Mwenyekiti wa kanisa la Moravian Jimbo la Misheni Mashariki Mch. Clement
 Fumbo akitangaza Halmashauri mpya ya kanisa hilo itakayokaa madarakadi 
hadi sinodi ya mwaka 2014 
            
HALI si shwari tena katika Kanisa la Moravian 
Jimbo la Misheni Mashariki kutokana na Mwenyekiti aliyesimamishwa 
uongozi na Mkutano Mkuu wa Jimbo (Sidodi), Mchungaji Clement Fumbo 
kujichukulia madaraka na kutangaza uongozi wake mpya.
Fumbo alitangaza uongozi huo juzi katika ibada 
iliyofanyika katika Kanisa la Moravian Ushirika wa Tabata akieleza kuwa 
uongozi wa juu wa kanisa unamtambua kuwa yeye ndiye mwenyekiti wa kanisa
 katika jimbo hilo la Misheni.
Wakati hayo yakijiri sintofahamu imebakia kwa 
waumini kuwa hivi sasa waufuate uongozi upi wa mwenyekiti 
aliyesimamishwa na sinodi ama Makamu Mwenyekiti Sauli Kajura aliyepewa 
mamlaka ya kuliongoza jimbo hadi kipindi cha mkutano mkuu wa uchaguzi 
utakaofanyika mwaka 2014.
Kutangazwa kwa uongozi huo wa kanisa kumejiri 
wakati pia kesi ikiendelea katika Mahakama ya Kisutu ambapo Mchungaji 
Fumbo alifungua kesi ya kupinga uamuzi wa Sinodi akieleza kuwa 
hakuhusika na upotevu wa Sh 500m hali iliyosababisha avuliwe uongozi huo
 kupitia sinodi ya dharura.
Akielezea hisia zake kwa waumini wa Ushirika wa 
Tabata, Mchungaji Fumbo alisema ameamua kuunda uongozi mpya wa jimbo ili
 shughuli za kitendaji zisiweze kuendelea baada ya makamu mwenyekiti 
,katibu na miongoni mwa wajumbe wa Halmashauri Kuu kusababisha mpasuko 
kati ya waumini na wachungaji.
Mchungaji Fumbo alisema Juni 5, mwaka 2012 
yalifanyika mapinduzi ya kumwondoa madarakani yeye  watendaji, na baadhi
 ya Wakristo kutengwa huku wachungaji wakitishiwa maisha kinyume na 
taratibu za kanisa hilo.
Alisema jambo hilo lilisababisha mgawanyiko ndani 
ya kanisa kwa ngazi ya viongozi na kuambukiza wachungaji na walei wa 
kanisa la jimbo hilo hata kwenye majimbo mengine ambayo yana masilahi na
 jimbo hilo.
Fumbo alisema Kanisa la Moravian Duniani 
(COUF)kupitia kwa mwakilishi wake umeingilia kati na kutuma ujumbe wake 
ambao ulikuwa Novemba 25,26, na 27 mwaka 2012 kwa lengo la kutafuta 
kiini cha mgogoro ili kupendekeza suluhisho lake.
“Katika mikutano yake ya tume iliona njama za 
makusudi za kumpindua mwenyekiti kwa njia isiyo halali kwa sababu 
zisizojulikana, ukiukwaji wa maadili ya uongozi na Katiba ya Kanisa la 
Moravian (COUF) na katiba ya Jimbo la Mashariki,”alisema na kuongeza:
“Kutokana na hayo tume imeagiza yawepo mazungumzo 
ya pande mbili yanayolenga kurudi kwenye mfumo wa uongozi wa mwaka 2010 
na kufuata taratibu za mambo yaliyosababisha kukosa maelewano na 
uchunguzi wa kina ufanyike kubaini kiini cha tatizo,”alisema Fumbo.
Alisema msuluhishi wa Kanisa la Moravian Duniani 
(COUF) alinyimwa ushirikiano kutoka kundi la Makamu Mwenyekiti na Katibu
 wake ambapo hawakutaka kusuluhishwa ili mgogoro umalizike.
Alisema kwa kuwa kanisa linahusu imani za watu kwa
 kuzingatia kwamba uongozi uliochaguliwa mwaka 2010 ukiwa chini ya 
mwenyekiti Fumbo haujamaliza muda wake mwaka 2014 ambapo ukizingatia 
yalifanyika mapinduzi ya kuondoa baadhi wa viongozi wa jimbo hilo 
(HAIJAMALIZIKA)
MWANANCHI
MWANANCHI



No comments:
Post a Comment