HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » KUNA KITU GANI KILICHOFICHIKA NDANI YA MAFUTA; KAMPUNI ZA MAFUTA ZASHUKIWA


Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Haruna Masebu, akifafanua jambo.

Katibu  Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Eliakimu Maswi, amezishukia Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura), na Bodi inayoratibu Mfumo wa Uingizaji wa Mafuta Nchini (Pic) kwa kushindwa kuwajibika katika tatizo la ukosefu wa mafuta.
Alisema hakuna sababu za msingi za kuwepo kwa uhaba wa mafuta ya petroli, dizeli na taa, wakati kuna akiba ya kutosha ya nishati hiyo nchini.
Maswi alisema hayo jana baada ya kuitisha mkutano wa waandishi wa habari kutoa ufafanuzi kufuatia kukosa mafuta katika mikoa kadhaa nchini wakati kuna akiba ya zaidi ya lita milioni 83 za mafuta.
Mkurugenzi wa Petroli Ewura, Godwin Samweli, alisema mafuta yapo ya kutosha, lakini tatizo lipo kwa wenye kampuni zilizopewa leseni za kuuza mafuta hayo nchini.
“Wenye makampuni wanakataa kuwauzia wenye vituo binafsi mafuta baada ya kusikia taarifa ya kukwama kwa meli zinazoleta mafuta hayo nchini,” alisema.
Naye Mkurugenzi wa Pic, Mansoor Hiran, alisema tatizo hilo linatokana na wakubwa kujiuzia wenyewe na kwamba wao hawana mamlaka ya kuzilazimisha kampuni zinazonunua mafuta kupeleka mikoani bali Ewura ndio wenye mamlaka hayo.
Maswi aliiagiza Ewura kuzichukulia hatua za kisheria kampuni zenye leseni zinazokataa kuuza mafuta kwa wamiliki wavituo vya binafsi.
Alisema mafuta yaliyopo nchini yanatosha kwa matumizi ya siku tano hadi saba na lita milioni 60.8 zimehifadhiwa  kwenye maghala ya TIPER kwa ajili ya soko la ndani na nje ya nchi.
CHANZO: NIPASHE

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: