boys ‘MDB’ iliokuwa unamsimamia rapper Young Dee, amedai hawafanyi tena kazi na rapper huyo kwa madai rapper huyo hana nidhamu.


Max Rioba ambaye ni mkurugenzi wa label hiyo, wiki moja iliyopita alionekana kulalamika katika mitandao ya kijamii akidai rapper huyo amerudi tena katika matumizi ya Madawa ya kulevya.
Akiongea Ijumaa hii katika kipindi cha FNL cha EATV, Max amedai habari za rapper kurudia matumizi ya Madawa ya kulevya na yeye anaziona katika mitandao ya kijamii kuhu akikiri kutofanya kazi tena na rapper huyo kwa madai ya kuwa hana nidhamu.
“Kwa sasa Young Dee hayupo tena kwangu,” alisema Max. “Sikumfukuza Young Dee kutoka kwangu, nilimwambia aondoke, kuna tofauti kati ya kumfukuza na kumwambia aondoke, sababu ni nidhamu.,”
Pia Max alidai kama rapper huyo atahitaji msaada wa pesa kutoka kwake ataendelea kumsaidia lakisi sio tena kuwa pamoja kama zamani.
“Young Dee akihitaji msaada wa kifedha nitamsaidia, hata binti aliyezaa naye akikwama kifedha mimi nitamsaidia, simchukii Young Dee,” alisema Max.
Katika hatua nyingine Max amedai kwa sasa hadhani kama atakuwa na nafasi tena ya kupokea msanii yeyote na kumsimamia.

MAPENZI YANGU NA JACQUELINE WOLPER YAPO MOYONI – HARMONIZE

Msanii wa muziki kutoka WCB, Harmonize amekanusha kuachana na mpenzi wake Jacqueline Wolper baada ya hivi karibuni kuzagaa taarifa katika mitandao ya kijamii kuwa wawili hao wameachana.

Madai hayo yalichukua sura mpya wiki chache zilizopita baada ya malkia huyo wa filamu kudaiwa kufuta picha za mkali huo wa wimbo Bado katika mtandao wake wa instagram.
Akiongea jana katika kipindi cha XXL cha Clouds FM, Harmonize alidai mapenzi yao yapo moyoni na watu wasichanganywe na issue ya kufuta picha instagram.
“Wolper alifuta tu picha za instagram hakufuta mapenzi yetu yapo moyoni,” alisema Harmonize.
Pia muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo Matatizo, alidai suala la malkia huyo kufuta picha instagram ni kawaida kwani anaweza kufuta na kuanza kupost mpya.
Wapenzi hao wamebadili utaratibu wa maisha yao kwani huko nyuma walikuwa wanasafiri na kula bata pamoja.

DARASSA ASHAURIWA NA DAKTARI KUTOFANYA SHOO KWA MUDA BAADA YA KUPATA AJALI.

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Msanii wa muziki wa kizazi kipya Darasa  akizungumza na na chombo kimoja cha radio hapa nchini amesema
 "Nipo hospitalini Muhimbili sasa hivi nawashukuru sana madaktari wa hapa wamenipokea vizuri wamenipa huduma nzuri sana, wamenicheki kwa sababu nilikuwa najisikia vibaya sana sehemu za kichwani nashukuru Mungu majibu yanaonyesha kila kitu kipo poa kabisa kuna damage ndogo wanaifanyia kazi naendelea na matibabu ila nimeshauriwa kupunguza mizunguko kwa wiki moja ili niweze kupumzika na kutibu hayo maumivu ya kichwa"

MWASITI AFUNGUKA BAADA YA KUPATA MANAGEMENT MPYA

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Msanii wa muziki Mwasiti Almas amesema ndani ya muda mchache toka apate management ya kumsimamia tayari ameshaanza kuona mabadiliko makubwa katika muziki wake.

Muimbaji huyo ambaye ameachia wimbo ‘Kaa Nao’ hivi karibuni, amedai ameanza kuona mabadiliko katika namna ambavyo nyimbo zake zinasambazwa. “Kesema kweli sasa hivi maisha ya muziki wangu yamebadilika sana kusema kweli ndani ya muda mfupi, tayari naona management yangu inafanya kazi yake ipasavyo.
 Mimi sikuwahi kuwa na management serious kama hii kusema kweli mpaka napangiwa vitu vya kufanya usiende kule fanya hivi hii ni dalili nzuri kwamba wapo serious,”

Pia muimbaji huyo amedai ameamua kuachia audio ya wimbo wake kwanza tofauti na wasanii wengine wanavyofanya ili audio ipate nafasi yake na video ipate nafasi yake.

Picha: Belle 9 azindua video mpya ya wimbo wake wa ‘Give IT TO ME’

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Belle 9 akizungumza na waandishi wa habari
Mastaa wa muziki, filamu pamoja na viongozi wa serikali Jumamosi hii walipamba usiku wa uzinduzi wa video mpya ya Belle 9 ‘Give IT TO ME’.
Tafrija hiyo fupi ambayo iliandaliwa na kampuni ya muimbaji huyo,Vitamin Music Group Limited, iliwakutanisha wadau mbalimbali wa muziki pamoja na waandishi wa habari.
Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete ni mmoja kati ya viongozi wajuu waliohudhuria uzinduzi huo.
Akiongea katika uzinduzi huo, Belle aliishukuru team nzima ya Vitamin Music Group Limited kwa kufanikisha tukio hilo pamoja na wadau mbalimbali ambao walijitokeza usiku huyo kwa ajili ya kumsupport. Angalia picha.

Navy Kenzo wakiwa ndani ya nyumba
Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete akiteta jambo na Diwani wa kata ya Mwanga Kigoma, Baba Levo


Millard Ayo akishow love na mdau


Joh Makini akiwa na Mx Carter
Mbunge Ridhiwani Kikwete (kwanza kulia) akiwa na mmoja kati ya wafanyakazi wa Vitamin Music Group Limited (katikati) pamoja na Joh Sambila (kwanza kushoto)




Darassa Apata Ajali Kahama

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


 Muonekano wa gari alilopata nalo ajali ainaya Toyota Harrier

Habari zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa mwanamuziki wa Hip Hop Bongo ambaye anasumbua na ngoma yake kali ya Muziki, Sharrif  Thabit ‘Darassa’ amenusurika kifo baada ya kupata ajali mbaya maeneo ya Ntobo barabara ya kuelekea Mgodi wa Bullyanhulu Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga.

Habari zimeeleza kuwa ndani ya gari hilo aina ya Toyota Harrier  ambalo dereva hajajulikana, Darassa alikuwa ameambatana na director wake, Hanscana pamoja na producer wake, Abba Process na wote wametoka salama.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Darassa amethibitisha kupata ajali hiyo na alipopigiwa simu na na mtandao huu alisema hawezi kuongea kwa sasa hivyo atafutwe baadaye.

SAIDA KAROLI ADAI KUACHANA NA MENEJA WAKE KULIMFANYA APOTEZE MWELEKEO KWENYE MUZIKI

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Msanii mkongwe wa muziki wa asili, Saida Karoli amefunguka kwa kusema kuwa moja ya sababu ambayo ilimfanya apotee kwenye muziki ni kitendo cha kuachana na meneja wake.
Muimbaji huyo ambaye aliachana na meneja wake toka 2007, amedai kitendo hicho kilimfanya ashindwe kujisimamia na kumfanya ashuke kwenye muziki.

“Baada ya kuachana na meneja wangu sikuweza kujisimamia mimi mwenyewe na pia kwa wakati ule ilikuwa ni ngumu sana kwa sababu muziki una mambo mengi na mimi nimekulia kijijini kwahiyo kujua baadhi ya vitu ilikuwa ngumu sana,” Saida aliiambia BBC.

“Sina nilipo kosea lakini najua kila kitu chenye mwanzo hakikosi kuwa na mwisho, simaanishi huo ndo mwisho wangu ila kwa kuwa nilianza na mtu, sasa unapomalizana naye ni kama unaanza maisha mapya ndio kitu kilicho nitokea mimi,” aliongeza.
Pia muimbaji huyo amesema kwa sasa anajipanga kuja kwa kishindo na kufanya mapinduzi katika muziki wa asili nchini.

EATV yamtangaza Salama Jabir kuwa host wa EATV Award 2016

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Mtangazaji mahiri wa vipindi vya burudani nchini, Salama Jabir ametangazwa na EATV kuwa host wa tuzo za EATV Award 2016 ambazo zitafanyika Disemba 10 katika ukumbi wa Mlimani City.

Jumla ya tuzo 10 zinatarajiwa kukabidhiwa kwa wasanii wa muziki na filamu siku hiyo.

Kupitia twitter ya EATV, imeandika;

Tunamtambulisha kwako HOST EATV AWARDS 2016, mkali wa hizi kazi.
Salama Jabir

Moja kati kipengele ambacho kitakuwa na msisimko siku hiyo ni kipengele cha msanii bora wakiume ambacho Alikiba, FA, G-Nako, Shetta na Ben Pol wanapigana vikumbo kuondoka na tuzo hiyo.

TID – UHALISIA WA MUZIKI WA BONGOFLEVA UMEPOTEA

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Msanii mkongwe wa muziki wa bongofleva TID amedai uhalisia wa muziki huyo umepotea baaada ya baadhi ya wasanii kuiga muziki wa nje.
Akiongea katika kipindi cha Ubaoni cha EFM Alhamisi hii, TID amesema muziki wa bongofleva umetokana na mchanganyiko wa muziki wa hip hop na RnB.
“Uhalisia ya muziki wa bongofleva umepotea watu sasa hivi wanataka kuimba kama Wanigeria, watu wanataka kuiga vitu vya nje lakini wakumbuke kwamba bongofleva maana yake ni mchanganyiko wa muziki wa hip hop na RnB,” alisema TID.
Muimbaji huyo amesema aliamua kuandika wimbo ‘confidence’ ili kuwaonyesha vijana wanatakiwa kufanya nini kwenye nyimbo zao.
Katika hatua nyingine muimbaji huyo amesema anashangaa kuona waandaaji wa tuzo za muziki nchini kushindwa kutoa tuzo kwa msanii wenye mchango mkubwa kwenye muziki.
“Ni mara chache sana kwenye tuzo zetu kushuhudia tuzo za heshima zinatoka kwa ‘legends’ wa muziki wetu kutambua mchango wao, hata aliyeanzisha tuzo za muziki za Kilimanjaro marehemu James Dandu sijashuhudia akipewa heshima yake tuzo hizi zinapofanyika.” alisema TID.

SIKULIZA NA UDOWNLOSAN NYIMBO MPYA HA KELVIN BOSCO -HAPPY

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu. 



Msanii mpya wa muziki wa bongofleva, Kelvin Bosco ameachia wimbo yake mpya 'Happy'. Wimbo huo umeandaliwa na studio za Home Town chini ya producer Elly Da BWAY.

USHINDI WA KISHINDO WA WIZKID KWENYE MTV MAMA UTUAMSHE KUHUSU TUNAVYOZICHUKULIA TUZO

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Ushindi wa kishindo wa Wizkid kwenye tuzo za MTV MAMA mwaka huu, unanikumbusha wale wanafunzi wa kiume ambao huwa hawana time kabisa na wasichana wa darasani, lakini bado watamnasa kila demu mkali.

Wanafunzi wa aina hii ni wale ambao huwa na akili sana darasani au kwao mambo safi (wana mkwanja) – vitu viwili muhimu vinavyowadatisha madenti wa kike! Warembo hujipeleka wenyewe!
Tangu kutangazwa kwa majina ya wasanii watakaowania tuzo hizo mwaka huu, Wizkid hakuwahi kusema chochote. Alikuwa kimya tu utadhani hakuna kinachoendelea licha ya kuwepo kwenye vipengele vingi.
Hakuwa na muda wa kusema ‘thanks for the nomation.’ Hakuwa na hata muda wa kusema ‘jama eeh, mwenzenu nimetajwa kwenye MTV MAMA hebu nipigieni kura.’ He didn’t give a damn! Si ajabu lakini kwasababu ni kawaida yake bwa’mdogo huyu. Yeye tuzo huziona kitu cha kawaida, mpe sawa, mnyime, fresh tu!
Ehh! Jumamosi kaibuka na tuzo nne, kawa ‘man of the night.’ Unadhani ni kura ndizo zimempa ushindi wa tuzo zote hizo? Napata tabu kuamini. Msanii mmoja mkubwa sana ameniambia, namnukuu: Sometimes KURA zinapotosha. Watu wamepiga kazi nzuri ila kura zinapick wengine.”
Anachomanisha kuwa, msimamo wa Wizkid kutojishughulisha na kusema lolote kuhusu tuzo, kunaweza kukawa kulimfanya asipate kura nyingi kihivyo, lakini ukweli ni kwamba, hakuna msanii Afrika aliyefanya makubwa kumzidi Wizkid mwaka huu.
Alishirikishwa kwenye wimbo ‘One Dance’ wa Drake ambao umeweka rekodi kibao ikiwemo ya kusikilizwa mara bilioni 1 kwenye mtandao wa Spotify na kuwa wa kwanza kuwahi kuvutia namba hizo. Wizkid amefanya kazi na Chris Brown, Trey Songz, French Montana na wasanii wengine wakubwa. Ndio msanii anayefanyia kazi Afrika anayefahamika zaidi kwa sasa Marekani. Hata kama hakuonesha kuzitilia maanani tuzo hizo, ilikuwa ngumu kumkwepa.
Fundisho hapa ni kwamba, wingi wa kura unaweza usiwe na maana yoyote katika kumpata mshindi. Haiko sawa kwa namna yake ndio maana Eddy Kenzo amelalamika. Kwamba kama waandaji wanasisitiza watu wapige kura, lakini waliopigiwa kura nyingi hawapewi ushindi, ya nini kuwaambia watu wapige kura? Ni sawa na kampuni kutangaza ajira na kuwafanyia usaili baadhi ya waombaji huku ikiwa na watu wengine itakaowapa kazi.
Hatuna ulazima wa kujilaumu au kuumia sana au kuushusha muziki wetu. Wasanii waliotuwakilisha wamefanya kazi kubwa na ngumu kuipeperusha bendera ya Tanzania. Tusiwabeze, tuwape moyo na kuwaunga mkono bila kuchoka. Katika kipindi wanachohitaji zaidi support yetu, basi ni hiki.

Video: Kagera All Star Ft Baghdad - Inaanza Na Wewe (Tetemeko Kagera)

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.



DIAMOND KUMLIPA SAIDA KAROLI ASILIMIA 25 YA USAMBAZAJI WA NYIMBO YA "SALOME"

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Diamond amedai kuwa Saida Karoli atapata asilimia 25 ya mapato ya wimbo wa Salome.

Diamond amerudia baadhi ya vitu kwenye wimbo wake mpya ‘Salome’ aliomshirikisha Raymond kutoka kwenye wimbo wa ‘Maria Salome’ wa Saida Karoli uliotoka takribani miaka 16 iliyopita.
Akiongea na 255 ya Clouds FM Jumatatu hii, hitmaker huyo wa Kidogo amesema kuwa walizungumza na uongozi wa Saida Karoli na kumpatia kiasi cha fedha pamoja na asilimia 25 ya usambazaji wa wimbo huo.
“Kitu tulichokifanya kabla ya kurelease wimbo, tulizungumza na uongozi wake, tukawaambia tunafanya hiki na hiki na kuna kiasi pia tukakitoa ili kiende kwake halafu tukampa 25% ya kuisambaza nyimbo hiyo. Kila income ya usambazaji ikiwa inaingia katika huu wimbo, mama atakuwa anapata percent,” amesema Diamond.
Mpaka sasa video ya ‘Salome’ ya Diamond ina siku mbili tangu ilipoachiwa kwenye mtandao wa YouTube lakini imefanikiwa kutazamwa mara 659k.

DIAMOND NA DAVIDO BADO SANA KWA “SAAD LAMJARRED” MSANII WA AFRIKA ANAYEONGOZA KWA NYIMBO ZAKE KUTAZAMWA ZAIDI

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Saad Lamjarred ni msanii mkubwa wa Morocco, ambaye namba zake zinatisha – ni balaa kabisa. Hii ni kwa sababu macho mengi uwafuatilia wasanii wa Nigeria pamoja na wasanii wa Afrika ya Mashariki bili kutazama kwa upande wa Afika ya Kaskazini kwenye nchi kama Morroco, Misri na Algeria.
Kwanza ana followers milioni 3.5 Instagram. Hiyo inafuta kile tulichokuwa tunaamini kuwa, Davido ndiye mwanamuziki wa Afrika mwenye followers wengi zaidi kwenye mtandao huo (2.9m) akifuatiwa na Diamond (2.7m) huku Wizkid akiwa na 2.5m.
Video yake mpya, GHALTANA ilitoka August 25, lakini hadi sasa imeangaliwa kwa zaidi ya mara milioni 36. Kama hiyo haitoshi, video ya wimbo wake, LM3ALLEM iliyotoka May 2, 2015 ina zaidi ya views milioni 390.
LM3ALLEM uliingia kwenye kitabu cha Guinness World Record kwa kupata views milioni 100 ndani ya miezi mitatu. Ni video ya kiarabu iliyotazamwa kuliko zote.
Nyimbo zake “Mal Habibi Malou” na “Machi Sahel” zimevutia views milioni 161 na milioni 66 kwenye Youtube hadi sasa.

