HABARI

Theme images by kelvinjay. Powered by Blogger.

MATUKIO

MICHEZO

SIASA

» »Unlabelled » Polisi, mgambo waua watu wanne katika vurugu za wamachinga

Matairi yakiwashwa moto wakati wa vurugu za wamachinga waliokuwa wakipinga kitendo cha kuhamishwa kinguvu eneo wanalofanyia biashara jijini Mwanza.
Mtaa wa Nyerere ukiwa na watu wachache wakati wa vurugu hizo
Askari wakilinda doria katika vurugu hizo
Gari likiwaka baada ya kuchomwa moto na wamachinga katika vurugu zilizotokea jijini Mwanza, baada ya Polisi kuwatimua katika eneo la kufanyia biashara wanalodai walitengewa. (PICHA ZA BLOGU YA SENGO)
 Vurugu kubwa zimeibuka katika Jiji la Mwanza kati ya wafanyabiashara wadogo wadogo maarufu wamachinga na mgambo wa jiji hilo na kusababisha mtu mmoja kupoteza maisha kwa kupigwa risasi.

Aidha, Polisi jijini Mwanza wameua watu watatu wanaodaiwa kuwa ni majambazi katika tukio la kurushiana risasi.


Mtu huyo aliyeuwawa kwa kupigwa risasi amefanya jumla ya idadi ya watu waliuwawa mkoani hapa katika matukio  tofauti kufikia wanne.


Kaimu  Kamanda  wa Polisi Mkoani Mwanza, Lily  Matola, akizungumza na waandishi wa habari jana, alisema katika tukio la vurugu za mgambo na wamachinga, mbali na kifo hicho watu wawili wamejeruhiwa kwa kupigwa risasi.


Alisema katika tukio hilo ambalo lilitokea jana, aliyeuawa ni mpigadebe mmoja ambaye jina lake wala makazi yake havijatambuliwa.


Kamanda Matola alisema katika vurugu hizo, wamachinga wawili walijeruhiwa kwa kupigwa risasi na wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando.


Alisema vurugu hizo ziliibuka jana kati ya saa 5 :00 asubuhi na 6:00 mchana muda mfupi baada ya mgambo wa mgambo hao walipokwenda eneo hilo kwa ajili ya kuendesha operesheni ya kuwaondoa wamachinga katika maeneo yasiyoruhusiwa kufanyabiashara na ndipo kukazuka mapigano.


Kamanda Matola alisema mgambo hao wakiwa eneo hilo wamachinga walianza kuwarushia mawe na katika kujiokoa, mgambo hao walianza kupiga risasi hewani na risasi moja ilimpata mpigadebe ambaye alifariki papo hapo.


Aliongeza kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando.

 
Kamanda Matola alisema kufuatia vurugu hizo, polisi wanawashikilia mgambo watatu huku wenzao  wawili  wakiwa  wamejeruhiwa vibaya na wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando.

Katika tukio lingine, watu watatu wanaosadikiwa kuwa majambazi wameuawa kwa kupigwa risasi katika eneo la Big Bite  lililopo Kilimahewa, Wilaya ya Ilemela jijini hapa.


Kwa mujibu wa Kamanda Matola, watuhumiwa hao ambao  hadi sasa  bado majina yao hayajatambuliwa, waliuawa  kwa kupigwa risasi, kati ya majira ya saa 4:00 na saa 5:00 juzi usiku.


Kamanda Matola alisema polisi waliokuwa katika doria, ghafla baada ya kuwashtuakia, kulizuka mapambano ya kurushia risasi kati ya majambazi hao na polisi.


Alisema majambazi hao walikuwa na bunduki  aina ya SMG  yenye namba za usajili T1964TB8799 ikiwa na risasi 43.


Kamanda Matola alisema wakati wa mapambano hayo, hakuna askari aliyejeruhiwa.


Alisema miili  ya majambazi hayo imehifadhiwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti  cha  Hospitali ya Rufaa ya Bugando.


Aliongeza kuwa Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi zaidi wa tukio hilo.



«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments: