Viongozi mbalimbali wa Chuo Kikuu Cha Dodoma Kuanzia Makamu Mkuu wa Chuo
Prof. Idrisa Kikula, Naibu Makamu Mkuu wa Elimu,Utafiti na Ushauri Prof
Ludovick Kinabo na Naibu Makamu Mkuu Mipango,Fedha na Utawala Prof
Shabani Mlacha,Dean wa collage ya Social Science, Wafanyakazi wa Chuo Kikuu Cha Dodoma, Pamoja na
Wanafunzi wa Kozi Mbalimbali leo wamehudhuri Kuaga Mwili wa Marehemu wa
Aliyekuwa Mhadhiri wa Chuo Kikuu Cha Dodoma (UDOM) Mh Deogratius
Camillius ambaye amefariki alfajili ya tarehe 24/10/2012 kwa Mshtuko
wakati akiangalia Mpira na Jamaa zake.
Baadhi ya Ndugu, Jamaa wa Marehemu wakiaanda kwaajili ya Kuaga Mwili wa Marehemu
Ibada ya Kuombea Mwili wa Marehemu
Deogratius Camillius ikiendelea huku waombolezaji wakiwa mbele ya jeneza
alilolazwa marehemu wakati wa ibada nyumbani kwake kisasa mjini Dodoma
leo. Kabla mwili wake haujasafirishwa kupelekwa Mkoani Morogoro
Kwaajili ya Mazishi.
Baadhi ya waombolezaji wakiwa katika majonzi na mshangao wa hali ya juu kwani iliwachukua muda mrefu sana kuamini kilichotokea
Kiongozi wa Dini akiendelea kuongoza Ibada ya Kumuombea Marehemu kabla
mwili wake haujasafirishwa kuelekea Morogoro kwaajili ya Mazishi
Jamaa na marafiki wakiaga mwili wa marehemu Kabla mwili wake haujasafirishwa kupelekwa Mkoani Morogoro
Kwaajili ya Mazishi.
Baadhi ya waombolezaji wakiwa katika majonzi
Mmoja wa viongozi wa UDOMASA MR MKANACHI akitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya UDOMASA
Principal wa College ya Social
Science and Humanities Prof. Casmir
Rubagumya akitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya Uongozi na
Wafanyakazi wa Chuo Kikuu Cha Dodoma leo katika msiba uliofanyika
Nyumbani Kwa Marehemu Mjini Dodoma kabla ya Mwili wake haujasafirishwa
kupelekwa Mkoani Morogoro kwaajili ya Mazishi.
Baadhi ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu Cha Dodoma, Ndugu, Jamaa na Marafiki
waliojitokeza kwenye Msiba wa Marehemu Deogratius Kamillius ambaye
amefariki leo majira ya asubuhi wakati akiwa hospitalini
Jeneza lililobeba mwili wa marehemu DEOGRATUS KAMILIUS likipandishwa
kwenye gari tayari kwa kusafirishwa kuelekea mkoani morogoro kwa ajili ya mazishi
Gari lililobeba Mwili wa Marehemu Deogratius Kamilius Likiwa tayari
kwaajili ya Safari ya Kuelekea Mkoani Morogoro kwaajili ya Mazishi.
Picha
Na Sulemani Magoma wa Lukaza Blog
BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA JINA LAKE LIHIMIDIWE.
CHANZO: LUKAZA BLOG
No comments:
Post a Comment