SHILOLE NA NUH MZIWANDA WAMALIZA BIFU LAO

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


Ilikuwa ni ‘break up’ iliyofuatiwa na uadui mkubwa. Ilipelekea hadi Nuh Mziwanda kuandika wimbo ‘Jike Shupa’ uliomlenga ex wake Shilole.

Haikuishia hapo, wawili hao waliendelea kurushiana maneno kwenye mitandao ya kijamii na kwenye mahojiano na kulaumiana kwa mengi. Hata hivyo mlalamikaji mkubwa alikuwa Nuh aliyemwelezea Shishi kama mwanamke aliyempotezea muda wake na kumkwamisha kwenye muziki.
Pia wimbo wa Shilole, Say My Name una mashairi yanayotaka kuhusiana na vunjiko la huba kati ya mastaa hao waliotengeneza vichwa vya habari wakiwa pamoja ikiwa ni pamoja na kujichora tattoo za majina yao.
Na sasa huenda wameamua kuyaacha yaliyopita yapite na wagange yajayo. Alhamis hii wawili hao waliweka picha zao kwenye Instagram kwa mara ya kwanza tangu waachane.

Akiweka picha ya Nuh kwenye akaunti yake ya Instagram, Shilole aliandika: God Bless You.

Naye Nuh alimweka Shishi kwenye akaunti yake na kuandika: Nakutakia kila la kheri mwanangu Mungu akuzidishie uendelee kutoboa katika Kazi yako.”

PICHA: DIAMOND AFANYA KUFURU KWENYE SHOW YAKE MERU NCHINI KENYA

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


 Diamond Platnumz ana miaka mingi ya kuvuna mapesa kutokana na show zake. Kutoka kwenye mapokezi yaliyovunja rekodi, Meru nchini Kenya hadi kuangusha show iliyohudhuriwa na makumi kwa maelfu ya mashabiki wenye kiu, staa huyo ameendelea kujiweka kwenye ligi yake mwenyewe.
 Ilikuwa ni show ya mtu mmoja na kwa picha alizoweka kwenye page yake ya Instagram, inaonesha jamaa alihama na kijiji. Tazama picha hapo chini.




TAZAMA HAPA VIDEO MPYA KALA JEREMIAH FT MIRIAM CHIRWA - WANANDOTO

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


TAMASHA KUBWA LA MUZIKI WA DANSI KUFANYIKA JUMAMOSI KATIKA VIWANJA VYA LEADERS JIJINI DAR

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.


 Mdau wa muziki wa dansi, Asha Baraka akizungumza katika mkutano huo kuhusu tamasha hilo la kukata na shoka ambalo alijawahi kufanyika hapa nchini.Picha na Geofrey Adroph
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akizungumza na wanamuziki hao kuhusu tamasha hilo la muziki wa dansi nchini.
Mwanamuzi wa mziki wa dansi, Ali Choki akiwaongoza wenzake kutoa burudani mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda walipofika ofisini kwake leo, kuzungumzia Tamasha la muziki huo litakalofanyika Jumamosi  Viwanja vya Leaders ambalo litashirikisha bendi 10 maarufu za hapa nchini.

Baadhi ya waandishi wakiwa kazini
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akiwa katika picha ya pamoja na wanamuziki wa dansi baada ya kuzungumza nao ofisi kwake.

SIKILIZA NA UDOWNLOAD NYIMBO MPYA YA KALA JEREMIAH FT. MIRIAM CHIRWA - "WANANDOTO"

Ndugu wasomaji wetu tunaomba support yenu kwa kutangaza nasi hapa kwenye hii blog kwa bei nafuu ili tuweze kuendelea kutoa habari bila tatizo lolote. Wasiliana nasi kupitia namba +255713363965 / +255755274953. Tunashukuru kwa ushirikiano wenu.