Kwa
siku nne sasa Iringa imekuwa na uhaba wa disel na petrol. Tatizo
linaripotiwa kuwemo katika sehemu nyingine za nchi. Jana nilishindwa
kabisa kupata mafuta Iringa. Nilikuwa na mafuta ya kuweza kunifikisha
Ilula tu.
Hapo nilidhani kungekuwa na kit
uo chenye mafuta.
Hapana! Bahati nzuri dereva wa basi la kwenda Uhambingeto aliweza kunisaidia kwa kuniuzia lita zake ishirini za dizeli. Zinifikisha Mikumi. Pale Mikumi nikafanikiwa kupata mafuta ya kununua kituoni. Vinginevyo, kwa mara ya kwanza jana nimelazimika kununua mafuta ya ' kulanguliwa'. Lita moja kwa shilingi elfu tatu. Hakyamungu!
Hapana! Bahati nzuri dereva wa basi la kwenda Uhambingeto aliweza kunisaidia kwa kuniuzia lita zake ishirini za dizeli. Zinifikisha Mikumi. Pale Mikumi nikafanikiwa kupata mafuta ya kununua kituoni. Vinginevyo, kwa mara ya kwanza jana nimelazimika kununua mafuta ya ' kulanguliwa'. Lita moja kwa shilingi elfu tatu. Hakyamungu!
Songea
Mjini Singida
Askari polisi wa mjini Singida akisimamia ugawaji wa petrol jana (29/10/2012) kwenye kituo cha mafuta cha Esso.
Baadhi
ya wafanyabiashara wa bodaboda mjini Singida,wakiwa kwenye foleni jana
(29/10/2012) wakisubiri kuuziwa petrol.Kwa zaidi ya wiki tatu,kumekuwa
na uhaba mkubwa wa nishati ya mafuta kitendo ambacho kimeathiri shughuli
nyingi za kiuchumi kwa wakazi wa mji wa Singida na vitongoji
vyake.
No comments:
Post a Comment